Ama kweli Lowassa amekwaa kisiki hatari!

Ama kweli Lowassa amekwaa kisiki hatari!

Labda tujaribu kuwa wabunifu kidogo...na tuache kutumia akili za misukule.....lowassa ndio raisi waawamu ya tano RIP ccm
 
mimi nakaa flat za lumumba hapa ila kila siku kuna vikao vya ghafula wanatetemeka jamani......sisi magufuli tunampenda lakini tatizo ni huyu sisiemu......
 
Pamoja na Kujiandaa Kuchukua nchi kwa zaidi ya miaka 25.

Pamoja na kuwanunua aslimia kubwa ya wahariri na waandishi wa kawaida wa vyombo vya habari


Pamoja na kuwanunua robo tatu ya wajumbe wa kamati kuu hadi kufikia hatua ya kum

Magufuli usikate tamaa ,watanzania wachache wenye uelewa na nchi yao wanatambua juhudi zako.!

Aya ya mwisho "Watanzania wachache" jua kuwa wengi hawamuelewi hivyo hawatapiga kura kwa CCM
 
Hakika ninawaeleza,hali ya CCM hivi sasa ni tete,waasisi wa kudondoka kwa CCM ni Viongozi wa CCM wenyewe!!Natarajia kura nyingi za CCM kwa UKAWA.Waliotoka CCM ni wengi mno,waliojitambulisha hadharani ni wachache wengi wanaugulia moyoni ni maelfu kwa maelfu!!
Nimezaliwa miaka ya 70 na nimeishi vijijini ndani kabisa katika mikoa zaidi ya nane (Njombe,Arusha,Kagera,Morogoro ,Iringa,Rukwa,Mbeya,Pwani na Tanga) mijini pamoja na nje ya nchi.Kati ya mataifa yaliyokuwa na rasilimali ambazo asilimia 90 ya watu wa Nchi hiyo hawanufaiki nazo ni Tanzania.Tuna kila ina ya madini.tuna gesi na makaa ya mawe,tuna mbuga na misitu.ardhi safi na vyanzo vya maji,bahari,milima na mabonde yenye rutuba.Wananchi wa Tanzania ni "maskini wa kutupwa" kuna watu kesho yao ni kitendawili kigumu na wengine wapo hata jiji maarufu la Dar es Salaam. Maisha yamekuwa maigizo. Takwimu zinaonesha ujinga umeongezeka kwa asilimia za kutisha,vijana wengi hawajui kusoma wala kuandika.Wanaendelea na masomo ya Vyuo Vikuu ni wale wenye uwezo wa fedha na mali.Wengi wameshindwa kuendelea kwa sababu hawana uwezo ni mikopo ina utata mwingi..Mpaka leo tunavyoandika magonjwa ambayo yametokomea duniani Tanzania ndio mahala pake.Jiji la Dar limekumbwa na ugonjwa wa aibu wa kipindupindu na wengi wameaga dunia kwa sababu ya uchafu.Mahospitalini wagonjwa wamelala mzungu wa nne kwa magonjwa mbalimbali na wakina mama wakijifungulia mitaroni ama vichochoroni!!!..Upande wa pili,watoto wa vigogo wanasoma nje ya nchi ama katika shule ambazo ada ya mwaka ni Milioni 80.Matibabu yao ya mafua na kikohozi ni ulaya na Marekani.Mavazi yao yamedizainiwa na Madizaina maarufu duniani.Mapumziko yao ni Vegas ama London.Benki zao ni Uswisi na Visiwa vya Uingereza. Vyakula vyao vinaagizwa kutoka Italy na Singapore,Usafiri wao ni ndege za kukodi na magari ya kifahari.Barabara za vumbi hawazijui asilani...Kuingangania CCM ni miongoni wa matatizo yetu Watanzania.Wakati umefika ni LAZIMA IONDOKE ili kama itakuwa na Jipya IJITAFAKARI.

uko vizuri. Hi ndio nchi ya kitu kidogo na ya watu wachache. Inauma sana watanzania tunadharaulika na nchi nyingine Kagame ni mfano mzuri
 
wengi malofa na wapumbavu katika ubora wao tutampa kura lowassa kwani tunaamini anakubalika na anauzika bila usumbufu. hayo ya mafioso na mafisadi unity yako huko ccm kwani ndio wanaonunua hata wapinzani ili wajitoe wabaki wao tu. Lowassa anasonga mbele na hakuna kisiki tena kwani njia inasafishwa na watanzania wapiga kura wenye kutaka mabadiliko ya mfumo kupitia sanduku la kura. pamoja na kumpa airtime vituo vyote vya luninga , pamoja na kuchana picha za mgombea wetu lakini hilo halitatubadili.
Pamoja na Kujiandaa Kuchukua nchi kwa zaidi ya miaka 25.

Pamoja na kuwanunua aslimia kubwa ya wahariri na waandishi wa kawaida wa vyombo vya habari


Pamoja na kuwanunua robo tatu ya wajumbe wa kamati kuu hadi kufikia hatua ya kumzomea Mwenyekiti.

Pamoja na kuvinunua vyama vikubwa vinne vya upinzani na yeye akiwa ndio mgombea pekee.

Pamoja na kumiliki mtandao mpana zaidi na wa hatari nchini Mafioso & Mafisadi Unity (MMU)

Lakini bado anaonekana kupwaya kwa Magufuli,alieanza harakati za urais juzi ,tena hana mtandao ,hana vyombo vya habari vya kueleweka hata ule mtandao hatari Mafioso & Mafisadi Unity (MMU) unamwogopa na kumwangalia kwa jicho la tatu.!

Magufuli usikate tamaa ,watanzania wachache wenye uelewa na nchi yao wanatambua juhudi zako.!
 
Ubogo wa samaki unakuja humu tutoa pumba wamekuonjesha pesa hapo ndo mwisho wa ubongo wako unamajukumu au unaishi kwa shemeji ako we pole na ccm yako
 
Kwenye mikutano yenu fanyeni haya halafu urudi tena hapa JF:

1. Msitumie malori kusafirisha watu
2. Msiwatangulize jukwaani akina daimond na ze komedi!

Kwani kuna tatizo gani kuleta watu wa maeneo ya mbali ambayo unaamini huwezi kufika ili waje wasikilize sera.Hicho kitu cha kujiamini na wingi wa watu kwenye mikutano kitawagharimu UKAWA.Binafsi nimeshuhudia watu wengi katika mazingira niliyopo wakihudhuria mikutano ya Wagombea wote wa Urais wanaokuja,lakini wanagawanyika sana ni yupi wampigie.Fanyeni siasa ya kisayansi.
 
Ubogo wa samaki unakuja humu tutoa pumba wamekuonjesha pesa hapo ndo mwisho wa ubongo wako unamajukumu au unaishi kwa shemeji ako we pole na ccm yako
Ungekaa kimya ingekua bora kuliko huu upuuzi uliouweka hapa.!
 
Upo bize kweli hapa JF kila thread kutetea ccm utafikiri utapiga kura mara milioni mbili kuokoa jahazi mfu ccm
wewe bawacha jitahidi umchgue magufuli achana na lile genge la wezi waliojikusanya wanajiita upawa.
 
11214338_10203843588288420_5482261875458435778_n.jpg
 
Back
Top Bottom