Samahani kama ntakuwa narudia ya wengine. Kaka swallow your pride. Kama mmekaa miaka miwili halafu mahaba yakaanza kudorora haikuwa dalili kwamba hakupendi. Hakuna mahali mahaba yanayodumu daima. Baada ya miaka miwili ndo mlikuwa mnaingia sasa kwenye uhalisia. Wengine yanadumu miezi, wengine wiki. Ukiona yaliyodumu miaka 5, 10....ujue kuna jitihada za makusudi za kuyapalilia. Ulitakiwa kuwa na subira na kama kweli ulikuwa unampenda sana sana ungekuja huku kuuliza jamani mahaba yamefifia, nipalilieje? Hapa nikikwambia utaje madhaifu yake matano uliyoyaona na kuyavumilia hiyo miaka miwili utaweza? Kwa mahaba mliyokuwa nayo sijui kama uliyaona.
Sasa mpenzi wako huyo kuondoka bila kulalamika wala kukonda haimaanishi kuwa hajaathirika. Kila mtu ana jinsi yake ya kukabiliana na changamoto. Huenda pamoja na kukupenda ameshukuru umemuacha mapema badala ya kuendelea kumpotezea muda. Ulitaka akulilie kama yule wa mwanzo ndo usikie raha ee? Kama unamkubali jishushe, omba radhi, toa sababu ni kwa nini unaona ni vyema mkarudiana na nini utafanya kumhakikishia usalama akirudi. Kujishusha na kuomba radhi ni "tabia ya kike" kwa mujibu wa wanaume ila unaweza kugusa moyo wa mwanamke kwa kumuonyesha "tabia za kike". Ukikosa omba msamaha, mpe attention,,,,Kwa ufupi poteza kidogo upate kikubwa. Usiogope kwamba anaweza kukataa. Akikataa basi, kwenye biashara kuna kupata na kupoteza. Bora ujaribu ushindwe.