ukiona unaitwa kwenye fursa wewe ndiye fursa mwenyewe..... Binafsi kuna mdau alitaka kuniunga huko lakini nikaanza kuona makando kando kwenye hizo presentation zao,
1. hawataki ushee na mtu information zao, kama umepata anaejiunga umpeleke pale wao watampiga darasa, hapa nilidoubt
2. bidhaa zao wanauza ghali sana, seriously na huu msoto wa bongo ninunue saa mil 2 ? si bora niende huko kibaha ndan ndan ninunue heka moja ?
3.wanapenda kujisifia sifia sana mara flani kanunua gari)wao kwa wao), mara ooh tunalipwa kwa dola sijui nini, lengo ni kukupa moto ili na wewe ujiunge fasta...
ukijiunga sijui na wewe utafute watu wajiunge kupitia wewe, ndio upate kamisheni, chain iendelee hivo hivo...
niliwahi kuhudhuria presentation moja ya forever miaka michache ilopita, sikupendezwa naona wanafanana japo huku amna kiingilio kama forever na huku amna kuuza bidhaa bali unanunua ukatumie mwenyewe....
kwa kifupi nimeona ni ubabaishaji tu amna lolote, za kuambiwa changanya na zako hamna hela rahisi