sagaciR
JF-Expert Member
- Jun 17, 2017
- 644
- 875
Neno WAKILI (noun) linatokana pia na neno MWAKILISHI (Adjective). Kisheria inamanisha mwakilishi wa mdawa (mdai, mdaiwa, mshtakiwa).
Mdawa anaweza kuwakilishwa Mahakamani kwa njia kadhaa ikiwemo:-
1. Ndugu (Relative)
2. Mwenye barua ya kisheria (power of attorney) na
3. Mtaalamu wa sheria aliyefuzu mafunzo ya uwakilishi mahakamani (Learned council)
Mwakilishi aliyetajwa katika kipengele cha 1 na 2 hapa, ni mwakilishi ASIYESOMEA uwakikishi Mahakamani. Bali mwakilishi aliyetajwa kwny kipengele cha 3 hapa juu ni mwakilishi ALIYESOMEA uwakilishi Mahakamani.
HIVYO BASI MWAKILISHI ALIYESOMEA KAZI HIYO ANAIYWA MWAKILISHI MSOMI (Wakili) BALI MWAKILISHI ASIYESOMEA KAZI HIYO SIO MWAKILISHI MSOMI.
Kwa kujibu swali lako wakili asiye msomi ni yule asiye na taaluma ya sheria ya uwakilishi mahakamani (to be precise a LEGAL LAYMAN like you).
NB:
Uwakikishi ninao uongelea hapa ni uwakilishi MAHAKAMANI PEKEE na sio pengine kama harusi, kikao, majadiliano n.k
Sent using Jamii Forums mobile app