Anachofanya Waziri Mkuu sio sawa, sio haki, sio Good Governance! Ni udhalilishaji na kuaibishana!

SafI SANA SAFI SANA! utawala mzuri sana huu mtu kama unajua kazi unayoifanya na unajirambua+ si mla rushwa bas utakua tayari kwa lolote lile kujibu.
 
WE PASCO KAMA LOWASA NDO ANAKUTUMA....KAMWAMBIE TOO LATE TO CATCH THE TRAIN....INFACT AMEBUGI...:lock1:
 
Kabisa unamaanisha unachokiongea? Anyway

Sijaongea. Nimeandika!

1.Ulikuwa unajua kuna makontena 300 yamepotea,najua hujui hadi PM alipotimba bandari

Hujui kama nilikuwa najua au la. Hivyo acha kujifanya unajua vitu ambavyo hujui.

2.Najua ulishakariri makontena yaliyopotea bandari ni 300,yet again PM akarudi akagundua mengine 2000 yamepotea,ulilijua hili

Acha kujifanya unajua maana nikikwambia uthibitishe hutaweza. Hujui kama nilishakariri au la. Hujui.

Unajua bado siamini kama unasema hujui nini kifanyike.

Hivi wewe unajua tofauti ya 'kujua' na 'kuamini'?
 
Leo umeongea Pumba Pasco Waache waibishwe wameyataka wenyewe. Kusoma hujui hata picha uioni? Wawe wa kweli na wajiandae kuwa na taarifa sahihi za kazi zao. Dought yangu ni kwenye misemo ya Mh. Waziri Mkuu, anauliza swali halafu anapotakiwa kujibiwa ana mkatisha mtu na kumuambia nimekuja kujifunza. Hiyo lugha si nzuri kwa cheo chake ni kama mipasho fulani Nilimuona kwenye TV alipokuwa anamuuliza Mkuu wa Taasisi ya Reli.
 
Jana niliiona video kupitia ITV ikimwonesha Waziri Mkuu akimhoji Mtendaji Mkuu TRL kuhusu walichofanyia Tsh. 3 billion walizokopa kutoka TIB. Na kwa nilichokiona, Waziri Mkuu hakumpa nafasi Bosi wa TRL kutoa maelezo ya kina. Bosi huyo alidokeza tu kwamba walitumia pesa zile kulipa mishahara. Asingeweza kutoa maelezo ya kina mbele ya camera kuhusu ilikuwaje akafanya hivyo badala ya kuzitumia pesa hizo kwa malengo yaliyokusudiwa. Kwa mfano, asingeweza kusema mbele ya camera kwamba alilazimishwa na Mwakyembe au Sitta kutumia pesa za mkopo kulipa mishahara badala ya kutekeleza miradi iliyokusudiwa. Pamoja na ukweli kwamba maswali ya Waziri Mkuu kwa Bosi wa TRL ni ya msingi, hakukuwa na haja ya kuuliza maswali hayo mbele ya camera. Angepaswa kutafuta kilichotokea kwa hizo pesa za mkopo na kuchukua hatua. Then, tutangaziwe hatua zilizochukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwataja watuhumiwa, kama wapo. Hakuna justification yoyote ya kumhoji mtu mbele ya camera kuhusu mkopo uliochukuliwa na shirika kwa kuwa mazingira yatambana kueleza ukweli. Waziri Mkuu anazidiwa na dhamira ya kutaka kuonekana akifanya kazi/akipambana na rushwa/ubadhilifu (to be seen fighting corruption). Ninamuunga mkono katika jitihada anazofanya kupambana na uchafu mwingi na uzembe katika utendaji serikalini. Lakini ajitahidi kuidhibiti "urge" ya kutaka kuonekana akifanya. Yeye ajielekeze zaidi katika kufanya kazi yake kwa ufasaha, kama ni sifa atazipata tu kwa kuwa Watanzania tutaona matokeo.
 
Hiyo inaweza kuwa "tactic" na kutuma ujumbe haraka. Hataweza kwenda Mwanza au Arusha au Mbeya kufanya mazungumzo katika vyumba vya miktano. Akifanya kimnya kimnya itachukua muda mrefu sana kuwa na "message sent". Viongozi waliotumia tactic hii ya suprise ni Sokoine, Mrema na Lowassa. Na kila mmoja aliona kwamba ilikuwa kazi kubwa. Good governance ilitumiwa na JK na uliona imeshindwa katika mazingira ya Kitanzania. Kwenye vita unaanza na suprises na sio negiations.
 
Geiglitz ungekuwa karibu ningekupa 10000/= ili urudishe bundle yako, uliyotumia kupost hapa. yani umenena vema. wataisoma namba.
 
Tunashangilia sana kwa njia huu utatu wa viongozi hawa unavyofanyika. Lakini likija kukutokea wewe au ndugu yako usije kujilizaliza hapa.

Pasco anakubaliana na hatua wanazochukua viongozi wetu, ila hakubaliani na style viongozi wanayotumia.

Kwani PM angefata utaratibu hao walipa kodi wangeponea wapi?

Hizo show-off sometimes hazina tija, sitashangaa kila mtumishi kutumia style hiyo bila kufata utaratibu kwa wananchi!
 
Last edited by a moderator:
Hapa kazi tu, acha wafanyiwe kazi. Watu km wanajua wanachofanya n kibaya basi n waache mapema. Wasitarajie watafanya ujinga alafu eti wataitwa chemba. Chemba kuongea nn!? utawala wa Maguful n utawala wa wazi hamna kuficha ficha mambo. Unachanwa live ili na wengne wajifunze kupitia kwako kilichokukuta. Watu hii nchi kuna vitengo walishavifanya km mali zao.. Hii nchi bila udikteta haiendi, maana ilikuwa imeshaoza na kunuka.. Fanya kazi inavyostahili, Magufuli utamckia tu
 
Sitaweza kutetea kauli yako mkuu sababu nchi imeharibika, inaitaji watu wa hivi inyooke, nyie wafanyakazi huko mlishajifanya miungu watu, ham ambiliki ham sikii, basi mfundishwe kazi, sababu hakuna namna.HAPA KAZI TUUUU.
 
Si haki, si sawa, ni kudhalilishana....maybe, we live that life kwenye private sector...I don't care...wacha wachemshwe akili zichangamke....
 
Kumbe watanzania tumezoea kuibiwa, yaani wakati wenzetu Kenya hapo Nairobi kuna flyover kibao sisi majizi ambayo yamefilisi nchi hii kwa miaka kibao mnataka yaitwe faragha kwakweli wabongo ni Shiidah na kwa huo wimbo wa good governance tutaendelea kuwa maskini miaka 100 ijayo
 
Hapa kazi tu, acha wafanyiwe kazi. Watu km wanajua wanachofanya n kibaya basi n waache mapema. Wasitarajie watafanya ujinga alafu eti wataitwa chemba. Chemba kuongea nn!? utawala wa Maguful n utawala wa wazi hamna kuficha ficha mambo. Unachanwa live ili na wengne wajifunze kupitia kwako kilichokukuta. Watu hii nchi kuna vitengo walishavifanya km mali zao.. Hii nchi bila udikteta haiendi, maana ilikuwa imeshaoza na kunuka.. Fanya kazi inavyostahili, Magufuli utamckia tu

Uko sawa kabisa, kwani wafanye siri wako chumban? Siri iko chumbani bana. 👅👅👅
 
NImeangali maoni ya wengi kati ya wale wanaopinga hatua zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano, nimegundua kuwa watu hawa aidha wao wenyewe wameathirika na matukio hayo moja kwa moja, au ndugu/rafiki zao wa karibu ni wahanga wa matukio hayo. Mahali ambapo taasisi imeruhusu makontena 349 yatolewe bila kulipa ushuru, lugha nzuri ya kuto kudhalilishana hapo ilikuwa ni ipi. Mahali ambapo makontena zidi ya elfu mbili yametolewa bandalini bila kulipa ushuru, lugha tamu ya kuwafurahisha waliofanya hayo ilikuwa ni ipi. Tuache unafiki, hapa kuna upotevu wa kodi ya serikali, hakuna kuchekeana maana ukicheka na nyani utavuna mabua. Mtumishi wa serikali bila aibu anamiliki nyumba zaidi ya ishirini, ni kitu gani hicho, acha wafu wawazike wafu wao.

Hii serikali inabidi iwe na mila za ki Korea kusini, ukihujumu ni risasi tu
 
Hata na wewe Manjagata unavyofanya sio poa kabisa. Why unamsema Pasco hadharani eti kwa kua yeye Pasco amemsema PM hadharani?

Nawe si ungemuendea chemba tu kuliko kusema hapa? SI HAKI, SI SAWA na SI GOOD GOVERNANCE.
Na wewe Shark hivi unavyofanya siyo vizuri kabisa, huu siyo utawala bora kabisa yaani unanigombeza hadharani namna hiyo kiongozi wangu? Si ungenifuata chemba tukayamaliza huko huko? Ha ha ha haaaaaa hii sasa ni hatari!
 
Back
Top Bottom