R-K-O
JF-Expert Member
- Jun 27, 2023
- 482
- 2,138
Ni binti naemjua kabisa alikuwa house girl akiwa na umri wa miaka 16 alitolewa huko Iringa aje kusaidia kazi, baada ya miaka sita familia ikaamua wampeleke sehemu ajifunze kushona, alipomaliza akarudi kwao kijijini wakampa cherehani na milioni 1 na nusu ya shukrani.
Binti hakukaa sana huko kwao akarudi mjini, alikuwa anasaidia kupika mgahawa flani wa mtaani kwa miezi miwili hivi ila ni mbali na sehemu aliyoishi akiwa house girl, watu wa mtaa moja tulioishi nae walidhani labda alifukuzwa wengine tuliomjua kasomeshwa cherehani, kapewa chereani na kapewa milioni na nusu tulihisi labda katapeliwa kila kitu na ndugu zake.
Muda si mrefu nae akafungua sehemu kwenye frem za kawaida hizi, sio uswazi sana anapika chakula cha mchana na jioni. wali, maharage, pilau na nyama.
Navyoongea sasa hivi ile sehemu ya mwanzo wapo mabinti wawili kawaacha hapo, yeye alishafungua sehemu nyingine na wateja wapo.
Ilinishawishi nimfatilie zaidi, hajanipa mchoro mzima ila aliniambia ile miezi miwili alikuwa anapitia training na kuijua biashara, ndipo nilipoelewa kwamba hakutapeliwa kama nilivyodhani mwanzo.
Kwa haraka haraka kwenye mgahawa moja anaweza kupata elf 30 faida, kwa migahawa miwili kwa mwezi ?
Nachohofia tu pengine akipata mario ampe mimba inaweza kumtikisa
Kwa upande mwengine nikianza kutafakari hawa wadogo zetu wengine ambao wamemaliza vyuo wapo ajira zenye mishahara ya laki na nusu hadi 5 tena ni private nafadhaika sana, wengi huona aibu kufanya baadhi ya shughuli kama kupika mitaani.
Binti hakukaa sana huko kwao akarudi mjini, alikuwa anasaidia kupika mgahawa flani wa mtaani kwa miezi miwili hivi ila ni mbali na sehemu aliyoishi akiwa house girl, watu wa mtaa moja tulioishi nae walidhani labda alifukuzwa wengine tuliomjua kasomeshwa cherehani, kapewa chereani na kapewa milioni na nusu tulihisi labda katapeliwa kila kitu na ndugu zake.
Muda si mrefu nae akafungua sehemu kwenye frem za kawaida hizi, sio uswazi sana anapika chakula cha mchana na jioni. wali, maharage, pilau na nyama.
Navyoongea sasa hivi ile sehemu ya mwanzo wapo mabinti wawili kawaacha hapo, yeye alishafungua sehemu nyingine na wateja wapo.
Ilinishawishi nimfatilie zaidi, hajanipa mchoro mzima ila aliniambia ile miezi miwili alikuwa anapitia training na kuijua biashara, ndipo nilipoelewa kwamba hakutapeliwa kama nilivyodhani mwanzo.
Kwa haraka haraka kwenye mgahawa moja anaweza kupata elf 30 faida, kwa migahawa miwili kwa mwezi ?
Nachohofia tu pengine akipata mario ampe mimba inaweza kumtikisa
Kwa upande mwengine nikianza kutafakari hawa wadogo zetu wengine ambao wamemaliza vyuo wapo ajira zenye mishahara ya laki na nusu hadi 5 tena ni private nafadhaika sana, wengi huona aibu kufanya baadhi ya shughuli kama kupika mitaani.