Alidai nimeoa bibi kizee, sasa anaomba msaada

Sasa akamuombe mkewe kijana anakuja kuombaje mzee?
Kwanza uache kujiita Sheikh!
Ukweli ni kwamba umeoa ajuza na nduguyo ana kupenda ndio maana alisema!

Msaidie au usimsaidie atabaki ndugu yako na dunia na jamii itajua tuu.. hivi unajisikiaje ndugu yako kuteseka ikiwa una uwezo wa kumsaidia?
 
msamehe tuu huyo ni ndugu yako,usipomsamehe utakuwa huna tofauti naye,kumsamehe nayo ni adhabu,em imagine baada ya kumsaidia atakuangaliaje,atapata aibu iliyoje halafu wewe ndo unazuga huna hata moja.hapo lazima heshima irudi na umbea ataacha,lakini usisahau kuwa huyo ni ndugu yako no matter what,kukuletea zengwe hakumfanyi kuwa sio ndugu yako.
 
Msaidie ndugu yako samehe yaliyopita piga moyo konde iyo damu yako anaweza kukusaidia mbeleni
 
Mkuu najua dogo wako alikuudhi sana..ila kiuhalisia hatakama ni mimi ningepinga wewe kumwoa huyo mama mwenye miaka 55.. Sio tamaduni zetu kumwoa mwanamke anaelingana na mama zetu...kwa hiyo mm nafikiri dogo alikua na nia nzuri tu ila ilipingana na mtazamo wako..
Mimi nafikiri msaidie tu..undugu hauishi..bado ni ndugu yako tu..wewe msaidie tu..
Kumbuka....usimtukane mamba kabla ya kuvuka mto.
 
Sijui kama nimeeleweka vizuri, naomba niweke hivi

Mm sikwenda kumuomba ushauri wakati nataka kuoa, sababu kuoa ni uamuzi wangu binafsi, hata yeye hakuja kuniomba ushauri wakati anaoa

Hivyo alichokifanya yeye ni majungu, alitembea kila kaya katika ukoo akipika majungu na kunisema vibaya, tena kwa matangazo makubwa, ni ukosefu mkubwa wa adabu kwa kaka yako
Sasa leo kinachomleta leo kuomba msaada kwa huyu huyu mwanamke mzee ni kipi? Je morally inakubalika? Mtu uliedai mzee hafai leo akusaidie inakuja?
Mbona hoja hii mnaikwepa kila nikiisema hamjibu?

Ni sawa na kumuita ndugu yako jambazi na unamtangaza kote kuwa mali zake amepata kwa ujambazi, halaf kesho unapata tatizo unaenda kwa huyo jambazi kuomba msaada, Je upewe huo msaada kweli?

Nijibuni
 
1. acha kubeba vitu kwa mda moyoni mwako ni kujitafutia magonjwa
2. usiwe mtu wa kulipiza kisasi maana ni kweli hata wewe umekiri kuwa mwanamke ni mtu mzima kwa umri huo uliotaja, ila we unakosea sana maana aliyedhalilishwa zaidi ai wewe bali ni huyo mwanamke ila ye yuko tayari kumsaidia iweje wewe ushindwe kutoa ruhusa hiyo.
3. iwapo utabana, huyo mdogo wako atakuwa kila siku anakuja kukulilia msaada na atakulaumu sana kuwa braza we sababu ya haya matatizo yote kipindi hiko yuko matatizoni, hivyo kwa kuwa nafasi ipo msaidie sahau ya nyuma na hapo ndo atarejesha heshoma yako na kwa shemeji yake na atasafisha majina yenu kwa watu.
4. muulize dogo atarudisha vipi hizo hela baada ya kusaidiwa maana usipokuwa makini hela hiyo itakuwa chanzo cha ugomvi kati yako na mkeo pindi atakapokuwa na haja nazo, pia watoto wa huyo mama watapata cha kuongea kuwa we ulimwoa mama yao kwa ajili ya pesa zao na hapo ndo utakuwa chanzo cha kukosa amani
 
Kumbe dogo alisema ukweli ambao huutaki kusikia sasa unajenga bifu, acha ujinga hakuna aijuae kesho so msaidie usijione maisha umeyapatia na usivunje kioo kwa kukuonesha tongotongo usoni mwako
 
Ohh my... Pole. Nimeishia hapo nliposoma miaka.
 
Waswahili walisema ngurue aramu ila ukiamua kumla kula alio nona" ndo alicho fanya kaka angu japo Mzee alitafuta mwenye Pesa we wazani angekuwa Mzee alafu anapesa ingekuwaje?
 
Kumbe dogo alisema ukweli ambao huutaki kusikia sasa unajenga bifu, acha ujinga hakuna aijuae kesho so msaidie usijione maisha umeyapatia na usivunje kioo kwa kukuonesha tongotongo usoni mwako
Yeye ndie alietukana mamba kabla hajavuka mtoto, hivyo huo msemo wa kioo unamfaa yy zaidi

Maisha hayana formula, hapa mjini kila mtu akikwambia jinsi alivyo Pata pesa au jinsi alivyofanikiwa kimaisha unaweza kuzirai, wapo majambazi, madawa ya kulevya, wengine walidhalilika ili kufanikiwa, hivyo mm nina akili zangu timamu kuamua kuoa mama mtu mzima wa 55 lengo ni kuweka maisha sawa Ndo maana hata yy dogo hakwenda kuomba pesa kwa ndugu wengine kaja kwangu, nisingemuoa huyu mwanamke na maisha yangu yakawa kama zamani angekwenda kuomba wapi hiyo 15 million, maana zamani wote familia nzima tulikua juu ya mawe sasa angemuomba nani kama nisingeoa huyu mwanamke?

Wakubwa zako wanapofanya vitu flan wanafanya kiutu uzima na wanajua wanachokifanya usiwabeze,
Yeye na wote walionibeza wakati naoa huyu mwanamke ndio hao sasa hawakauki kwangu kuomba misaada, sasa huo tuiteje kama sio unafiki?

Mbona yeye dogo amemshika ugoni mkewe mara mbili na hajamwacha lakini mbona mm kaka yake nipo kimya sijawahi hata siku moja kumwambia amwache mkewe, you know why? Ni maamuzi yake it's non of my business
Sasa Kuna jambo kubwa kwenye maisha kama mkeo kulala na mtu. Mwingine? Lakini mm kwa kifua changu cha kiutu uzima nilikaa kimya na kumwachia amalize mwenyewe

Acha ajifunze maisha through the hard way
 
Kumbe ulimuowa uyu mama sababu ulikuwa juu ya mawe[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] kumbe kweli umefata Pesa sio mapenzi asante kwa kuwa mkweli
 
Na unajua wewe kitandani uko weak mdogo wako anapiga had pushups on bed acha amsaidie coz baadae watasaidiana!
 
Swali la kizushi mfano ww ndo ungekuwa tajiri unaela alafu uyo mama Hana ela je ungekuwa????
Au ungekuwa na kina wema sepetunga
 
Kumbe ulimuowa uyu mama sababu ulikuwa juu ya mawe[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] kumbe kweli umefata Pesa sio mapenzi asante kwa kuwa mkweli
Ulitaka niwatangazie watu kwamba nimefuata pesa?

Ulitaka niwatangazie ndugu kuwa jamani nimeoa huyu mama kufuata pesa?

Off course alinipenda mwenyewe na kuomba nimsitiri yaani nimwoe, Ingawa kiukweli ni mzuri, huo umri mnauona ni umri mkubwa lakini ukimwona ni kama yupo some where 35 hivi, kwa hiyo sio tu pesa pekee, mvuto pia anao
Infact naridhika kimapenzi kuliko nilivyokua natoka na wanawake wa rika langu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…