All good men are married, so sad

Hapo kwenye sifa za huyo mwanaume tu ndio mnapokosea wadada, mnapenda waume za watu kuliko waume zenu mnaostahili, tatizo wamawake wengi siku hz wanafikiria kupata wanaume waliofanikiwa and stable financially pasipokujua most of them wako occupied. Mimi ushauri wangu jaribu kuondoa hiyo pointi ya AWE NA UWEZO WA KIFEDHA ama ile pointi ya AWE AMEFANIKIWA. Mtafute kikaragosi wako ambae ni kapuku tu awe msomi asiwe msomi, mpe changamoto, mmotivate, mpe akili (wanawake wanajua kushauri) shirikianeni kufanikiwa, sikudanganyi utafurahi na maisha, hautategemea kutafuta those financially stable, CREATE YOUR'S waoaji ni wengi sana
 
Hapo kwenye sifa za huyo mwanaume tu ndio mnapokosea wadada, mnapenda waume za watu kuliko waume zenu mnaostahili, tatizo wamawake wengi siku hz wanafikiria kupata wanaume waliofanikiwa and stable financially pasipokujua most of them wako occupied. Mimi ushauri wangu jaribu kuondoa hiyo pointi ya AWE NA UWEZO WA KIFEDHA ama ile pointi ya AWE AMEFANIKIWA. Mtafute kikaragosi wako ambae ni kapuku tu awe msomi asiwe msomi, mpe changamoto, mmotivate, mpe akili (wanawake wanajua kushauri) shirikianeni kufanikiwa, sikudanganyi utafurahi na maisha, hautategemea kutafuta those financially stable, CREATE YOUR'S waoaji ni wengi sana
Tho hakuna sehemu nimetaj ninataka mwenye pesa ila naomba nikujibu, kwa ustaarabu kabisa, hivi unadhani miaka hi yote sikuwahi kumtengeneza mu ambae hakuwa na maisha? kwa taarifa yako nilikuwa kwenye mahusiano huyo mtu nilimkuta akiwa na maisha kawaida tumefanya mengi akawa ninavyotaka mimi tho yeye ndo alikuwa mtoa pesa mimi msimamizi , mshauri mzuri, for 4good years nilikuwa nimemsubiri yakatokea ya kutokea tukaachana. kwa sasa anamiliki mamilion ya kutosha tu ila mimi ndo nilikuwa msingi fanya hiki fanya kile. je kwa hali kama hiyo bado unanion anapenda hela kiasi kwamba niokote yeyeote? so shida nilizozipitia unataka nizirudie kisa natafuta ufalme wa mbinguni? ninahitaji kupumzika. nina kazi yangu nina ka uwezo ka kujihudumia bila kumtegemea mtu. ndo maana natafuta mzee mwenzangu.

hayo maneno yako uwambie wanawake ambao wana umri kama wangu hawajui cement ni sh ngapi sio mimi sio mimi anaejua cement kiasi hiki inachanganya na mchanga kiasi hiki.

kwenye uzi wangu sikuandika mambo ya pesa ila kwakuwa umetaka kujua kilichopo moyoni mwangu. nachukua nafasi hii kukwambia hao uloita vikalagosi sichukui maana mimi sio kikalagosi, mme akikosa ntamkubali huyo mme wa mtu coz he is smart gentle , well off, in short he has everything I need. sitokuwa wa kwanza na wa mwisho kufanya hivyo.

my dia usipende kuhukumu hujui mtu amepitia yapi. pia nisamehe kama kuna sehemu nimekukwaza.
 
Kuna mwenzako kastaafu kwa hiyari Hana mtoto Hana mume,
Sasa wewe hapo una miaka mitano tu ya kumtafuta mtoto alafu unaleta ujanja ujanja hapa, Mana Kama ulivunja ungo na Miaka kumi ukifikisha 40 Kwisha kazi.
 
Duh...Umetoa changamoto ambayo pia ni funzo sio kwao tu bali pia kwa Wengine..!
Kuingia Kiwanja chenye Mgogoro ni shida Kwa Wanaume na Wanawake..!
 
Kila la kheri dear upate hitaji lako. Naelewa sana feeling ya kuhitaji kitu fulani ila hakitokei au kinatokea tofauti inaumiza sana.

Ukimpata utuletee mrejesho eeh.
 
Hao waume wa watu unaowaona wako caring,wametengenezwa kuwa hivyo na wake zao..na wengine wako hivyo hasa kwa ladies ambao hawajaolewa lengo ni muwape mbususu tu siyo kwamba wanawapenda...Trust me 98% ya wanaume waliooa wameoa wanawake wanaowapenda ila tamaa tu huwafanya wachepuke na kujifanya wanapenda zaidi michepuko ila siyo kweli...Yes wako stable financially after years of hustling na wake zao...so na wewe angalia mtu mwenye sifa za nje then funga ndoa mtengeneze maisha pamoja.

Ninachoweza kukushauri tu unaelekea kwenye menopause hivyo changamka usije shindwa kupata mtoto
 
salaam.

Ama kweli wanaume smart wanao jitambua wanaojua thamani ya mwanamke, wote wameoa inasikitisha sana.

Hivi inawezekana vipi kila mwanaume anae onesha interest kwangu nikamuelewa nikija kumcheki kidoleni nakutana na pete? Hivi ni mimi tu au na wanawake wengine wanakutana na changamoto hii?

Wakuu, sio kwamba wanaume waoaji hawapo, wapo tena wengi sana tatizo ni je huyo anaekuja moyo umempenda? mtu wa kuishi nae lazima moyo umpende.

Je ina maana wakaka ambao hamjaoa ni kweli kwamba hamna sifa kama za hawa married men? kweli hampo?
Nimekuja hapa kusema la moyoni na si kwamba huku ninapoishi hakuna wanaume, wanaume wapo ila wengi wao wameoa, amHbao hawajaoa unakuta moyo haujampenda.

Umri umeenda ninahitaji kuwa na familiya ambayo nitakuwa huru nayo bila lawama. Niwe wazi kuna mtu yupo tiyari kwenda kwetu hata leo tatizo ni mme wa mtu. ana kila sifa ya mwanaume ninaemtaka lakini tatizo ndo hilo. Sijaingia mahusiano nae kwa sababu zifuatazo:,

1: Nitamwambia nini mama?
2: Namuogopa Mungu,
3: Familiya yake wakijua nitafanyaje mimi?
4: Nitakosa raha ya kuwa nae huru, nitakosa raha ya kuwa karibu na ukweni ( mbaya sana)
5: Nitalaumiwa na jamii etc

Hivyo basi nikaona siwezi hiki kiwanja chenye mgogoro, I deserve to have my own family:

Wewe mwanaume,
1) umri 37-45
2) mkristo mcha Mungu ukiwa RC itapendeza
3) Mchapa kazi haswaaa, mtafutaji kama mimi ( staki mwanaume anaelialia yeye kila siku hana hela lawama haziishi huyu hapana)
4) Anajipenda na anapenda kuishi maisha safi
5) mrefu
6)caring person, etc

Kama una hizo sifa njoo pm.
hakuna mtu asiependa vitu vizuri, hakuna asiependa mafanikio, ndo maana nimekuja hapa maybe nikakutana na mtu ambae tunaendana.

Kuhusu mimi,
1: age 35 ndo maana natafuta mzee mwenzangu.
2) sina mtoto, sijawahi kuolewa ila mwanaume huyo akiwa na mtoto mmoja na hana mgogoro na mzazi mwenzie mtamlea coz I like kids.
3) Elimu chuo kikuu
4) Kazi ninayo
5) kinywaji situmii
6) Rangi , rangi safi ya kati situmii mikorogo
7) Dini RC
8) mchapa kazi haswaa with brain.

Mume wangu nimechoka kukusubiri, nimekufuata huku nisije angukie mikononi mwa mme wa mtu. tho ana kila kitu ninachokitaka lakini nikikumbuka mme wa mtu sumu nalia, usichelewe plz nina muda mchache wa kufanya maamuzi.

GOD BE WITH YOU.
Nina 52, sifa nyingine zote ninazo... njoo mrembo tuyajenge, ulichonifurahisha hukuomba nauli maana wenzako wanatuazibu Sana wazee pendapenda!
 
Nina 52, sifa nyingine zote ninazo... njoo mrembo tuyajenge, ulichonifurahisha hukuomba nauli maana wenzako wanatuazibu Sana wazee pendapenda!
ahaaaa ndio mimi siombagi visent vidogo kama vi 50000 lakini najiuliza hata wewe 52yrs nauli inakua shida? nauli ya bus ama ndege? maana mimi kama ni mbali sipandagi basi sipendi kujitesa. unamaanisha nauliipi unombwa?

note ikitokea nikaomba naomba kapesa karefu sana so usinione malaika kiviile, ila mimi vipesa vya vocha sijui na ujinga mwingine hapana siombi. hivo ninanishushia heshima. afu mwanaume ukimuomba vipesa vidogo ni kama dhalau.
vip bado unanitaka nimejaribu kuwa muwazi.
 
ahaaaa ndio mimi siombagi visent vidogo kama vi 50000 lakini najiuliza hata wewe 52yrs nauli inakua shida? nauli ya bus ama ndege? maana mimi kama ni mbali sipandagi basi sipendi kujitesa. unamaanisha nauliipi unombwa?

note ikitokea nikaomba naomba kapesa karefu sana so usinione malaika kiviile, ila mimi vipesa vya vocha sijui na ujinga mwingine hapana siombi. hivo ninanishushia heshima. afu mwanaume ukimuomba vipesa vidogo ni kama dhalau.
vip bado unanitaka nimejaribu kuwa muwazi.
We ndio mrembo wangu, malaika kwangu.... wekeza mawazo kwenye pendo letu, Bado moyo wangu unakuhitaji uniondolee upweke niliokuwanao.

Vumulia kidogo, Kila mmoja ale mshahara wake... Ila baada ya miaka 8 mzigo wa pspf utakuhusu kama hutojali

bado nakutaka malaika
 
We ndio mrembo wangu, malaika kwangu.... wekeza mawazo kwenye pendo letu, Bado moyo wangu unakuhitaji uniondolee upweke niliokuwanao.

Vumulia kidogo, Kila mmoja ale mshahara wake... Ila baada ya miaka 8 mzigo wa pspf utakuhusu kama hutojali

bado nakutaka malaika
changamsha kijiwe🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom