Ananidanganya ili anioe

Ananidanganya ili anioe

Ahsanteni wote nitaolewa nitamvumilia tu,ila naogopa rafiki zangu wakijua hata hatuna kitanda si watanicheka jamani
Katika ndoa usiruhusu aibu na uoga ikutawale. Ukikubali na kuamini kwa Dhati utafanikiwa. Kama Jamaa anamanisha na wew ukakubali kwa moyo wa dhati nakushauri uolewe hakuna Sababu ya kuofia marafiki.
Kumbuka unapofanikiwa hao hao marafiki ndo wanakuwa wakwanza kukupongeza na unapofeli uwa wa kwanza kukucheka pia. So ishi maisha yako uliyochagua na siyo kumsilikiza kila Mmoja au kuishi anavyoishi.
Ahsante
 
Jamani misha ni kusaidiana,kumbukeni jamaa anatafuta kazi bado na hali ya sasa ya uchumi. Kwanini yeye asiendelee na shule ikiwa wazazi wana uwezo apate kumalizia elimu ya chuo wakati mwanaume anasaka kazi na yeye akitoka atafute kazi waweze kujenga maisha pamoj?,maana akisema avumilie ni sawa wataoana na kuishi kwa zawadi kuna kul,kuvaa,na jamaa hajatengemaa. Waendelee na urafiki wao ikibidi wachumbiane kabisa ijulikane kwa kila mmoja ili waweke ukaribu jamaa akipata kazi au shughuli ya kumuingizia kipato atamwoa hata akiwa bado yupo chuo na yeye akimaliza chuo wanaungan kusaka life. Sijui lakini ila ni mtazamo tu.
 
Shikamoo wakubwa,Mimi ni binti mkubwa kiasi nimemaliza form six mwaka huu kuna huyu kaka jamani yeye ana miaka 31yaani amengangania anioe sasa Mimi nashindwa tutaishije nilishafika kwake hats kitanda hana analala chini bado anatafuta Kazi ananiambia nikubali tufanye harusi zawadi tutakazopata tutaanzia maisha halafu akipata Kazi atanisomesha yeye chuo.nishauri mlioolewa na nyie mlianza kulala chini kama Mimi.
Miaka 31 hana kitanda??? Jiulize kama ameshindwa miaka hiyo yote kutafuta hela ya kununua kitanda akikuoa si ndo itakuwa hatari? Ninavyofahamu kuna majukumu ya hapa na pale yataongezeka na hata hicho kitanda sijui kama atanunua.

Ila akili kumkichwa ukipenda kuolewa nenda lakini utapauka mpaka utajuta kuolewa yani utazeeka ukiwa na miaka miwili katika ndoa(just kidding).
 
Wabongo bana, sijui ni lini tutaacha ku judge watu wengine kwa kuangalia umri. Utafikiri imeandikwa mahali ukiwa na umri fulani lazima umiliki kitu hiki na kile,uwe na mtoto, uwe umeoa au kuolewa,mara hivi mara vile. Ukienda kinyume eti 'una matatizo'.. We still have a very long way to go.
 
Hiyo form six yako haijakusaidia kabisa.....

Anyway olewa tu...utachakaa kabla ya umri wako.... na mtaishi maisha ya kuombaomba... hamna mbele nyuma wala kati mtaishije???
 
Hujadanganywa bana embu rekebisha hapo.. Kama unampenda kalale chini ila kama humpendi subiri afanikiwe ndiyo uende kupenda hela
 
Pole binti na Hongera pia..
1. Sikiliza moyo wako
2. Unaweza kusoma chuo hata kama upo ndoani
3. Mafanikio katika maisha hayana wakati, yanaweza tokea mwanzoni, katikati au mwishoni mwa maisha.

NIMEIPENDA HIYO YA TATU..."VINA MWANZO KATI NA MWISHO"...KUNA WIMBO WA MSANII WA BONGO FLAVA ALIWAHI KUIMBA...AHAHAHA
 
Mimi Nina wasiwasi huyo ni mume wa mtu kakimbia familia yake kaanza kuishi upya ndomana hata kitanda hana .anakudanganya huyo
 
Ahsanteni wote nitaolewa nitamvumilia tu,ila naogopa rafiki zangu wakijua hata hatuna kitanda si watanicheka jamani
Usipende kufanya kitu kwa kujiuliza watu watanionaje/watanicheka

Sikiliza moyo

Tumia akili yako

Fanya maamuzi yako ukiwa timamu ili badae usiwe na wa kumlaumu.

Japo hana kitu je ni mtu wa kujituma? Anashaurika?
 
Wenye ndoa zao wakushauri mi napita tu
 
nadhani binti bado hujatujua vizur sisi wanaume embu nenda kasome hiv huwaonea huruma wazaz ambao walikuwa na matarajio makubwa kutoka kwako?
 
Back
Top Bottom