Jakubumba
JF-Expert Member
- Mar 5, 2011
- 1,624
- 501
Babu yangu ana umri wa miaka 70 na ana wanawake 10, mke wa kumi alikuwa ni mchumba wangu ambae tulipendana sana na kuahidiana kuoana. Lakini kwa Tamaa ya wazazi wao kupenda mali babu aliwarubuni kirahi na kujipatia mke ingawa alikuwa anajua tuna mahusiano. Binti amekuwa hana raha kabisa kwa mda wote huo, na mahusiano yetu yaliendelea kama kawaida maana aliniambia kama hatutaendelea atajiua. Ana umri wa miaka 21 na mimi 25. Babu amewapa zamu wake zake za kulala nao,yeye alikuwa na siku moja kwa mwezi hivyo tulijua ratiba yake vizuri. Kumbe machare yalimcheza akatega mtego na kutunasa. Ukoo umekaa na umeamua kuwa mimi niondoke kabisa kwenye familia kwa maana kwamba umenitenga. Nina siku kumi za kujiandaa kuondoka ila binti ameniambia nikimuacha anajiua. Je nifanyeje? Mimi namjua vizuri sana analoliongea na anamaanisha maana uhusiano watu kabla hajaolewa ulikuwa wa miaka 4. Ushauri wenu ni wa muhimu sana, kabila langu mkurya, najua hapo wakurya wa musoma watanielewa sana.