Anayekutawala amekuzidi Akili

Mtu kama hana akili hawezi kukutawala.
Akili anakuwa nayo ndio ila si lazima awe anakuzidi akili japo anaweza pia akawa anakuzidi akili. Kikubwa hapa ni nguvu; kwamba mnyonge hawezi kumtawla mwenye nguvu isipokuwa mwenye nguvu ndiye aliye na uwezo wa kumtawala mnyonge
 
ANAYEKUTAWALA AMEKUZIDI AKILI

Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli.

Ukiona mtu amekuzidi na kukutawala kisiasa, kiuchumi, kijamii au kiteknolojia basi fahamu kabisa mtu au jamii hiyo imekuzidi Akili.

Akili ndio inayotawala mambo yote duniani. Ili upewe Mamlaka na nguvu basi lazima uwe na akili kuwashinda wengine hasa hao unaowatawala.

Kijinsia, Mwanaume anaakili kuliko Mwanamke ndio maana anamtawala. Ingawaje zipo siasa na porojo za kuwafariji wanawake kuwa wanaakili kuwashinda wanaume lakini kiuhalisia Mwanaume anaakili zaidi kuliko Mwanamke. Ndio maana Mwanaume anamtawala Mwanamke.

Kijamii, Wazungu na jamii zao wanaakili kushinda Waafrika, na Waarabu na wachina na jamii zingine. Ndio maana wazungu miaka nenda rudi wanatawala huu ulimwengu.

Kuna ile kujidanganya kuwa utawala ni majaliwa lakini hata hiyo akili yenyewe ni Majaliwa. Kila kitu kwenye maisha ni Majaliwa.

Wanyama wa porini tunawatawala kwa sababu ya sisi kuwashinda kiakili.
Huwezi tawala kitu ambacho kimekuzidi Akili hiyo haiwezekani na haitakuja kutokea.

Elewa kuwa wewe unaakili nyembamba au ndogo ndio maana unatawaliwa, na ndio maana wewe sio mtawala. Ingawaje unaweza na unaruhusiwa kujifariji kuwa umewazidi waliokutawala akili hiyo haibadilishi chochote kuwa wewe kiakili upo Chini.

Kama nitaulizwa ni kwa nini CCM mpaka leo inatawala mpaka leo basi moja kwa moja nitakuambia kuwa CCM inaakili kuliko vyama vingine. Yaani Watu wa ccm(inawezakuwa isiwe wote) wanaakili kuliko vyama vingine.
Haiwezekani kila mpambano na kila uchaguzi CCM ishinde tuu. Hiyo ni kuonyesha kuwa wanaakili kuwashinda wapinzani wao.

Watu wajinga hupenda kutoa visingizio katika kushindwa au pale wanaposhindwa na wenye Akili.
Sijui polisi, sijui wanatumia vyombo vya Dola, sasa kwa nini ninyi msitafute akili ya kupata ushawishi kwenye hivyo vyombo vya Dola kama mnajua kuwa kuna wakati ili mpate ushindi basi vyombo vya dola vinaweza kuwasaidia. AKILI.

Unakuta mtu anajiona anaakili kuliko Boss wake. Mpaka unamshangaa. Hiyo ni dalili ya kuchanganyikiwa. Huwezi kuwa na akili zaidi ya mtu ambaye amekuzidi na amekutawala katika uchumi alafu useme unamzidi akili za uchumi.

Kwenye Vita baina ya Israel na Palestina, watu wajinga na wenye upeo mdogo wanakataa kuwa Israel haina Akili na utawala wake unatokana na Kusaidiwa na Marekani. Yaani kama sio Marekani basi Israel haiiwezi Palestina na Waarabu. Unakuja kugundua kuwa wanaosema hivyo upeo wao upo chini katika kuyachambua mambo.

Hawajiulizi mbona Ukraine inasaidiwa na Marekani, na nchi za Nato lakini Inashindwa mbele ya Urusi. Hawajiulizi hivyo kwa sababu hawajui kuwa Akili ndogo haiwezi kuishinda akili kubwa.
Urusi ni akili kubwa hivyo inapokutana na Ukraine hapo ni lazima Ukraine ashindwe tuu bila kujali huyo Ukraine atasaidiwa na Marekani au Nato.

Wewe kama unajua ili ushinde unatakiwa ufanye moja mbili tatu. Kwa nini usifanye hizo moja mbili tatu.
Mshindani wako akikushinda unaleta visingizio.
Ooooh! Fulani kaenda kwa waganga wa kienyeji, sijui anauza madawa ya kulevya, ndio maana anapesa, pesa za wizi zile.
Hivi kwa ujinga wako unafikiri hata huo Wizi au kuuza madawa ya kulevya hakuhitaji AKILI?

Nenda nawe ukauze au kaibe ili ujue huyo mwenzako amekuzidi Akili na atakutawala kwa ufinyu wa akili yako.

Elewa kuwa Akili ni akili tuu. Bila kujali ni Akili ya uadilifu au akili ya uhalifu. Kutawaliwa ni kutawaliwa tuu iwe unatawaliwa kwa Haki au kwa haramu.

Jambo moja nalotaka kusema ni kuwa, ukishindwa kubali umeshindwa, kukubali kushindwa ni mwanzo wa kujitambua na unaweza kujua wapi pakuanzia.
Lakini kujifanya unauwezo wakati uwezo huo huna na kama ungekuwa nao usingeshindwa ni dalili ya kutojitambua.

Mimi nimemaliza,

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Pengine una maanisha "ujasiri" = Being brave enough to...., na sio "Akili" = inteligence/cleverness.

Kwa baadhi ya mambo neno FATE = Majaliwa, linaweza kufit zaidi maelezo yaliyotolewa (mf. Historia ya Chifu Mkwawa).

Neno akili lina ukomo kwa vile baadhi ya mifano iliyotolewa haifui dafu kwa kundi kubwa la viumbe waliojipanga kutawala/kushinda kundi dogo hata kama lina akili kiasi gani.
Mfano, kundi la simba porini likimuua tembo limesaidiwa na:
-wepesi wa mwili
-Aina ya meno na makucha waliyoumbiwa (tearing)
-Msukumo (urge) wa njaa na mahitaji ya chakula chake (Carnival)

Tembo akiuawa ni kwa sababu:
-Ukubwa wa mwili, sio rahisi kujificha au kubadili uelekeo
-Naturally yeye ni chakula cha wanyama walao nyama,
-n.k.
Je unataka kusema Sadam Hussein au Osama walizidiwa akili na Taifa la Marekani?
Anyway, nakubaliana na mtoa mada kwamba, akili ina mchango mkubwa kutawala jambo lolote tena bila kutumia nguvu. Bali tusisahau nguvu iliyomo kupitia ulaghai, timing na mifumo.
 
Pengine una maanisha "ujasiri" = Being brave enough to...., na sio "Akili" = inteligence/cleverness.

Kwa baadhi ya mambo neno FATE = Majaliwa, linaweza kufit zaidi maelezo yaliyotolewa (mf. Historia ya Chifu Mkwawa).

Neno akili lina ukomo kwa vile baadhi ya mifano iliyotolewa haifui dafu kwa kundi kubwa la viumbe waliojipanga kutawala/kushinda kundi dogo hata kama lina akili kiasi gani.
Mfano, kundi la simba porini likimuua tembo limesaidiwa na:
-wepesi wa mwili
-Aina ya meno na makucha waliyoumbiwa (tearing)
-Msukumo (urge) wa njaa na mahitaji ya chakula chake (Carnival)

Tembo akiuawa ni kwa sababu:
-Ukubwa wa mwili, sio rahisi kujificha au kubadili uelekeo
-Naturally yeye ni chakula cha wanyama walao nyama,
-n.k.
Je unataka kusema Sadam Hussein au Osama walizidiwa akili na Taifa la Marekani?
Anyway, nakubaliana na mtoa mada kwamba, akili ina mchango mkubwa kutawala jambo lolote tena bila kutumia nguvu. Bali tusisahau nguvu iliyomo kupitia ulaghai, timing na mifumo.

Hata binadamu ni chakula kwa wanyama kama Chafu, chui, mamba, Simba n.k.
Kutokuliwa kwa wanyama kunatokana na uwezo wake wa kujilinda, Akili.

Simba atamuua tembo kutokana na Akili. Uwezo wa akili za simba ambao unawafanya kushirikiana ndio kunakowafanya wamshinfe tembo. Wanajua bila kushirikiana hawana uwezo wa kumshinda tembo. Hiyo ni Akili.
Simba meno yake hayana nguvu kubwa (bite strength) ukilinganisha Mamba, Tiger na Fisi.
Pia simba hana nguvu wala uzito kumshinda Tembo, kifaru na nyati. Ila akili na ujasiri amewazidi hao wote.

Ndio maana simba anaitwa mfalme wa nyika.

Sadaka Hussein na Osama Bin Laden walizidiwa karibu kila kitu na Marekani sio tuu Akili bali hata Nguvu, ushawishi, pesa n.k.
 
Akili anakuwa nayo ndio ila si lazima awe anakuzidi akili japo anaweza pia akawa anakuzidi akili. Kikubwa hapa ni nguvu; kwamba mnyonge hawezi kumtawla mwenye nguvu isipokuwa mwenye nguvu ndiye aliye na uwezo wa kumtawala mnyonge

Nguvu za nini?
Kama ni nguvu za mwili basi umekwama.
Wenye miili mikubwa wengi wanatawaliwa na wenye miili midogo midogo. Na wengi ni vibarua. Wanatumikishwa.

Akili ndio inayoongozwa hata huo mwili wako.
 
Aisee niliwaambia wanafunzi wangu kuwa wasimcheke mwanafunzi mfupi na mwembamba ila watazame kichwani kujua kabeba Nini ili wasimcheke boss wao wa kesho
 
[QUOTE="Robert Heriel Mtibeli, post: 48243606,

Kushindwa kujinasua individually kwenye situation fulani kwa kukosa nyenzo au sapoti ya society, hakumaanishi wewe hauna akili.

Yafaa nini uki-demonstrate akili zako ukaishia kupotea mazima? Ushahidi wa hizo akili utatoka wapi?
 
ANAYEKUTAWALA AMEKUZIDI AKILI

Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli.

Ukiona mtu amekuzidi na kukutawala kisiasa, kiuchumi, kijamii au kiteknolojia basi fahamu kabisa mtu au jamii hiyo imekuzidi Akili.

Akili ndio inayotawala mambo yote duniani. Ili upewe Mamlaka na nguvu basi lazima uwe na akili kuwashinda wengine hasa hao unaowatawala.

Kijinsia, Mwanaume anaakili kuliko Mwanamke ndio maana anamtawala. Ingawaje zipo siasa na porojo za kuwafariji wanawake kuwa wanaakili kuwashinda wanaume lakini kiuhalisia Mwanaume anaakili zaidi kuliko Mwanamke. Ndio maana Mwanaume anamtawala Mwanamke.

Kijamii, Wazungu na jamii zao wanaakili kushinda Waafrika, na Waarabu na wachina na jamii zingine. Ndio maana wazungu miaka nenda rudi wanatawala huu ulimwengu.

Kuna ile kujidanganya kuwa utawala ni majaliwa lakini hata hiyo akili yenyewe ni Majaliwa. Kila kitu kwenye maisha ni Majaliwa.

Wanyama wa porini tunawatawala kwa sababu ya sisi kuwashinda kiakili.
Huwezi tawala kitu ambacho kimekuzidi Akili hiyo haiwezekani na haitakuja kutokea.

Elewa kuwa wewe unaakili nyembamba au ndogo ndio maana unatawaliwa, na ndio maana wewe sio mtawala. Ingawaje unaweza na unaruhusiwa kujifariji kuwa umewazidi waliokutawala akili hiyo haibadilishi chochote kuwa wewe kiakili upo Chini.

Kama nitaulizwa ni kwa nini CCM mpaka leo inatawala mpaka leo basi moja kwa moja nitakuambia kuwa CCM inaakili kuliko vyama vingine. Yaani Watu wa ccm(inawezakuwa isiwe wote) wanaakili kuliko vyama vingine.
Haiwezekani kila mpambano na kila uchaguzi CCM ishinde tuu. Hiyo ni kuonyesha kuwa wanaakili kuwashinda wapinzani wao.

Watu wajinga hupenda kutoa visingizio katika kushindwa au pale wanaposhindwa na wenye Akili.
Sijui polisi, sijui wanatumia vyombo vya Dola, sasa kwa nini ninyi msitafute akili ya kupata ushawishi kwenye hivyo vyombo vya Dola kama mnajua kuwa kuna wakati ili mpate ushindi basi vyombo vya dola vinaweza kuwasaidia. AKILI.

Unakuta mtu anajiona anaakili kuliko Boss wake. Mpaka unamshangaa. Hiyo ni dalili ya kuchanganyikiwa. Huwezi kuwa na akili zaidi ya mtu ambaye amekuzidi na amekutawala katika uchumi alafu useme unamzidi akili za uchumi.

Kwenye Vita baina ya Israel na Palestina, watu wajinga na wenye upeo mdogo wanakataa kuwa Israel haina Akili na utawala wake unatokana na Kusaidiwa na Marekani. Yaani kama sio Marekani basi Israel haiiwezi Palestina na Waarabu. Unakuja kugundua kuwa wanaosema hivyo upeo wao upo chini katika kuyachambua mambo.

Hawajiulizi mbona Ukraine inasaidiwa na Marekani, na nchi za Nato lakini Inashindwa mbele ya Urusi. Hawajiulizi hivyo kwa sababu hawajui kuwa Akili ndogo haiwezi kuishinda akili kubwa.
Urusi ni akili kubwa hivyo inapokutana na Ukraine hapo ni lazima Ukraine ashindwe tuu bila kujali huyo Ukraine atasaidiwa na Marekani au Nato.

Wewe kama unajua ili ushinde unatakiwa ufanye moja mbili tatu. Kwa nini usifanye hizo moja mbili tatu.
Mshindani wako akikushinda unaleta visingizio.
Ooooh! Fulani kaenda kwa waganga wa kienyeji, sijui anauza madawa ya kulevya, ndio maana anapesa, pesa za wizi zile.
Hivi kwa ujinga wako unafikiri hata huo Wizi au kuuza madawa ya kulevya hakuhitaji AKILI?

Nenda nawe ukauze au kaibe ili ujue huyo mwenzako amekuzidi Akili na atakutawala kwa ufinyu wa akili yako.

Elewa kuwa Akili ni akili tuu. Bila kujali ni Akili ya uadilifu au akili ya uhalifu. Kutawaliwa ni kutawaliwa tuu iwe unatawaliwa kwa Haki au kwa haramu.

Jambo moja nalotaka kusema ni kuwa, ukishindwa kubali umeshindwa, kukubali kushindwa ni mwanzo wa kujitambua na unaweza kujua wapi pakuanzia.
Lakini kujifanya unauwezo wakati uwezo huo huna na kama ungekuwa nao usingeshindwa ni dalili ya kutojitambua.

Mimi nimemaliza,

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Ndugu kumbuka utawala ni mfumo, mtawala ni mtu aliye ndani ya mfumo.
 
Kuna utawala wa mabavu na utawala wa akili au vyote kwa pamoja.

Hata hivyo, kipimo kizuri zaidi cha akili ni uwezo wa ku- survive.

Kipimo hiki kinajifunua kupitia umahiri wa kubadilika kwenda na nyakati na mazingira, na wala sio mabavu au akili kama inavyopimwa darasani.
 
Back
Top Bottom