Husninyo
Platinum Member
- Oct 24, 2010
- 24,167
- 10,226
Pendo amekosa tu kujitambua na kujiamini. Ukiwa kama mshauri wake msaidie ajitambue kuwa Clement hamfai, hastahili kuwa naye na sie wa hadhi yake kimaadili na hata kimapenzi. Kitendo cha Clement kumshauri tu kuitoa ile mimba ilikuwa ni dalili tosha kuwa Clement hakuwa amedhamiria kuishi naye kama mpenzi wake. Mwanaume mwenye mapenzi ya kweli na nia angemwambia imeshatokea, twende kwa wazazi tukaji'shtaki', tuombe msamaha tupewe Baraka ya kuwa mwili mmoja tulee mwanetu. Lakini kwa kuwa Clement hakuwa amempenda kwa dhati ndio maana alimwambia akaitoe. Pili mwambie Pendo kuwa yeye ana bahati kuwa MUNGU amemwonyesha mapema kuwa Clement siye, ingekuwa vipi kama angeolewa naye kasha Clement akamletea mwanamke mwingine ndani na kuanza kuishi naye? Au angemtesa kimapenzi? Mwisho mwambie Pendo aamke Clement siyo wake, wake yupo na anavyozidi kumfuata Clement ndivyo Clement anavyozidi kumdharau na anaweza hata kumtake for his advantage ili tu ajifurahishe. Na pia kwa kumfuata fuata Clement na kulilia asipopendwa hajitendei haki yeye na nafsi yake. Mdedicatie wimbo wa Serebuka wa Mwasiti
dada mkubwa huu ushauri murua kabisa. pendo amtoe clement akilini. yaliyopita yamepita na agange yajayo.