Juzi nilikuwa kwenye internet cafe pembeni yangu kulikuwa na watoto wa wawili wa kiume miaka kama 10 au 11 wamefungua page mbili moja FB nyingine ponograph wakiona mtu anasogea wanaweka Fb kiukweli nilishindwa kusema kitu ila nina wafahamu na wazazi wao nitajaribu kusema nao maana tupo mtaa mmoja, sasa najiuliza walijuaje mitandao ya picha za ngono huu utandawazi. Utatumaliza
Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
Kuna jambo jingine nililiona kwa harakaharaka. Kwenye notification alikuwa na message kama 5, maana yake ni mwanachama active. Isitoshe kibaya zaidi alipoanza kunionyesha anachokifanya alikuwa ana requests za friendship
kama watu 5 na kwa haraka haraka akawa ana-accept (bila hata kuangalia profile ya huyo mtu), hilo kweli nilimkataza kwa kumwambia si sawa ku-accept kila mtu.
Na ana confidance kweli, hata password yake alikuwa anaweka kwa kujipinda nisiione!
usiyemjua
password anaficha ili inbox anakuonesha wazi bila aibu. Napata taabu kuamini hii stori. Akili za mtoto wa miaka minane haijakomaa mpaka kuwa na akili ya kujiwekea fake identity / personality kwenye mtandao. Na kama hii stori ni ya kweli ni jukumu lako kama anko wake kuwaambia wazazi wake ulichokiona kuliko kuja kusimulia hapa ukijifanya kuhurumia kizazi cha huyu mtoto mdogo.
Kama wewe imekuwa vigumu kuamini kama mimi mwanzo basi kuna tatizo kubwa kwenye jamii yetu hasa watoto.
Sijui kwa nini nimsingizie, ili iweje!!
Halafu si kila jambo unaloliona kwa mtoto unaenda kumsimulia mzazi wake haraka haraka, lazima kutumia busara kuwafahamu vizuri wazazi wake (kwa sababu sijazoeana nao sana). Na hata mtoto ni vizuri kujua kwanza ni vipi amefikia hatua hiyo, unaweza kukuta kuna mlolongo wa ndugu hapo kwao na huo ndio mchezo.
Inawezekana imekuwa rahisi kwangu kujua hayo yote kwa sababu ni rafiki wa watoto. Ninapoishi kuna hata baadhi majirani zangu siwajui majina, lakini ukitaka kujua leo nimekula nini waulize watoto. Nawafahamu vizuri
Nanyie bana kwa kujichetua!hivi ni mtoto gani atakaye soma msondo ngoma baba anasim ya toch mama ana line simu hana akajua kutumia facebook huyo wakishua bana
muulizeni mtoa mada kama haja kwambia anasoma fm academia au akudo ipact kingeleza kimo shuleni wanafundishwa pc na dada zake au kaka zake wanatumia pc zaidi ya hapo mtoa mada peleka uwazi usituone wajinga...nimepita tuu kasuku mtu
kuna rafiki yangu bintiyake ana miaka 12 ana marafiki 130,huwa naangaliaga picha zakeee nabaki! haya.
Unafikir nimenyamaza mtani!
mamake ni mmojawa hao130 na comment zake saaasa!
Nitaendelea kuwa mzazi wa kizamani........Aisee!
Nilimuuliza mwanangu kama ana email account akasema hana; kama shuleni wana Internet access akasema hawana. (Faida moja wapo ya boarding school; huwezi enda Internet cafe). Na kummanage mtoto wakati wa likizo ni rahisi.
Ngoja leo nimtege kama ana FB account nijue. Aisee kazi ipo!
Aisee!
Nilimuuliza mwanangu kama ana email account akasema hana; kama shuleni wana Internet access akasema hawana. (Faida moja wapo ya boarding school; huwezi enda Internet cafe). Na kummanage mtoto wakati wa likizo ni rahisi.
Ngoja leo nimtege kama ana FB account nijue. Aisee kazi ipo!
Nitaendelea kuwa mzazi wa kizamani........
Mwanangu atajinunulia simu yake binafsi akiwa chuo au atakapoanza kazi, kwa hela yake.
Internet atatumia under my supervision
kuna siku mwanangu wa 13 years alirudi home na simu kapewa na dadangu..... nikaichukua ile simu mpaka leo ipo chumbani kwangu. siku nyingine binamu yangu akampa simu, mwanangu akaikataa na akamwambia kuwa mama ataichukua maana anasema tutumie simu ya nyumbani.Naungana nawe, ila sina uhakika huko mbele ya safari tutafikaje. Coz tutakataa kuwanunulia simu, ila 'mijitu' yenyewe itanunua na itampa (mbaya akiwa mtoto wa kike, au hata wa kiume yaweza tokea).
Nilikuja kustuka mtoto wangu wa miaka 9 kafunguliwa akaunti FB na ndugu yake, who is 12 (ambaye hatuishi naye), tayari na lundo la marafiki! Ndugu mwenyewe yeye 'amejaaliwa' kununuliwa simu na mzazi wake, kwa hiyo kwake upatikanaji wa internet siyo shida. Sasa wa kwangu anashangaa, kuwa kwa nini yeye simnunulii simu wakati mwenzake amenunuliwa simu na mzazi wake? Na kwa nini yeye asiruhusiwe kuendelea kutumia FB wakati kwa mwenzie siyo shida? Na mazingira yaliyopo ni lazima kipindi fulani ndugu akae kwangu, unaona mazingira ya ulezi hapo?