Salaam!
Katika kusaka faraja murua, juzi kati nilikutana na mdada mmoja hivi murua kabisa. Zoezi la kubadilishana namba likaenda vizuri.
Leo asubuhi na mapema kaniomba hela ya chai; nami, kwa kuzingatia bei halisi ya maandazi huku kijijini ambayo ni tshs 100, nikamrushia buku na mia mbili ya kutolea. Nilifanya hivyo nikiamini kuwa maandazi saba na kikombe cha chai atapata.
Ajabu ni kuwa alipopokea aliniuliza kama mara tatu hivi kuwa nimemtumia au la. Nilipomwambia kuwa ndiyo nimemtumia 1,200 ili apate buku ya chai, hajajibu chochote na hapokei simu mpaka muda huu. Nikafikiri labda amepatwa na ugonjwa kumbe taarifa za kiintelejinsia zinasema ni mzima wa afya tu.
Kuna nini hapa?!!!
Katika kusaka faraja murua, juzi kati nilikutana na mdada mmoja hivi murua kabisa. Zoezi la kubadilishana namba likaenda vizuri.
Leo asubuhi na mapema kaniomba hela ya chai; nami, kwa kuzingatia bei halisi ya maandazi huku kijijini ambayo ni tshs 100, nikamrushia buku na mia mbili ya kutolea. Nilifanya hivyo nikiamini kuwa maandazi saba na kikombe cha chai atapata.
Ajabu ni kuwa alipopokea aliniuliza kama mara tatu hivi kuwa nimemtumia au la. Nilipomwambia kuwa ndiyo nimemtumia 1,200 ili apate buku ya chai, hajajibu chochote na hapokei simu mpaka muda huu. Nikafikiri labda amepatwa na ugonjwa kumbe taarifa za kiintelejinsia zinasema ni mzima wa afya tu.
Kuna nini hapa?!!!