Uchaguzi 2020 Aliyemshauri Rais Magufuli alipatia, Kama asingezuia shughuli za kisiasa kwa muda wa miaka 5, uchaguzi huu angeshindwa vibaya sana

Mtarban

JF-Expert Member
Jan 14, 2015
3,818
5,007
Najaribu kuwaza Kama tokea 2015 Rais Magufuli angeruhusu shughuli za kisiasa kuendelea Kama ilivyokuwa kipindi Cha nyuma, na hivyo Wapinzani kupata fursa ya kufanya mikutano ya kisiasa Mara kwa Mara ili kuwaambia wananchi juu ya madudu ambayo yamefanyika ndani ya miaka 5, Basi uchaguzi wa mwaka huu Magufuli angeshindwa vibaya sana.

Alicheza karata zake vizuri, ingawa pamoja na Kwamba wapinzani wote walizibwa midomo, wakafungwa kamba wasifanye siasa, na hivyo yeye pekee kuzunguka nchi nzima kuwaeleza wananchi Yale anayoyafanya, lakini bado inaonyesha watu wanataka mabadiliko.

Upinzani unaonekana kupokelewa kuliko kawaida. Pamoja na kwamba watu wamepigwa swaga za madaraja, barabara, Ndege n.k lakini wanataka maisha Bora, ajira na huduma nzuri za afya, vitu ambavyo wamevikosa katika awamu hii.
 
Achana na Story za kwenye vijiwe vya kahawa wewe, upinzani wana mabadiko gani

Wanaona ajira ndio pointi, ajira ni tatizo dunia nzima, hao wapinzani wasikudanganye kwamba wakiingia ikulu wataajiri kila mtu anayehitimu labda kama wanataka waiingize nchi kwenye madeni yasiyolipika yatayopelekea wadai kuchukua miundombinu ili wajilipe kama ilivyo kwa ndugu zetu hapo.

Mapato ya airport na shirika lao la umeme yanaenda nje moja kwa moja kwa sababu ya madeni makubwa, kama hicho ndo tunataka tumpe nchi yule anaetumia ajali kuombea kura, eti maumivu aliyopata hatakubali mtu mwingine ayapitie, nani kasema wananchi tutapigwa risasi? Kifupi upinzani hamna jipya.
 
Kwa hiyo unamuunga mkono Rais kwa kuweka Sekta ya Ajira pembeni kwamba Kama angeipa kipaumbele Basi angekopa Sana? Hahahahahaha. Poor ideas
Kama una limit ya kufikiri usipende kusema umeelewa hadharani. Ulichonasa wewe sicho nilichotega. Si ajabu unakesha sana jitahidi kulala uboreshe ubongo wako.

Kama una uthibitisho kuwa hakujawa na ajira kwa takribani miaka 5 ulete. We kama umekosa ajira endelea kuomba Mungu akusogezee siku yako lakini usisingizie hajaajiri watu wanakula vitengo kila leo.
 
Achana na Story za kwenye vijiwe vya kahawa wewe, upinzani wana mabadiko gani kama sio upuuzi mtupu. Wanaona ajira ndio pointi, ajira ni tatizo dunia nzima, hao wapinzani wasikudanganye kwamba wakiingia ikulu wataajiri kila mtu anayehitimu labda kama wanataka waiingize nchi kwenye madeni yasiyolipika yatayopelekea wadai kuchukua miundombinu ili wajilipe kama ilivyo kwa ndugu zetu hapo, mapato ya airport na shirika lao la umeme yanaenda nje moja kwa moja kwa sababu ya madeni makubwa, kama hicho ndo tunataka tumpe nchi yule anaetumia ajali kuombea kura, eti maumivu aliyopata hatakubali mtu mwingine ayapitie, nani kasema wananchi tutapigwa risasi? Kifupi upinzani hamna jipya.
Na wale wastaafu waliokatwa mafao miaka yote ya ajira sasa wanasubiri mafao miaka 3
 
Kama una limit ya kufikiri usipende kusema umeelewa hadharani. Ulichonasa wewe sicho nilichotega. Si ajabu unakesha sana jitahidi kulala uboreshe ubongo wako.
Soma hapo ulichokiandika harafu ukitafakari ili uelewebkuwa unamaanisha Nini. Unaandika harafu hujui unachokimaanisha. Lakini pia jipe muda wa kupitia Deni la taifa na pia ujue kuanzia 2015 Hadi Sasa nchi imekopa kiasi gani na Rais Ni wa chama gani.

Wanaona ajira ndio pointi, ajira ni tatizo dunia nzima, hao wapinzani wasikudanganye kwamba wakiingia ikulu wataajiri kila mtu anayehitimu labda kama wanataka waiingize nchi kwenye madeni yasiyolipika yatayopelekea wadai kuchukua miundombinu ili wajilipe kama ilivyo kwa ndugu zetu hapo, mapato ya airport na shirika lao la umeme yanaenda nje moja kwa moja kwa sababu ya madeni makubwa
 
Kama una limit ya kufikiri usipende kusema umeelewa hadharani. Ulichonasa wewe sicho nilichotega. Si ajabu unakesha sana jitahidi kulala uboreshe ubongo wako. Kama una uthibitisho kuwa hakujawa na ajira kwa takribani miaka 5 ulete. We kama umekosa ajira endelea kuomba Mungu akusogezee siku yako lakini usisingizie hajaajiri watu wanakula vitengo kila leo.
Madaktari na walimu wanaomaliza vyuo vikuu serikali ya awamu ya 5 imewaajiri kwa wingi sana mpk wengine wanakataa kazi hizo.

Awamu ya 5 oyeeeeee.
 
Soma hapo ulichokiandika harafu ukitafakari ili uelewebkuwa unamaanisha Nini. Unaandika harafu hujui unachokimaanisha. Lakini pia jipe muda wa kupitia Deni la taifa na pia ujue kuanzia 2015 Hadi Sasa nchi imekopa kiasi gani na Rais Ni wa chama gani...
Otober si mbali kuyajua mawazo na maamuzi ya raia wa Tanzania.
 
Najaribu kuwaza Kama tokea 2015 Rais Magufuli angeruhusu shughuli za kisiasa kuendelea Kama ilivyokuwa kipindi Cha nyuma, na hivyo Wapinzani kupata fursa ya kufanya mikutano ya kisiasa Mara kwa Mara ili kuwaambia wananchi juu ya madudu ambayo yamefanyika ndani ya miaka 5, Basi uchaguzi wa mwaka huu Magufuli angeshindwa vibaya sana...
Tofautisha siasa na shughuli za kiuchumi na maendeleo. Huwezi kuwa na flyover inayo rahisisha Usafiri ikawa sehemu ya maandamano,
Kisa ni haki za "watu".

Au unatakiwa kuwa shambani , mwingine anakuja na mkutano wa "kukupatia" huru au bei nzuri , hiyo bei nzuri utaipataje wakati haupo shambani?? Labda useme kwa kuwa mazao yatakuwa machache??
 
Alimshauri vibaya, sababu;

1. Ni ushauri unaovunja katiba. Wananchi wameingia mkataba na mtumishi wao yaani Rais ili ailinde na kuitetea katiba.

2. Ushauri huo umechochea hasira kwa wananchi maana pamapokuwa na freedom of assembly and freedom of expression, wananchi wanapata nafasi ya kusema yale yanayo waudhi.

Tunachokiona sasa hivi ni hasira ambayo wananchi wameiweka vifuani for the good five years under this sadist.
 
Back
Top Bottom