Usiwalaumi wananchi kwa kuwaita eti wajinga!
maadui matatu aliosema nyerere(na sasa wameongezeka) ni upi umetokomezwa..ujinga hufutwa na elimu na jukumu la serikali kuelimisha na kufuta ujinga...
Hivi ulishawai kuamini mikakati ya wapinzani hasa Chadema.
ni kipi ni kikuaminishacho katika chama tawala....fikra zako chaguo lako..umeridhika na ccm endelea kutotaka(
kuamini mikakati ya ccm) mabadiliko
Ikiwa Leo kiongozi anatoa kauli hii, baada siku mbili anaigeuka kauli yake tena Bila hata kuomba radhi kwa kauli ya awali nani alaumiwe.
unaongozwa zaidi na mihemko ya hisia na chuki kuliko kureason suala kwa ushahidi..kauli za jumla jumla niote kauli ipi kati ya zipi...
magufuli umteteaye umesahau aliahidi kompyuta kwa kila mwalimu..siku kadhaa ccm wakakanusha naye wala hakuomba radhi wala kuliongelea tena..#unafikimbaya
Ikiwa Chadema yote ikiongozwa na Mbowe wametuaminisha ufisadi wa Lowassa kwa miaka nane, tena wamefikia hatua ya kutuasa atakae mchagua Lowassa akapimwe akili, Leo Bila hata aibu wala kutuomba radhi kwa kutudanganya miaka yote hii wanatuambia huyu mtu ni Safi hana tuhuma zozote.
rasi wako alikwambia za kuambiwa changanya na zako..sasa sijui status ya ''zako''
Hata kama mtaji wa ccm ni ujinga, binafsi naamini mtaji wa ccm ni ujinga
ewaaa..na huku ukiendelea kumpigia chapuo Magufuli(watu haohao waliowekeza kwenye ujinga)
Chama ni misingi, ila upinzani hauna misingi wala itikadi ya kueleweka, kifupi ni vigeu geu wasioamini kile wanachokisimia.
unaweza niambia misingi na itikadi ya CCM ya Magufuli wako kwa ushahidi wa matendo yao?
Sio wote tupo tayari kupigia kura hata maiti kama wengi wenu mnavyoapa.
ungetambua no 1 enemy wa maendeleo nchi hii ungeng`amua kwa undani misingi ya kauli hiyo na si kuibeba kama ilivyo..
..naendelea kusisitiza mtaji wa ccm ni ujinga...
umeichoka huku unampigia debe mgombea wake..sasa wewe unatofauti gani hao unaodai hawana misimamo...?ama hakuna wagombea wengine ukiacha hao wawili..
huku si kujitekenya kisa kucheka mwenyewe..
huwezi kukandia ccm na Ukawa kisha ukatumia nguvu nyingi kumnadi Magufuli kana kwamba hakuna wagombea wa vyama vingine...
ila upinzani hauko tayari kuongoza nchi zaidi ya Sanaa za Ruzuku.
nasisitiza..unaongozwa na mihemko na hisia katika kufikiri yajayo huku ukifunika kombe tulioshuhudia yakitendeka kutoka chama tawala....