Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,106
Nimpongeze Karibu Mkuu aliyetanguliwa wa Wizara ya Mambo ya Ndani mdogo wetu Gaspar Mamuya kwa utumishi wa kukumbukwa katika wizara hiyo. Huyu Bwana niliwahi kukutana naye kwenye mgogoro flani wa taasisi za dini, alitoa ushauri kama mzazi na hakuwa na majivuno.
Pamoja na hayo wizara ilitulia sana na kelele za kubambikiwa kesi watu zilipungua. Nidhamu ya polisi ilikuwa kubwa na hatukuona makaripio au kutunishiana misuli kwenye vyombo vya habari.
Upole wake sidhani kama ungemwacha atulie katika wizara hiyo kuelekea uchaguzi. Kipindi cha uchaguzi ndipo wizara ikabidhiwa watu wa vurugu na wanaoweza kusimamia yasiyoweza kusimamiwa
Katibu Mkuu mpya wa wizara ya mambo ya ndani ni nani? Amewahi kufanya kazi maeneo gani na ufanisi wake upoje? Je ameteuliwa kama mwana mtandao wa goli la mkono au anakwenda kusimamia uchaguzi wa haki?
Pamoja na hayo wizara ilitulia sana na kelele za kubambikiwa kesi watu zilipungua. Nidhamu ya polisi ilikuwa kubwa na hatukuona makaripio au kutunishiana misuli kwenye vyombo vya habari.
Upole wake sidhani kama ungemwacha atulie katika wizara hiyo kuelekea uchaguzi. Kipindi cha uchaguzi ndipo wizara ikabidhiwa watu wa vurugu na wanaoweza kusimamia yasiyoweza kusimamiwa
Katibu Mkuu mpya wa wizara ya mambo ya ndani ni nani? Amewahi kufanya kazi maeneo gani na ufanisi wake upoje? Je ameteuliwa kama mwana mtandao wa goli la mkono au anakwenda kusimamia uchaguzi wa haki?