Alpha na Omega ya historia ya Israeli ya kale

Hawa waizrael wa 1948 waliingia palestina iliyokua inakaliwa nA waarabu na wakaigawa palestina ili taifa jipya la israel liundwe
Sasa ina maana hakukua na mipaka iliokua inatenganisha israel na palestina? Kabla hawa jamaa hawajaletwa
Walienda kuigawa palestina kwa sababu ndio ilikua sehem yao kabla hawajatawanyika....na wasingeweza kuwafukuza wapalestina kwani nao wengi wao walizaliwa pale baada ya mababu zao kuhamia wasingekua na pa kwenda
 
Walienda kuigawa palestina kwa sababu ndio ilikua sehem yao kabla hawajatawanyika....na wasingeweza kuwafukuza wapalestina kwani nao wengi wao walizaliwa pale baada ya mababu zao kuhamia wasingekua na pa kwenda
hamna logic hapo,walioishi hapo ni babu wa mababu wao miaka karibu 3000 nyuma,huwezi kurudi kudai ardhi baada ya miaka yote hiyo,
 
Mkuu Kimario hapa unazungumzia Israel kama nchi au Mu-Israel kama mwananchi wa taifa la Isarel?

Maana kama ni Israel as state tunaangalia Geographical location yake so kama Israel ya zamn na ya sasa ungetueleza ile ya zaman ilikua maeneo ya Iraq ila ya sasa imesogea apo Palestina.

Bt Israel kama wananchi wake kuna vitu unapaswa kuangalia ili ukete FACTS zenye ushawishi na si simulizi uchwara kama hii.

Kati ya vitu ambavyo ungeainisha
1. Lugha asilia ingawa watu wanaweza izungumza lakn tunajua English niya malkia. Hivyo tueleze lugha.

2. Makabila, tueleze palkua na makabira haya sahv makabira yale wapo Rwanda na c Israel ya sasa.

3. Tamaduni.Kwamba waisrael wa mwanzo walikuwa na tamaduni hiz ila hawa wana tamadun hz. Hapa ni pamoja na sherehe nk.


Haya ni baadhi ya mambo unayoweza tumia kutetea mada yako hiyo na c kama ulivoeleza.
Mkuu shida yangu ni kwamba kama maangamizi ya yerusalem mwaka 70bk ndio ulikua mwisho wa israeli ya kale na kizazi chake je hawa wayahudi wa sasa ni kizazi cha nani? Kati ya yakobo na esau
Na hawa jamaa walifika vipi ulaya hadi zikaanza harakati za kuwapa nchi ya kukaa
 
Judah Alkalai NA
Yehuda Bibas movement ilianza na hawa kabla ya huyu jamaa yeye alisoma habari na motivations za hao babu zake wayahudi mmoja aliishi hispania na kufukuzwa akakimbilia afrika kazkazini.
Ila hii ya leo Ilizanza kwa vuguvugu la vijana wazayuni waliokuwa wanakaa kijijini kabisa Poland enzi hizo iko Russia. Kiongozi wao akiwa ni David Ben gulion. walijiorganize hadi 1906 wakahamia palestina enzi hizo kulikuwa na wayahudi 55000 na kati ya hao 40000 bado walikuwa na uraia wa Urusi.
Lakini wao wanaamini uraia au uisrael wao hauhesabiwi kwa mipaka ya ardhi bali ni kwa Moyo. hATA AWE WAPI YEYE NI MUISRAEL. ANGALIZO SIONI UHUSIANO WA WAISRAEL HAWA NA MAMBO YA KIDINI.
KUKUKUMBUSHA KAMA WALIKUWEPO PIA BAADA YA 70AD. ISLAMIC CALPHATE CHINI YA CALIPH UMAR WALIITEKA NA WAYAHUDI WOTE WAKAWA KOLONI LA HUYO JAMAA, NA VIPINDI VYOTE VYA CLUSADE WAYAHUDI WALIKUWEPO NA WAKRISTO WACHACHE PIA.
Thanks mseza mkulu so hii ni israeli ya watu gani mkuu kama sii wale wa kidini
 
Nilijua unapoint lakini baadae nikagundua lengo lako kuu n kuwafutia uteule waliopewa waisrael!! Binadam wana mambo!! Alichotoa Mungu hakinyang'anyiki
Point ipo mkuu je uteule wao tunajua ulitokana na ibrahim isaka na yakobo na kizazi chake hawa ndio waisraeli wateule wa mungu je israel hii ya sasa ya 1948 ndio kizazi hiki au ni vipi?
 
Mkuu shida yangu ni kwamba kama maangamizi ya yerusalem mwaka 70bk ndio ulikua mwisho wa israeli ya kale na kizazi chake je hawa wayahudi wa sasa ni kizazi cha nani? Kati ya yakobo na esau
Na hawa jamaa walifika vipi ulaya hadi zikaanza harakati za kuwapa nchi ya kukaa
mwaka 70 bk ,sidhani kama warumi walichukuwa watu kuwapeleka utumwani,kulitokea uasi jerusalem kupinga utawala wa warumi,alieongoza uasi alijiita kuwa masihi aliyetabiliwa kuja kuwakomboa wayahudi toka mikononi mwa warumi,
kabla ya hapo unakumbuka yesu nae aliwahi kuja na madai hayo ya kwamba kaja kuwakomboa wayahudi na akajiita yeye ndo mfalme wa israel na akaingia jerusalem kwa maandamano kwamba yeye ni mfalme,kitendo kilichopelekea warumi wamkamate na kumsulubu,
huyu masihi wa mwaka 70 yeye hakutumia maandamano,bali alitumia vita,warumi walizima uasi na kuchoma moto hekalu na baadhi ya nyumba za wayahudi pale jerusalem
 
Point ipo mkuu je uteule wao tunajua ulitokana na ibrahim isaka na yakobo na kizazi chake hawa ndio waisraeli wateule wa mungu je israel hii ya sasa ya 1948 ndio kizazi hiki au ni vipi?
nijuavyo mimi ule uteule ni wa kutunga tu,lakini pia kile kizazi si hiki cha mwaka 1948,wakati wanahamishwa utumwani,si kwamba taifa lote lilienda utumwani,ni watu wachache tu kwa mamia ambao kuna baadhi walirudi,baadhi walitokomea mpaka nchi za ulaya,baadhi walibaki uhamishoni mfano kule iran mpaka leo kuna wayahudi
 
nijuavyo mimi ule uteule ni wa kutunga tu,lakini pia kile kizazi si hiki cha mwaka 1948,wakati wanahamishwa utumwani,si kwamba taifa lote lilienda utumwani,ni watu wachache tu kwa mamia ambao kuna baadhi walirudi,baadhi walitokomea mpaka nchi za ulaya,baadhi walibaki uhamishoni mfano kule iran mpaka leo kuna wayahudi
Mkuu elungata tunaona musa akiwatoa wana israel nchini misri kwa ahadi ya mungu
Pia tunamuona yoshua akichukua kijiti kuwafikisha waisraeli katika nchi ambayo mungu aliwapa ya kanaani
Hii kanaani ilikua pia na watu lakini mungu alishwapa waisrael nchi ile so hii nchi ya kanaan ambayo waisrael walipewa na rasmi ikaitwa israeli badala ya kanaan
Swali linakuja kama kanaani ilikua imepakana na wafilisti ambayo watu wanadai ndio palestina ya sasa ilikuaje hawa wayahudi wakaingia palestina badala ya kanaani walikokua mwanzo? Je hii kanaani kwa sasa inajulikana vipi hivi sasa naamini utanielewa vizuri hapa
 
Thanks mseza mkulu so hii ni israeli ya watu gani mkuu kama sii wale wa kidini
Namaanisha nini?
Ni kweli Historia ya Wayahudi inakuwa traced kuanzia Adam hadi yakobo katika bibilia. Na hapo walipo sasa ni kweli palinunuliwa na Babu yao kwa mujibu wa kifungu cha bibilia., Na hata safari yao kutoka Misri walikuwa wanakwenda hapo walipo sasa. hata baada ya yesu kupigwa kwa yerusalem na wao kusambaratika na kukimbilia sehemu mbalimbali ulaya na afrika na baadae baadhi yao wakajikusanya na kurudi hao wachache tu maana wengi karibu3/4 wamesambaa dunia nzima.

Mimi naanini Hapo walipo ni sahihi na ni sehemu yao wanapaswa kuwa. Ila hao waliopo kuna watu wanawanyenyekea kama wana upendeleo flani wa kidini. Sioni kama ni sahihi. Ikija suala la Mungu kila mmoja anawajibika kufuata utaratibu wake sio Muisrael wala Msukuma. They are all equal before God.Kwa kusema hivyo nikimaanisha hao waliopo ni taifa tu kama Tanzania na wanapaswa kufuata utaratibu wa Mungu na kuacha mambo yao kama kuwauwa waparestine, etc

Walirudi vipi,kwa mbinu zipi,kwa nini walikataa walipopewa ardhi na UN kati ya Uganda na Kenya au ethiopia wakaamua kwenda eneo lenye jangwa,madimbwi yaliyojaa mbu. etc hapo sioni Dini ni mikakati yao ya kisiasa ila Ndio hao hao wala sio kweli ni watoto wa hesau.
 
Mkuu elungata tunaona musa akiwatoa wana israel nchini misri kwa ahadi ya mungu
Pia tunamuona yoshua akichukua kijiti kuwafikisha waisraeli katika nchi ambayo mungu aliwapa ya kanaani
Hii kanaani ilikua pia na watu lakini mungu alishwapa waisrael nchi ile so hii nchi ya kanaan ambayo waisrael walipewa na rasmi ikaitwa israeli badala ya kanaan
Swali linakuja kama kanaani ilikua imepakana na wafilisti ambayo watu wanadai ndio palestina ya sasa ilikuaje hawa wayahudi wakaingia palestina badala ya kanaani walikokua mwanzo? Je hii kanaani kwa sasa inajulikana vipi hivi sasa naamini utanielewa vizuri hapa
hakukuwepo ufalme wa caanan,caanan ilikuwa ni jina la eneo ambamo ndani yake zilikuwemo tawala nyingi wakiwemo wafilisti.
Jaribu kupiga picha ya caanan kama tuseme africa mashariki.
Waisrael walipokuja toka misri kuja caanan hawajakuta utawala wa caanan,bali walikuta tawala nyingi wakiwemo wafilisti.
Hata baada ya kuanzisha tawala ya israel,ukweli ni kuwa vita hapo haikutulia kamwe,kumbuka miaka karibu 300 baada ya waisrael kufika caanan ,ndipo daudi aliweza kuiteka jerusalem toka kwa wajebu.
Mfano kipindi cha samson,israel ilikuwa inatawaliwa na wafilist katika baadhi ya maeneo,kwa miaka yote mambo eneo hilo yalikuwa yanabadilika kutokana na nani aliekuwa nguvu kijeshi,hata utawala wa uyahudi na israel zilikuwa ni falme ndogo kulinganisha na falme kubwa kama babel,asyria na misri.
Tukija pia kuhusu palestina,lilikuwa ni jina la eneo hilo baada ya caanan,ndani yake zikiwemo jamii mbalimbali ndani yake lakini zikitawaliwa na warumi,so wakaazi wa eneo hilo bila kujali kabila walijulikana kama wapalestina.
 
Hivi mkuu unajua kuna izraeli 2 ?
Kuna izrael ya kale ambayo naizungumzia hapa pia unaipata kwenye bible
Lakini pia kuna hii izraeli iliozaliwa 1948 hii sii izraeli ya taifa la mungu ni izraeli nyingine kabisa
Sasa kwa akili zako baada ya maangamizi ya yerusalemu ya mwaka 70k ulitaka israeli ya kale iendelee ku exist tuu?..na hayo maangamiz ya kale yalitabiriwa kibiblia ili watawanyike na baadae kuja kuunganishwa kuwa taifa moja...soma kitabu cha ezekiel utaelewa hii kitu.....
 
Hizi kk ndo nini slafu mbona zinapungua tu1200 kk
Hafi 587 kk, kisha mia 140 kk hadi 63 kk zamani miaka ilikuwa ikirudi nyuma?
 
Sasa kwa akili zako baada ya maangamizi ya yerusalemu ya mwaka 70k ulitaka israeli ya kale iendelee ku exist tuu?..na hayo maangamiz ya kale yalitabiriwa kibiblia ili watawanyike na baadae kuja kuunganishwa kuwa taifa moja...soma kitabu cha ezekiel utaelewa hii kitu.....
ukifanya research utagundua kuwa baada ya sekeseke la mwaka 70AD,hawakutanyika.
Nakumbuka mtawanyiko ulianza miaka mingi kabla ya hapo wakati wa asyria walipouvamia kingdom of israel na makabila ya 10 ya israel ndo yakatawanyika,na haya hitwa makabila yaliyopotea ya wana wa israel,baada ya hapo ulibaki utawala wa yuda ambao ulidumu kwa miaka zaidi ya 100 kabla wababel hawajavamia na kuutawanya ufalme wa yuda.
Baada ya hapo kwa mamia ya miaka hapakuwepo na israel.
Hadi wanakuja kutawala warumi hapakuwepo na utawala wa israel bali herode alitawala kwa amri kutoka Roman empire.

Hadi anazaliwa yesu,hapakuwa na israel,yesu anakua mpaka anafarika miaka 35 baadae hakuna israel,kisha miaka 35 baadae yaani mwaka 70AD ,ndo pakatokea yale maasi,ambayo yalipelekea warumi kulichoma moto hekalu,mda wote huo hilo eneo liliitwa palestina officially,

lakini tena ukumbuke miaka mingi baadae,karibu miaka 500 ndipo waarabu nao wakaanza kuliteka eneo hilo,kwamaana ya tawala mbalimbali za kiarabu na pia persian,mongolia,waturuki na hatimaye British Empire ambao baada ya vita kuu ya pili ya dunia,waliwarubuni waarabu wakaasi utawala wa ottoman empire ambao kwa wakati huo ukitawala eneo lote mpaka palestina.
Baada ya waturuki kushindwa na palestina ikawa chini ya udhamini wa british empire .
Ni waingereza ambao baadae waliwezesha wayahudi kurudi palestina kwa maelewano ya kuishi miongoni mwao na jamii waliyoikuta pale,yaani wapalestina.
Wayahudi walinunua maeneo machache then wakaanzisha vita na hatimaye 1948 wakajitangazia uhuru
 
Sasa kwa akili zako baada ya maangamizi ya yerusalemu ya mwaka 70k ulitaka israeli ya kale iendelee ku exist tuu?..na hayo maangamiz ya kale yalitabiriwa kibiblia ili watawanyike na baadae kuja kuunganishwa kuwa taifa moja...soma kitabu cha ezekiel utaelewa hii kitu.....
Najua unasema kuhusu 66/8 lakini mi nakataa kwa kua taifa hili la kisasa halisemi kua lilichaguliwa na mungu bali lilitokana na mkataba wa umoja wa mataifa
Ben gurion mwenyewe alikataa taifa hilo kuutwa mungu wa israel bali akasema iitwe mwamba wa israeli
Kweli mungu alitimiza unabii wake kwa israel karne ya 19? Jibu ni hapana kwa sababu unabii wa isaya 66/8 ulitimia hapa ezra 1/2
Jipange upya
 
Hizi kk ndo nini slafu mbona zinapungua tu1200 kk
Hafi 587 kk, kisha mia 140 kk hadi 63 kk zamani miaka ilikuwa ikirudi nyuma?
kabla ya kristo,yaani kabla hajazaliwa yesu,miaka ilikuwa inapiga rivasi,
yesu mwenyewe kazaliwa arround4AD, mwaka wa nne baada ya kuzaliwa yesu
 
Walienda kuigawa palestina kwa sababu ndio ilikua sehem yao kabla hawajatawanyika....na wasingeweza kuwafukuza wapalestina kwani nao wengi wao walizaliwa pale baada ya mababu zao kuhamia wasingekua na pa kwenda
Sawa ila nikuulize wakati wa yesu israeli ilikupo na palestina ilikuepo si ndio na kuna watu wanadai palestina ndio filisti ya zamani na tunajua filisti na israel ilikua ni nchi 2 tofauti na hata vita ya goliati ambae alikua mfilisti na daudi ambae alikua mwisrael sio
Sasa kama palestina ndio ilikua nchi ya wafilisti zama hizo je kanaani waliopewa waisrael iko wapi hivi sasa?
 
ukifanya research utagundua kuwa baada ya sekeseke la mwaka 70AD,hawakutanyika.
Nakumbuka mtawanyiko ulianza miaka mingi kabla ya hapo wakati wa asyria walipouvamia kingdom of israel na makabila ya 10 ya israel ndo yakatawanyika,na haya hitwa makabila yaliyopotea ya wana wa israel,baada ya hapo ulibaki utawala wa yuda ambao ulidumu kwa miaka zaidi ya 100 kabla wababel hawajavamia na kuutawanya ufalme wa yuda.
Baada ya hapo kwa mamia ya miaka hapakuwepo na israel.
Hadi wanakuja kutawala warumi hapakuwepo na utawala wa israel bali herode alitawala kwa amri kutoka Roman empire.

Hadi anazaliwa yesu,hapakuwa na israel,yesu anakua mpaka anafarika miaka 35 baadae hakuna israel,kisha miaka 35 baadae yaani mwaka 70AD ,ndo pakatokea yale maasi,ambayo yalipelekea warumi kulichoma moto hekalu,mda wote huo hilo eneo liliitwa palestina officially,

lakini tena ukumbuke miaka mingi baadae,karibu miaka 500 ndipo waarabu nao wakaanza kuliteka eneo hilo,kwamaana ya tawala mbalimbali za kiarabu na pia persian,mongolia,waturuki na hatimaye British Empire ambao baada ya vita kuu ya pili ya dunia,waliwarubuni waarabu wakaasi utawala wa ottoman empire ambao kwa wakati huo ukitawala eneo lote mpaka palestina.
Baada ya waturuki kushindwa na palestina ikawa chini ya udhamini wa british empire .
Ni waingereza ambao baadae waliwezesha wayahudi kurudi palestina kwa maelewano ya kuishi miongoni mwao na jamii waliyoikuta pale,yaani wapalestina.
Wayahudi walinunua maeneo machache then wakaanzisha vita na hatimaye 1948 wakajitangazia uhuru
Mkuu ni kwa nini wakristo wamepungua sana palestina na inasemekana wengi wao wamekimbia kwa kua wanabaguliwa na wapalestina kwa kua ni kundi dogo hii imeekaaje kuna ukweli hapa?
 
Ukoo wa esau mtoto mkubwa wa isaka na ambaye alikuwa pacha wa jacobo walikuwa wameweka makazi yao hapohapo caanan,na utawala wao ukiitwa kingdom of Edom,baadae nikipata mda ntajaribu kuweka ramani,
lakini pia arround caanan zilikuwepo tawala zingine mfano Moab kingdom,Amon kigdom,phoenicia,hittite,filist na makabila mengine mengi,
kusema kweli eneo ambalo halikukumbwa na hamahama ni Gaza.
Tangu enzi za abraham gaza haijabadilika hata ukicheki raman hiyo hapo juu utaona kuwa waisrael hawakupata kuiweka gaza katika mamlaka yao toka zamani,
hata miaka ya karibuni walipoikalia baadae waliiacha
 
Mkuu ni kwa nini wakristo wamepungua sana palestina na inasemekana wengi wao wamekimbia kwa kua wanabaguliwa na wapalestina kwa kua ni kundi dogo hii imeekaaje kuna ukweli hapa?
wamepungua katika maeneo ya israel,,katika palestina mfano bethlehem,wakristo ni wengi kwani kipindi cha xmas huonagi rais wa palestina katika mkesha?
Hata wakati wayahudi wanarudi na kuanzisha harakati zao wakristo na wapalestine walikuwa pamoja agaisnt,ujue mkirsto wa palestina sio mzungu,ni mpalestine wa kuzaliwa
 
Back
Top Bottom