Aliyempigisha ‘deki’ Mwalimu aigomea CWT

Aliyempigisha ‘deki’ Mwalimu aigomea CWT

very sad sio haki kabsa hivo ni kumdharirisha mwalim
 
Walimu ni watu wa kuwaheshimu sana, wametutoa mbali, wamekubali ukweli kwamba wao ni madaraja ya kutuwezesha kwenda upande wa pili. Uzalilishaji wao sio jambo la busara, matukio tu kila kukicha kila mtu anajifanya Mungu mtu.
 
image.jpeg
Tatizo nafasi hizi walizopewa hawa makada wenzangu zinawapwaya.Wanapenda kwenda na matukio,wanaiga mkubwa anachokifanya!!Wanafikiri kudhalilisha walimu ndio kuwawajibisha,kumbe kuna tofauti kubwa sana ya kuwajibisha na kudhalilisha.

Uwajibishaji kwa mtumishi wa umma unaendana na sheria,kanuni na taratibu,wakati kudhalilisha kunaendana na matamko,mihemuko na sifa za kijinga.Eliud hana uzoefu wowote wa kuwa mkurugenzi tena kwenye halmashauri kama ya Misungwi.

Nafasi za Ukurugenzi sio nafasi za u-DC,ambapo unaweza muokota mtu hata barabarani na ukampa hiyo nafasi.Ukurugenzi wa Halmashauri ni nafasi nzito,inayomtaka mtu kuwa na uzoefu usiopungua miaka 10 ndani ya utumishi wa Umma,ili kumfanya mtu awe mzoefu na kanuni,sheria na taratibu za kuongoza.

Eliudi aligombea ubunge wa CCM kura za maoni jimbo la Mbeya Mjini,kigezo chake ni ukada na si uweledi,asipokemewa kwa hili la kundekisha mwalimu,ipo siku anaweza fika Hospital ya Wilaya akamtaka nesi amchambishe....CWT mkomalieni huyu mpaka ajifunze.
 
Kunahaja ya walimu kujitathimini upya na kujua maagizo halari yanayotolewa na wakuu wao! Sidhani kama wanapaswa kutekeleza kila agizo. Hii ni ishara kwamba viongozi wa juu ktk halmashauri na manispaa ndani ya kada ya Elimu wanaweza hata kutembea na walimu kwani inaonekana siyo wanaheshimiwa tu bali wanaabudiwa!!
 
ELIUD Mwaiteleke, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, aliyeamuru Hamis Sengo, mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Shilala kudeki darasa mbele ya wanafunzi ‘amekitolea nje’ Chama Cha Walimu (CWT) mkoani Mwanza baada ya viongozi wake kutaka kumuona na kumtaka aombe radhi.

Tukio la mkurugenzi huyo kumdhalilisha mwalimu huyo mbele ya wanafunzi wake, lilitokea Oktoba 17, mwaka huu shuleni hapo, baada ya ‘bosi’ huyo wa halmashauri kukuta baadhi ya madarasa yakiwa machafu.

Mkurugenzi Mwaiteleke akiwa ameambatana na maofisa wengine wa serikali ngazi ya wilaya hiyo, alifika shuleni hapo majira ya jioni na kumuita mwalimu (Sengo) ili aeleze kwanini madarasa ni machafu na kumtaka kudeki kitendo kilichotekelezwa na mwalimu huyo bila kupinga.

Sibora Kisheri, mwenyekiti wa CWT mkoani hapa amesema kuwa wamelipokea tukio hilo kwa masikitiko na kwamba wamemtaka mkurugenzi huyo kuomba radhi bila mafanikio.

“Tumefanya mazungumzo na tukaazimia kumtaka mkurugenzi huyo kuomba radhi na kumhamisha mwalimu huyo shuleni hapo kwa gharama zake na asifanye kitendo hicho kwa mwalimu mwingine.

Endapo mkurungezi huyo atashindwa kutekeleza maagizo hayo, tutachukua hatua kali zaidi kwani tumechoka kuonewa na viongozi wa serikali kila kukicha.

Kisheri amesema kuwa viongozi wa CWT walienda kuonana na mkurugenzi huyo lakini hakutaka kuonesha ushirikiano kwao na alidai kwamba leo anasafiri hawawezi kuonana na sisi.

“Mkurugenzi ni msimamizi wa watumishi lakini tunashangaa kuona kiongozi kama huyo anageuka kuwa mnyanyasaji na viongozi wasidhani kama sisi ni wanyonge, tunaweza kuchukua maamzi magumu zaidi ya hayo,” amesema Kisheri.

Alipopigiwa simu yake zaidi ya mara tano, ilikuwa ikiita na kukatwa lakini baadae ilipokelewa na mkurugenzi huyo kumtaka mwandishi kuwa yupo barabarani na hawezi kuzungumzia suala hilo.

Mkurugenzi: Nipo barabarani, sikusikii vizuri ni tukio gani?

Mwandishi: Ni tukio la kumuamuru mwalimu kudeki darasa ulilolifanya Oktoba 17.

Mkurugenzi: Ngoja nikutumie namba za afisa habari wa wilaya (Misungwi) atakueleza suala hilo.

Mbona kawaida sana, angewekwa lokapu sibora kudeki kuliko kulala ndani?, watanzania bana mambo mengine tunayakuza kweli, ni adhabu kama adhabu zingine jamani.
 
Mbona kawaida sana, angewekwa lokapu sibora kudeki kuliko kulala ndani?, watanzania bana mambo mengine tunayakuza kweli, ni adhabu kama adhabu zingine jamani.

You are not serious.Kama Mzazi wako ni mwalimu akifanyiwa hivyo hope utajibu ulichojibu.Bila Mwalimu asingekuwa hapo alipo.Ukiona wateuliwa wanafanya mambo ya ajabu basi ujue ni replica ya aliyewateua
 
Mbona sasa waheshimiwa mawaziri hawatoi matamko na kuchukua hatua kama walivyofanya kwa walimu wale wa field walivyokiuka taaluma zao?Yuko wapi Joyce Ndalichako,yuko wapi Simbachawene,Mwigulu pia yuko wapi?Walimu nchi hii wananyanyaswa sana.
 
Back
Top Bottom