Anayefahamu kuhusu biashara ya Q-Net

Anayefahamu kuhusu biashara ya Q-Net

kajojo

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2012
Posts
2,946
Reaction score
5,487
Naomba kuwauliza wana Jf kama kuna mtu amesha wahi kusikia lolote kuhusiana na hii biashara ya Q-NET anielezee. Kwasababu hivi karibuni kuna ndugu yangu ameniomba nimkopeshe hela kias cha shilingi milioni moja ili aweze kujiunga na hii bishara.

Nilitaka kujua kwanza inahusiana na nini. Alini elezea kifupi kwamba ni biashara unayo jiunga kwa kiasi cha shilingi milioni 3 ambapo ukisha jiunga kuna points unapata za kuanzia, na pia kuna products mbalimbali kama elimu, holidays, kununua vitu kama saa na vingine.

Sasa ishu ni kwamba mimi nna wasiwasi na hiyo biashara yenyewe wanaiita Q-NET, sijawahi isikia mahali na nahisi ni kama hizi biashara nyingine kama za kina Rifaro na kina GNLD na forever living
na pili sina uhakika kama ataweza nirudishia hiyo pesa pindi itakapo gundulika kama ni utapeli.

Nimejaribu kumshauri aachane nayo lakini amekua akisisitiza nimpatie hiyo pesa kwasababu ni biashara itakayo imlipa Vizuri na atanirudishia ndani ya mwezi mmoja.

Naomba mwenye ufahamu wa hii business inayo fahamika kama Q-NET anifafanulie.
 
Hiyo biashara sista angu ameshaingia na ananishawishi kujiunga lkn mambo yangu wakati huu ni mabaya. Kifupi unahitaji capital ya kama 3m au zaidi kununua products zao zinaweza kuw saa au holiday package. Ukishanunua unakuwa member, sasa ili uweze kupata commission inakubidi na wewe ulete wenzako wawili. Sista ameniambia kuna watu wanapokea kamisheni kwa mwezi mpaka $3000 (dola elfu tatu), hata yeye amedai ameshaanza kupokea kamisheni yake. Yaani ukishajiunga, na ukafanikiwa kuinvite wenzako wawili au zaidi, kazi pekee kwako ni kuendesha semina kwa members wapya, yaani utapangiwa tarehe na venue kwa ajili ya kuwaelekeza. Ukiweza hivyo basi utajiri nje nje yaani mpunga utakuwa unaingia kila mwezi tu.
Note: Hayo niliyosema nimeelezewa na sista lkn bado sijaprove, kama kuna mtu ambaye tayari ni member aje atuthibitishie
 
Hizi biashara zimeshamiri sana, ukihesabu vizuri mahesabu yao unapata majibu haya
EITHER ni
1:wezi
2:Ni satanic link, why
?
jaribu kukokotoa chain nzima na monthly salary utaona kuna pesa itazid within a company ambayo hupati jibu inatoka wapi?.
3ml.Kubwa sana usawa huu ukiwekeza kwenye kilimo
 
Hizi biashara zimeshamiri sana, ukihesabu vizuri mahesabu yao unapata majibu haya
EITHER ni
1:wezi
2:Ni satanic link, why
?
jaribu kukokotoa chain nzima na monthly salary utaona kuna pesa itazid within a company ambayo hupati jibu inatoka wapi?.
3ml.Kubwa sana usawa huu ukiwekeza kwenye kilimo

ASANTE KWA USHAURI
 
Hizi biashara zimeshamiri sana, ukihesabu vizuri mahesabu yao unapata majibu haya
EITHER ni
1:wezi
2:Ni satanic link, why
?
jaribu kukokotoa chain nzima na monthly salary utaona kuna pesa itazid within a company ambayo hupati jibu inatoka wapi?.
3ml.Kubwa sana usawa huu ukiwekeza kwenye kilimo

ASANTE KWA USHAURI
 
Nimesikia kuwa hii ni business networking organization na watu wanapiga mkwanja wakutosha huko. Naomba kama kuna anayeifahamu hii atujuze kwa maslahi ya wengi.
 
Nimesikia kuwa hii ni business networking organization na watu wanapiga mkwanja wakutosha huko. Naomba kama kuna anayeifahamu hii atujuze kwa maslahi ya wengi.

ndyo ni kitu inalipa tena seriously soma hyo picha
 

Attachments

  • agency.JPG
    agency.JPG
    35.7 KB · Views: 309
Qnet ni matapeli kuna jamaa yangu alijiunga july mwaka jana alinunua saa kama m4 hivi akawa ananishauri nijiunge akiahidi kuna pesa nje nje nikamwambia nampa miezi sita atagundua katapeliwa nashukuru ilichukua miezi mitatu kujua ule ni utapeli wa kisheria.
 
Ukiona fursa za kuitana sijui utoe hela utafute watu ni ujinga ty achana nayo kama unahutaji bidhàa nunua kwenye soko la kawaida
 
Cha bure ni kipi hapo Francis? People are paid in commissions basis we unasema wanatapeliwa?? Kwanza Qnet ni muunganiko wa makampuni mengi tu ilo ni jina tu la kimtandaoni...Maisha ya watu yanabadilika kutokana na Qnet we unasema utapeli?? Mtaje aliyetapeliwa na useme ametapeliwa kwa staili gani then tuongee vizuri
 
Back
Top Bottom