Maty
JF-Expert Member
- Aug 24, 2010
- 2,167
- 725
Tuliambiwa tukaujaze ulimwengu,sasa Paulin mpz ww ukikataa kuzaa inakuwaje?well nowdaiz kuna wadada weeeengi hawapendi kuzaa eti baada ya kuzaa shape yake itaharibika(Naomba usiingie ktk kundi hili)
- Wapo wanaozaa na kukataa kunyonyesha eti maziwa yatalala(Naomba usiingie ktk kundi hili)
No pain no gain,tabu zote utakazo pata,kutapika,mahasira,kusema sema ovyo,kuchukia watu,kutopenda kula etc yana mwisho mzuri ambao furaha yake haina kipimo kabisa na kila mtoto fuhara yake huja tofauti.
- Paulini kuna wanawake weeeeengi wanatamani kushika na kubeba,kunyonyesha mtoto lkn hawapati,kuna wanawake wanalia na Mungu usiku na mchana wapate japo mtoto mmoja lkn hawana mtoto,wapo wanaoenda kwa waganga na wametoa vitu vya thamani kubwa pia hawajapata mtoto
- Paulini mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu hivyo basi kwa wakati wake mtoto hupatikana na kwa wakati wake utajua na kuwa jasiri ktk malezi ya watoto,tena mama hodari sana ambae watoto wako watafata misingi bora ya maisha.Kila kitu na wakati wake.
-Pauline mama hana mpinzani usione tuko makazini kutwa masimu nyumbani"Dada amekunywa uji,ok so anacheza,vipi hana joto?muogeshe kidogo mbadilishe Daipaz,sa 5 mbembeleze alale akiamka saga chakula ndizi changanya na samaki alafu tengeneza juic ya embe,sa kumi ikifika mpe maziwa sawa eeeh?mkae salama mwanangu"
-Ma outings yana mda na wakati wake wa kuwa na mzee hilo halina mjadala lkn cha muhimu ni kupangilia mda wako vzr,kazi,mume/mtoto,marafiki na jamaa usisahau.
Pearl umenikumbusha mbali na kunifurahisha lol, hapo kwa simu tena itokee ulimuacha anaumwa ndio kabisaaa kila saa dada joto halijapanda, vp amekunywa uji, maziwa je? mpondee basi viazi umjaribishe kidogo. Anacheza!! kweli hebu nipe simu nimsikie kidogo anavyocheka basi ukisikia zile baba dada na yale makelele mengine roho inasuuzika kabisa.
Mi nakumbuka alivyokua akiumwa kuhara akilegea basi automatically na mimi nalegea, akichangamka na mimi naanza kuchangamka, jamani watu ambao huwa wanaondoka sijui anaacha mtoto hajui amekula au hajala au wengine anamtupa kijijini ye anaponda maisha nadhani huwa mioyo yao inahitilafu kidogo, kwani ile mama kujisikia vibaya mtoto akipata tatizo mbona ni natural jamani sa hao wenzetu wameumbwaje?