Aliyempigisha ‘deki’ Mwalimu aigomea CWT

Aliyempigisha ‘deki’ Mwalimu aigomea CWT

Na mwalimu nae jamani, mbona anakuwa muoga hivyo? Au ana vyeti feki? Kwani angekataa? Maana najua hata wangetunishiana misuri, mbele ya mahakama haki ingetendeka tu. Halafu bado tunawaza kuja kuwa na kizazi cha free thinkers? Kwa aina hii ya uoga wa walimu? Mungu aiingilie kati.
Nakubaliana nawe kabisa kama watanzania hatutajifunza kusema hapana, tunakoenda pabaya heshima itakuwa hamna tena. Kama kungekuwa na umuhimu wa kumueleza kitu au kumuonya angemwita ofisini kwake na kumueleza, huko ni kudhalilishana.
 
CWT NI....

.SANA yaani wanamtaka aombe radhi? kweli? hivi huyo mwalimu aliyedeki zipo sawa kichwani??? mfano asingedeki wangemfanyaje? naye hajielewi
 
Na mwalimu nae jamani, mbona anakuwa muoga hivyo? Au ana vyeti feki? Kwani angekataa? Maana najua hata wangetunishiana misuri, mbele ya mahakama haki ingetendeka tu. Halafu bado tunawaza kuja kuwa na kizazi cha free thinkers? Kwa aina hii ya uoga wa walimu? Mungu aiingilie kati.
Mkuu umenena jambo la maana sana,wakati wa kunyenyekea hadi upumbavu ushapita!kataa kwa nguvu zote unapoona dhahiri haki yako inapotea.Inauma sana!
 
ELIUD Mwaiteleke, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, aliyeamuru Hamis Sengo, mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Shilala kudeki darasa mbele ya wanafunzi ‘amekitolea nje’ Chama Cha Walimu (CWT) mkoani Mwanza baada ya viongozi wake kutaka kumuona na kumtaka aombe radhi.

Tukio la mkurugenzi huyo kumdhalilisha mwalimu huyo mbele ya wanafunzi wake, lilitokea Oktoba 17, mwaka huu shuleni hapo, baada ya ‘bosi’ huyo wa halmashauri kukuta baadhi ya madarasa yakiwa machafu.

Mkurugenzi Mwaiteleke akiwa ameambatana na maofisa wengine wa serikali ngazi ya wilaya hiyo, alifika shuleni hapo majira ya jioni na kumuita mwalimu (Sengo) ili aeleze kwanini madarasa ni machafu na kumtaka kudeki kitendo kilichotekelezwa na mwalimu huyo bila kupinga.

Sibora Kisheri, mwenyekiti wa CWT mkoani hapa amesema kuwa wamelipokea tukio hilo kwa masikitiko na kwamba wamemtaka mkurugenzi huyo kuomba radhi bila mafanikio.

“Tumefanya mazungumzo na tukaazimia kumtaka mkurugenzi huyo kuomba radhi na kumhamisha mwalimu huyo shuleni hapo kwa gharama zake na asifanye kitendo hicho kwa mwalimu mwingine.

Endapo mkurungezi huyo atashindwa kutekeleza maagizo hayo, tutachukua hatua kali zaidi kwani tumechoka kuonewa na viongozi wa serikali kila kukicha.

Kisheri amesema kuwa viongozi wa CWT walienda kuonana na mkurugenzi huyo lakini hakutaka kuonesha ushirikiano kwao na alidai kwamba leo anasafiri hawawezi kuonana na sisi.

“Mkurugenzi ni msimamizi wa watumishi lakini tunashangaa kuona kiongozi kama huyo anageuka kuwa mnyanyasaji na viongozi wasidhani kama sisi ni wanyonge, tunaweza kuchukua maamzi magumu zaidi ya hayo,” amesema Kisheri.

Alipopigiwa simu yake zaidi ya mara tano, ilikuwa ikiita na kukatwa lakini baadae ilipokelewa na mkurugenzi huyo kumtaka mwandishi kuwa yupo barabarani na hawezi kuzungumzia suala hilo.

Mkurugenzi: Nipo barabarani, sikusikii vizuri ni tukio gani?

Mwandishi: Ni tukio la kumuamuru mwalimu kudeki darasa ulilolifanya Oktoba 17.

Mkurugenzi: Ngoja nikutumie namba za afisa habari wa wilaya (Misungwi) atakueleza suala hilo.

Chanzo: Mwanahalisi Online

CWT hawana ubavu wa ku kumkabiri. Kama amefanya ufidhuri huo na aliyemteua hajamfukuza, basi ujue ana baraka zake. CWT wafanye kazi ya ziada
 
View attachment 421998 Tatizo nafasi hizi walizopewa hawa makada wenzangu zinawapwaya.Wanapenda kwenda na matukio,wanaiga mkubwa anachokifanya!!Wanafikiri kudhalilisha walimu ndio kuwawajibisha,kumbe kuna tofauti kubwa sana ya kuwajibisha na kudhalilisha.

Uwajibishaji kwa mtumishi wa umma unaendana na sheria,kanuni na taratibu,wakati kudhalilisha kunaendana na matamko,mihemuko na sifa za kijinga.Eliud hana uzoefu wowote wa kuwa mkurugenzi tena kwenye halmashauri kama ya Misungwi.

Nafasi za Ukurugenzi sio nafasi za u-DC,ambapo unaweza muokota mtu hata barabarani na ukampa hiyo nafasi.Ukurugenzi wa Halmashauri ni nafasi nzito,inayomtaka mtu kuwa na uzoefu usiopungua miaka 10 ndani ya utumishi wa Umma,ili kumfanya mtu awe mzoefu na kanuni,sheria na taratibu za kuongoza.

Eliudi aligombea ubunge wa CCM kura za maoni jimbo la Mbeya Mjini,kigezo chake ni ukada na si uweledi,asipokemewa kwa hili la kundekisha mwalimu,ipo siku anaweza fika Hospital ya Wilaya akamtaka nesi amchambishe....CWT mkomalieni huyu mpaka ajifunze.
Jitu lenyewe linaonekana muflisi kichwani hata kwa kuliangalia tu. Watu wanaofanya vitu vya ajabu ajabu wapewapo madaraka ukifuatilia historia zao huwa wamepitia maisha MABOVU na ya shida sana kwa kiasi ambacho tayari hali hiyo huwa imeshaathiri namna yao ya kufikiri katika mambo fulani.
 
Mbona kawaida sana, angewekwa lokapu sibora kudeki kuliko kulala ndani?, watanzania bana mambo mengine tunayakuza kweli, ni adhabu kama adhabu zingine jamani.
Kulala ndani ni kitu gani mkuu, hata ingekuwa kifungo cha maisha Kwa upande wangu ingekuwa poa tu, adhabu mbele ya wanafunzi hapo heshima hakuna tena na huyo Mwalimu nina uhakika amesha athirika kisaikilojia, ndio ile utakuta hata akipita kwenye kundi la wanafunzi wanacheka yao yeye lazima atajishtukia.. Bora kidogo ingekuwa mbele ya staff wenzake
 
Kulala ndani ni kitu gani mkuu, hata ingekuwa kifungo cha maisha Kwa upande wangu ingekuwa poa tu, adhabu mbele ya wanafunzi hapo heshima hakuna tena na huyo Mwalimu nina uhakika amesha athirika kisaikilojia, ndio ile utakuta hata akipita kwenye kundi la wanafunzi wanacheka yao yeye lazima atajishtukia.. Bora kidogo ingekuwa mbele ya staff wenzake
Basi sawa
 
CWT acheni ubabaishaji na kutuhadaa..

Mkurugenzi amefanya kazi yake kwa nia njema ya kuwarekebisha walimu vilaza..

Hamtamuweza Mkurugenzi... Ni boss wenu
 
Mi ningekuwa mwalimu nisingedeki ***** zake, mambo ya utwana hayo. Mi sijui niko tofauti, maana tangu nilivyokuwa mtoto sikuwa na nidhamu ya uoga. Yaani kwasababu we ni boss ndio unitelee mazereu, dah haitakaa itokee hiyo! Yaani ningemwambia kama unaona darasa chafu afadhari leo umekuja utusaidie kudeki.
 
Ila walimu nidham ya uoga inazid huo ni ujinga kwa mwalim kukubali kudeki inauma sana mi ni mwalim, ila huyo cjuwi kaa vyeti ni vyake
 
Kujitambua nako ni muhimu. Teachers need to know who they are and their rights. Unaambiwa upige deki eti nawe unainama kupiga deki. Huyo teacher pia ni tatizo. Ingekuwa mimi ningeshamng'oa meno huyo mkurugenzi. Imefikia hatua sasa ili mtu fulani aonekane anafanya kazi basi amnyanyase wa chini.
 
Back
Top Bottom