Amini nawaambia, hakuna wa kumbishia Marekani kwa lolote. Akisema, dunia imesema; akiagiza ni kutekeleza tu

Kiuchumi ndiye nambari moja, akimuacha mbali mno wa pili-China. Kijeshi, ndiye kinara. Kiintelijensia, hakuna zaidi yake. Kiushawishi (kwakuwa anaongoza na kuwa na nguvu ya kiuchumi, kijeshi na kiintelijensia), hakuna anayemzidi ushawishi Marekani.

Mtu yeyote atakuwa sahihi akisema kuwa Marekani ndiye kiranja Mkuu wa dunia hii. Ndiye ambaye aweza kusema au kuagiza hili au lile na likatekelezwa. Ndiye ambaye anaweza kupeleleza bila kueleza na kufuatilia bila kufuatiliwa na akajua kila alitakalo. Nguvu ya kifedha!

Marekani hana mpinzani humu duniani kwasasa. Kila nchi husema na kufanya lakini inapofikia kuna mvutano na Marekani, nchi husika hujirudi na kusikiliza kwa makini Marekani anataka au hataki nini. Hata kama nchi husika hulifanya jambo kisiasa, haliwi mbali na akitakacho mwenyenguvu Marekani.

Inauma kukiri hili. Lakini, ndiyo ukweli wenyewe. Kiongozi wa Korea Kaskazini kukaa meza ya mazungumzo na Trump si jambo dogo. Hivi sasa anakula shushu. Kimyakimya. Amini nawaambia, pamoja na porojo zote tunazoweza kuambiana, hakuna kama Marekani kwa dunia tuliyonayo hivi sasa.

Pompeo, Jasusi mbobezi na Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Ujazusi la Marekani almaarufu kama CIA, Waziri wa sasa wa Mambo ya Nje wa Marekani ameshasema aliyoyasema kumhusu Makonda na Tanzania kwa ujumla. Tuseme yote lakini tukumbuke Marekeni ndiye mwenye nguvu.

Haitatusaidia barua ya Msando wala kuiweka hoja kando kama simu isiyo na bando. Marekani imefuatilia; imekusanya; imechambua na imetuambia. Ni kazi kwetu kusuka kusuka au kunyoa. Niaminini mimi, hakuna kama Marekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam.
Marekani hawezi kumpa maagizo mchina au mrusi hata siku moja
 
crocodile wengi mnachanganya kudhani ni Marekani yote Ushoga ni halali, kuna majimbo Ushoga hauruhusiwi kabisa. Majimbo kama Alabama, Arizona, Louisiana, Mississippi, North Carolina, Oklahoma, South Carolina,Texas na Utah zina sheria za kupinga ushoga. Na mpaka dakika hii ninapoandika hapa si kweli kwamba mashoga Marekani wanaishi maishi ya Uhuru unaosemwa na watetezi wa CCM na Makonda dhidi ya Marekani.

Marekani Mashoga wamepata Ushindi kwenye mahakama mbali mbali za nchi hiyo kwamba wasibaguliwe kwani na wenyewe wana haki sawa kama wale wasio mashoga. Siyo kwamba Ushoga ni jambo linalokubalika kwa kila mtu Marekani.
Sawa bwana na nalitambua hilo.Kama Suala ni haki ya mtu, nashangaa tu vipi wasenge wawe na haki zaidi ya wenye ndoa za mitala ambayo kule ni illegal federally. Huku yote tufanye lakini tukiwagusa hao wa kuinamishana, wababe hao. Kuna nguvu za giza tu.
Siku hizi wanatuwekea hata kwenye katuni za watoto!!
 
Siku hizi wanatuwekea hata kwenye katuni za watoto!!
Mambo ya Ushoga si mambo ya Serikali ya Marekani bali ni ya watu wa LGBT ambao wamefanikiwa kujenga ushawishi wao kwa vyombo vya habari kwamba na wao ni watu kama wale wasio kama wao. Trump na chama chake ni wapinzani wa mambo hayo na ndiyo maana amezuia "Transgender" kuajiriwa jeshini.

Katuni kwa watoto ni uzembe wa wazazi kuwasimamia watoto wao. Siyo kila familia watoto wao wanaangalia hizo katuni.

Marekani kuoa wake zaidi ya mmoja huwezi kukamatwa. Msingi wa mmke mmoja unatokana na wajenzi wa taifa hilo wengi wao walitokana na misingi ya kilokole.
 
Kama Venezuela, Cuba, North Korea, Somalia, Iran, Iraq, Syria, Libya ni makundi ya magaidi basi na iwe hivyo.

Gaidi kwa mmoja ni mpigania Uhuru kwa mwengine. Hata Mandela alihukumiwa kifungp cha maisha kwa ugaidi, jee, alikuwa gaidi kweli?
Hakuna hata nchi moja hapo unaweza kusema uzamie ukatafute maisha,yani zimeshajifia kabla,marekani hawezi kutumia resources zake kupigana na nchi kama hizo,ameshaweka mazingira wanamsaidia kwa kupigana wenyewe kwa wenyewe,kulipuana mabomu kama yote wenyewe kwa wenyewe.
 
Hakuna hata nchi moja hapo unaweza kusema uzamie ukatafute maisha,yani zimeshajifia kabla,marekani hawezi kutumia resources zake kupigana na nchi kama hizo,ameshaweka mazingira wanamsaidia kwa kupigana wenyewe kwa wenyewe,kulipuana mabomu kama yote wenyewe kwa wenyewe.
Watu wanaandika nini wewe unaandika nini.

Kwa watu kama wewe, Tanzania tuna safari ndefu sana ya kwenda.
 
Kiuchumi ndiye nambari moja, akimuacha mbali mno wa pili-China. Kijeshi, ndiye kinara. Kiintelijensia, hakuna zaidi yake. Kiushawishi (kwakuwa anaongoza na kuwa na nguvu ya kiuchumi, kijeshi na kiintelijensia), hakuna anayemzidi ushawishi Marekani.

Mtu yeyote atakuwa sahihi akisema kuwa Marekani ndiye kiranja Mkuu wa dunia hii. Ndiye ambaye aweza kusema au kuagiza hili au lile na likatekelezwa. Ndiye ambaye anaweza kupeleleza bila kueleza na kufuatilia bila kufuatiliwa na akajua kila alitakalo. Nguvu ya kifedha!

Marekani hana mpinzani humu duniani kwasasa. Kila nchi husema na kufanya lakini inapofikia kuna mvutano na Marekani, nchi husika hujirudi na kusikiliza kwa makini Marekani anataka au hataki nini. Hata kama nchi husika hulifanya jambo kisiasa, haliwi mbali na akitakacho mwenyenguvu Marekani.

Inauma kukiri hili. Lakini, ndiyo ukweli wenyewe. Kiongozi wa Korea Kaskazini kukaa meza ya mazungumzo na Trump si jambo dogo. Hivi sasa anakula shushu. Kimyakimya. Amini nawaambia, pamoja na porojo zote tunazoweza kuambiana, hakuna kama Marekani kwa dunia tuliyonayo hivi sasa.

Pompeo, Jasusi mbobezi na Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Ujazusi la Marekani almaarufu kama CIA, Waziri wa sasa wa Mambo ya Nje wa Marekani ameshasema aliyoyasema kumhusu Makonda na Tanzania kwa ujumla. Tuseme yote lakini tukumbuke Marekeni ndiye mwenye nguvu.

Haitatusaidia barua ya Msando wala kuiweka hoja kando kama simu isiyo na bando. Marekani imefuatilia; imekusanya; imechambua na imetuambia. Ni kazi kwetu kusuka kusuka au kunyoa. Niaminini mimi, hakuna kama Marekani!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam.
WEka hapa barua ya Msando tuipitie!
 
Hiki ndicho anachoweza msando


Sent using Rocket Propelled Grenade
 
Back
Top Bottom