Aliyempigisha ‘deki’ Mwalimu aigomea CWT

Aliyempigisha ‘deki’ Mwalimu aigomea CWT

Jamani binafsi naona ukimdhalilisha mtu ambaye ana element za upinzani na wanaodai haki zao huwez kushushwa cheo ila kupandishwa lakin ukigusa wale wanaolinda dola hauachwi kiufupi utawala huu niwakibaguzi sijapata kuona.
 
Hii ngumu kuitetea...mwalimu alikuwa anafundisha darasa chafu...mkurungezi kakuta mwl anafundishia darasa chafu...kwa mazoea yetu mkurungezi angemwita pembeni-.amnong'onezee mwl 'darasa ni chafu'...mwl hakuona darasa chafu?

Sina utetezi wa uchafu..sorry for that
 
Siombi mabaya lkn ipo siku wataumbuka watakutana na vichwa maji kwani kiuajiriwa serikalini ndiyo kuwa na masisha mazuri wasijaribu huu moto wamemuonea sana mwalimu lkn one day yes.
 
Hii ngumu kuitetea...mwalimu alikuwa anafundisha darasa chafu...mkurungezi kakuta mwl anafundishia darasa chafu...kwa mazoea yetu mkurungezi angemwita pembeni-.amnong'onezee mwl 'darasa ni chafu'...mwl hakuona darasa chafu?

Sina utetezi wa uchafu..sorry for that
Nasikia darasa mojawapo ndio lilikuwa chafu, mengine yalikuwa masafi na ndio yaliyokuwa yanatumika, kwahiyo huenda lile chafu lilikuwa halitumiki, kitu ambacho ni kawaida sana kwa shule zetu za pembezon, mana huko vumbi huwa halikwepeki plus shida ya maji n.k.

Mtetee Mwl, alionewa na kudhalilishwa..!!
 
Ni wakati sasa walimu muamke na kutetea haki zenu.

Ikumbukwe kwamba kazi ya ualimu nu ngumu na inahitaji uwe kio cha jamii, sasa kwa kwenda mbali zaidi nankuonyesha udhaifu kama huo nyinyo mtakua vitambaa vya kufutia hasira na chungu cha kupikia sifa za viongozi wa juuu.

Kwa hili lililotokea inaashiria matukio menginenmengi tu yatakayozidi kuwadharirisha ili hali ikijurikana kuwa ni kada inayofanya kazi chini ya changamoto kubwa.

Mmevumilia kuitenda kazi kwa mazingira magumu, kama mishahara midogo, na kusahauliwa katika kila mema.
Heshima yenu ilishushwa zaidi na viongozi na mpaka kupelekea mwalimu kudharauliwa na jamii hivi sasa, imeenda mbali zaidi sasa na wanafunzi wataanza kuwadharau kwa kasi kubwa

Ngoja tuone hili mnalotatua vipi


Siku wakakuta mtoto amevaa sale iliyo chanika mtaamlishwa na nguo zenu mzichane
 
Kosa la mwalimu hilo,we utakubali vp mtu mzima mwenzako akupigishe deki sasa? Huo nao ni umburura wa kiwango cha juu,mi sikubali na kama ni kazi basi niachishwe tu..na mtu huwezi kuachishwa kazi kwa kosa la kukataa kupiga deki
 
Usikute ametumwa na mkulu kama alivyofanya G. wa Arusha kwa Lema.
nimepata taarifa kuwa raisi kampigia simu kumpongeza, baada ya kumpigia simu kaomba aongee na mtu wa jirani ili kudhiirisha ni yeye mtukufu
 
Watumishi wa umma hata kama wana shida namna gani, hata kama ni maskini, hawastahili kuwa wanyonge kiasi hicho. Wasikubali kufanyiwa mambo ya hovyo kama huyo Mwalimu, kisa ni mkurugenzi, au kada wa CCM. Ukimtii m.pumbavu, wewe unakuwa m.pumbavu zaidi.

Wajibu wa kuilinda na kuitetea haki yako ni wa kwako mwenyewe, vyombo vingine huja baada ya wewe mwenyewe kudhihirishia kuwa haki yako inavunjwa.

Huyo Mwalimu aliyedekishwa darasa mbele ya wanafunzi alijua kuwa anadhalilishwa au aliona anastahili kufanyiwa hivyo?
 
Walimu walio wengi ni watu wa ovyo wasiokua na msimamo acha awaburuze tu
 
Mhh jamani mbona mnawanyanyasa walimu? Kilio chao nani anakisikiliza?


Pole ziwaendee walimu wote

Walimu inabidi wapate viongozi imara wa kuwatetea!Hawa waliopo sasa ni waoga sana!Mwl ni kada ambayo hata viongozi wa serikali wanawadharau sana sababu hawana umoja
 
JAMANI WAALIMU WENGINE NI WACHAFU WANASHINDWA KUSIMAMIA WANAFUNZI KUFANYA USAFI..MIMI NAMPA PONGEZI HUYO MKURUGENZI
Wewe nawe akili ni kijiko. Huyo mkurugenzi alifika shuleni hapo mida ya jioni that means darasa lilikuwa limetumika, utategemeaje darasa lililotumika kuanzia asubuhi liwe safi? Ingekuwa asubuhi labda; na hata ingekuwa ni muda gani huyo mkurugenzi hakupaswa kufanya jambo la kijuha kama hilo
 
Kishaona dalili ya kutumbuliwa huyoooo,anajifanya naye mungu mtu.Daaaahhh hua naskiaga vibaya mno kuona mwalimu akionewa au kudhalilishwa,tunajisahau sana wakati hao ndo walez na wasimamiz wa taaluma zetu
Inauma sana n kitendo cha unyanyasaji sana bila mwalimu yy angekuwa japo mi sio mwalimu ila walimu wananyanyaswa sana duh
 
Mkurugenzi wa sasa wa Misungwi ni mbovu sana na hana sifa za uongozi, kama alienda kupangua kila idara ya afya katika hospitali ya wilaya ya Misungwi na kuwapanga madaktari kila department na kuwahamisha ovyo - ovyo utafikiri na yeye ana fani ya udaktari, yaani ni shida, kwa miaka mitano ya huyu jamaa Misungwi haitoboi.
 
Back
Top Bottom