Aliyekuwa Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, agoma kukabidhi Ofisi kwa Sheikh Walid

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
Pamoja na kwamba Uteuzi wake ulitenguliwa, ameendelea kufanya kazi ndani ya Ofisi.

Katibu wa Baraza la Mashehe wa Dar es Salaam Shekh Ally Kizegero aitisha kikao kinyume cha Utaratibu

Nia ni kuwagawa Mashehe wa Dar. Kitendo kinachofanya na Elhad inadaiwa ni Uhaini

====

Aliyekua Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, ameendelea kudharau Mamlaka ya juu ya BAKWATA kwa kuendelea kufanya fujo.

Pamoja na kugoma kukabidhi ofisi kwa Mteule mpya wa nafasi yake Sheikh Walid, kiongozi huyo wa zamani ameitisha kikao cha Mashehe wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kisingizio cha kuagwa akiwa na malengo ovu.

Akijua hana mamlaka hiyo Elhad kamuagiza Katibu wa Baraza la Mashehe wa Dar es Salaam Shekh Ally Kizegero kuitisha kikao leo saa nane mchana bila ridhaa ya Sheikh wa mkoa wala Mufti Mkuu Sheikh Abubakar Zubeir

Sheikh Alhadi anaagwa, kwani amestaafu?

Katibu wa baraza la masheikh mkoa wa dsm,anaitisha kikao hicho bila kumshirikisha kaimu sheikh wa mkoa Dsm, sheikh walid, na kupokea maelekezo toka sheikh Alhadi, huu ni uhaini uliwa wazi kabisa.

Ni lazima mamlaka za juu BAKWATA Taifa, ziwashuhulikie katibu wa baraza la masheikh mkoa wa dsm na wajumbe wote wa baraza la masheikh mkoa wa dsm wanaoendelea kushiriki katika vurugu hizo,zenye picha ya uhaini.

Alhadi asimamiwe na mamlaka za juu BAKWATA Taifa, ili akabidhi ofisi ya sheikh wa mkoa,haraka iwezekanavyo na aache mara moja kutumia ofisi hiyo kwa ajili ya jumuiya yake ya marishiano(kwani Alhadi anatumia ofisi ya sheikh wa mkoa wa dar es salaam,kuendeshea taasisi nyingine mbili zisizo za Bakwata).

Tangazo la kikao hicho linasomeka.

TANGAZO NDO HILI HAPA CHINI

Assalaam alykum,

Ndugu shekh na mjumbe wa baraza la mashekh mkoa D'salaam

Nitumie fursa hii kukualika katika kikao Cha baraza mkoa D'salaam chenye agenda ya kumuaga Dr.shekh Alhad mussa salum aliyekua shekh wa mkoa D'salaam.

Siku: ni kesho j.mosi
Ukumbi ni karimjee
Muda ni saa nane mchana

Wako Shekh Ally Kizegero
........................
Katibu B/ la mashekh mkoa

=====

UPDATES

Mkutano wake umezuiliwa. na ameambiwa sio halali. Ikabidi aondoke na kwenda Korogwe kwenye msiba wa familia ya Mufti
 
Pamoja na kwamba Uteuzi wake ulitenguliwa, ameendelea kufanya kazi ndani ya Ofisi.

Katibu wa Baraza la Mashehe wa Dar es Salaam Shekh Ally Kizegero aitisha kikao kinyume cha Utaratibu

Nia ni kuwagawa Mashehe wa Dar. Kitendo kinachofanya na Elhad inadaiwa ni Uhaini

====

Aliyekua Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, ameendelea kudharau Mamlaka ya juu ya BAKWATA kwa kuendelea kufanya fujo.

Pamoja na kugoma kukabidhi ofisi kwa Mteule mpya wa nafasi yake Sheikh Walid, kiongozi huyo wa zamani ameitisha kikao cha Mashehe wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kisingizio cha kuagwa akiwa na malengo ovu.

Akijua hana mamlaka hiyo Elhad kamuagiza Katibu wa Baraza la Mashehe wa Dar es Salaam Shekh Ally Kizegero kuitisha kikao leo saa nane mchana bila ridhaa ya Sheikh wa mkoa wala Mufti Mkuu Sheikh Abubakar Zubeir

Sheikh Alhadi anaagwa, kwani amestaafu?

Katibu wa baraza la masheikh mkoa wa dsm,anaitisha kikao hicho bila kumshirikisha kaimu sheikh wa mkoa Dsm, sheikh walid, na kupokea maelekezo toka sheikh Alhadi, huu ni uhaini uliwa wazi kabisa.

Ni lazima mamlaka za juu BAKWATA Taifa, ziwashuhulikie katibu wa baraza la masheikh mkoa wa dsm na wajumbe wote wa baraza la masheikh mkoa wa dsm wanaoendelea kushiriki katika vurugu hizo,zenye picha ya uhaini.

Alhadi asimamiwe na mamlaka za juu BAKWATA Taifa, ili akabidhi ofisi ya sheikh wa mkoa,haraka iwezekanavyo na aache mara moja kutumia ofisi hiyo kwa ajili ya jumuiya yake ya marishiano(kwani Alhadi anatumia ofisi ya sheikh wa mkoa wa dar es salaam,kuendeshea taasisi nyingine mbili zisizo za Bakwata).

Tangazo la kikao hicho linasomeka.

TANGAZO NDO HILI HAPA CHINI

Assalaam alykum,

Ndugu shekh na mjumbe wa baraza la mashekh mkoa D'salaam

Nitumie fursa hii kukualika katika kikao Cha baraza mkoa D'salaam chenye agenda ya kumuaga Dr.shekh Alhad mussa salum aliyekua shekh wa mkoa D'salaam.

Siku: ni kesho j.mosi
Ukumbi ni karimjee
Muda ni saa nane mchana

Wako Shekh Ally Kizegero
........................
Katibu B/ la mashekh mkoa
Acheni wivu kwa kuagwa nongwa Acheni uhuni, subiria aagwe kisha jumatatu mpewe ofisi yenu.
 
Back
Top Bottom