Umslopagazi
JF-Expert Member
- May 16, 2013
- 1,737
- 935
Habari za hivi Pundi Zilizotufikia kutoka kanda ya ziwa na kudhibitishwa na msemaji mkuu wa Chadema Tumaini Makene.
Kwa sasa inaweza kuthibitishwa rasmi na kwa usahihi kuwa ratiba ya kumpatia heshima za mwisho kumuaga kiongozi wetu mahiri na kipenzi cha watu Alphonce Mawazo imebadilika.
Baada ya mashauriano kupitia vikao yaliyofanyika takriban siku nzima ya jana hadi usiku, imekubalika kuwa Mawazo hatazikwa kesho Jumatatu kama ilivyokuwa imepangwa awali na leo hataagwa mjini Geita kama ambavyo wananchi walikuwa wameshataarifiwa kupitia njia mbalimbali.
Taarifa ya ratiba nyingine kuhusu utoaji heshima za mwisho kumuaga Mawazo na mazishi yake, itatolewa baadae.
Asanteni
Tumaini Makene
Kwani Makene ndio msemaji wa familia ya marehemu? Haya mambo mbona wanayafanya mtaji wa kisiasa!