Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 25,448
- 46,216
Kuna tafsiri ambayo wana Simba SC Tanzania wanayo kwa Mwenyekiti wa Klabu yao MURTAZA MANGUNGU na kuna tafsiri wana Simba wanayo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi CRESENTIUS MAGORI.
Bahati mbaya sana nadiriki kusema wengi wanawatafsiri hawa watu TOFAUTI (Vice Versa) na ukweli ulivyo. Mmoja anaonekana kama mtu hohe hahe na asiejielewa wala kujua kitu na mwingine anaonekana kama mjuzi wa mambo ambaye hakuna anayemshinda kwenye mpira wa nchi hii na masuala ya klabu ya Simba.
Nimefuatilia jambo lao tangu jana na leo nimefanya mahojiano nao wote wawili, nimejifunza mambo mengi sana.
Mmoja ni msikivu, anafuata taratibu, anatumia busara, hajakivaa cheo cha Mwenyekiti, mtu muangwana ambaye hataki ugomvi wala kuparurana na watu kısa cheo, ameweka manufaa ya klabu mbele bila kujisifu wala kumtangazia mtu, ana iona klabu ni mali ya wana Simba wote walio na thamani sawa.
Mwingine ni mjuaji ambaye bila yeye Simba si lolote, mjuzi wa mambo ya soka na mbobezi ambaye anastahili vyeo vyote na heshima, anaijua Simba kuliko yoyote, yeye ni Simba ‘A’ na wengine wanafata nyuma yake, ameipigania Simba na kuichangia pengine kuliko yoyote bila kujali aliowakuta klabuni, neno lake ni amri klabuni hapo.
Kwa mujibu ya maelezo yao ya leo sikuona shida ya Mangungu kwa kilichotokea jana na mpaka sasa sikuona UBATILI wa jambo zima, kama ambavyo sijaona uhalali wa chapisho la Magori tena likawekwa kwenye page ya klabu likimnannga Mwenyekiti wa Simba SC.
Mangungu anasema Bodi ilipoteza uhai wake baada ya katiba mpya kupitishwa na BMT, kilichokuwa kinafanyika ni busara ya kiuongozi tu kuiweka hai kuepusha migogoro isiyo ya lazima. Lakini amelazimishwa na Serikali kuteua wajumbe wa baraza la wadhamini na akipewa deadline, hawa ni wasimamizi wa mali za Simba SC na yeye ndo Mwenyekiti wake, shida iko wapi? Kama jambo hili lisingefanywa sasa lingefanywa lini?. "
Bahati mbaya sana nadiriki kusema wengi wanawatafsiri hawa watu TOFAUTI (Vice Versa) na ukweli ulivyo. Mmoja anaonekana kama mtu hohe hahe na asiejielewa wala kujua kitu na mwingine anaonekana kama mjuzi wa mambo ambaye hakuna anayemshinda kwenye mpira wa nchi hii na masuala ya klabu ya Simba.
Nimefuatilia jambo lao tangu jana na leo nimefanya mahojiano nao wote wawili, nimejifunza mambo mengi sana.
Mmoja ni msikivu, anafuata taratibu, anatumia busara, hajakivaa cheo cha Mwenyekiti, mtu muangwana ambaye hataki ugomvi wala kuparurana na watu kısa cheo, ameweka manufaa ya klabu mbele bila kujisifu wala kumtangazia mtu, ana iona klabu ni mali ya wana Simba wote walio na thamani sawa.
Mwingine ni mjuaji ambaye bila yeye Simba si lolote, mjuzi wa mambo ya soka na mbobezi ambaye anastahili vyeo vyote na heshima, anaijua Simba kuliko yoyote, yeye ni Simba ‘A’ na wengine wanafata nyuma yake, ameipigania Simba na kuichangia pengine kuliko yoyote bila kujali aliowakuta klabuni, neno lake ni amri klabuni hapo.
Kwa mujibu ya maelezo yao ya leo sikuona shida ya Mangungu kwa kilichotokea jana na mpaka sasa sikuona UBATILI wa jambo zima, kama ambavyo sijaona uhalali wa chapisho la Magori tena likawekwa kwenye page ya klabu likimnannga Mwenyekiti wa Simba SC.
Mangungu anasema Bodi ilipoteza uhai wake baada ya katiba mpya kupitishwa na BMT, kilichokuwa kinafanyika ni busara ya kiuongozi tu kuiweka hai kuepusha migogoro isiyo ya lazima. Lakini amelazimishwa na Serikali kuteua wajumbe wa baraza la wadhamini na akipewa deadline, hawa ni wasimamizi wa mali za Simba SC na yeye ndo Mwenyekiti wake, shida iko wapi? Kama jambo hili lisingefanywa sasa lingefanywa lini?. "