Kwanza ni fact kuwa ulioa mtu anayekuzidi umri mno hivyo dogo alikuwa sahihi sana.Pia inaonekana mdogo wako ni muangaikaji kukuzidi,wewe unalelewa hiyo kusema sijui pesa yako iko katika mzunguko ni zuga tu lakini dogo kajenga nyumba ni bahati mbaya tu uwanja kumbe ulikuwa unamnunuzi mwingine pia.Maisha ni safari husipomruhusu huyo mmama amsaidie bila shaka Mungu atamuinua mtu mwingine amsaidie au hata nyumba ikibomolewa Mungu atamuwezesha tena pengine zaidi ya mahali alipo sasa.Kumbuka huyo ndiye ndugu yako ni gurantee kuwa ukitangulia mbele za haki na mkeo ni yeye atawaangalia wanenu (kama umebahatika kuzaa na huyo mmama).
Hoja yako haina mashiko, Bahati nzuri nimefafanua wakati najibu Hoja za wachangiaji mbali mbali ikiwemo comment iliyopita kabla hii ya kwako, labda kama majibu hayajakuridhisha, ila nina Hoja za msingi sana
Narudia tena, nisingeoa huyu mwanamke mzee yeye angepata nguvu za kuja kuomba hiyo 15 million? Jibu ni hapana, kabla ya kumuoa huyu maisha yangu anayajua kuwa Sina hizo pesa, hivyo kaja kuomba akijua wazi huyu mke wangu anazo hizo pesa, sasa unapataje nguvu kuomba pesa kwa mtu uliedai mzee na ulidai asiolewe?
Kama huyu mdogo wangu ni mchakarikaji ameshindwaje kupata kwingine hii pesa hadi kujidhalilisha hadi kuja kumuomba mtu aliemsema vibaya hapo mwanzo?
Mkewe wa ndoa alizini na mwanaume mwingine mwaka 2013 yeye akiwa safari ndani ya kitanda cha ndoa, pamoja na watu ikiwemo wazazi wetu kupiga kelele kuwa ampe talaka huyo mwanamke lakini mdogo wangu hakumpa mkewe talaka, na anae hadi leo, katika mgogoro huo wote nilikaa kimya, sikujihusisha nao kabisa, maana naheshimu uamuzi wake, wala sikuzunguka kumtangaza, Je Kuna kitu kikubwa kwenye maisha kama mkeo kukusaliti?
Sasa mbona mm niliheshimu mawazo na uamuzi wake? Nilijua Kuna maisha baada ya suala hilo
Hivyo na yeye alipaswa kuelewa Kuna maisha mengine mbali na suala langu la kuoa huyu mke wangu aliedai mzee, maisha hayaishii kwenye suala hilo
Ni wazi huyu dogo hana ukomavu kwenye maisha
Alichokifanya ni kutembea kote akipika majungu na kunidhalilisha kila kona, Leo anakuja kuomba msaada hapo hapo alipotukana, haiwezekani
Badala ya kufanya alivyofanya, ni heri angekuja kwangu straight away na kunitazama usoni na kuniambia mm mwenyewe kwamba kaka uamuzi wako sio sahihi ningemwelewa, lakini hakufanya hivyo, badala yake alienda kupika majungu
By the way unafahamu ni kwa nn katika miezi sita yote aliyopewa na mahakama kulipa hizo pesa hakuja kwangu hadi zimebaki wiki mbili? Ni kwa sababu aliona aibu kuja kwangu kwa kitendo alichokifanya, sasa amekuja as a last resort hana jinsi afanyeje? Aliowatuma wote walikataa ndipo akaja mwenyewe
Hoja yako kuhusu mm kupenda mtelemko, majibu yangu kwako ni, hapa mjini huwa hatuulizi watu jinsi walivyo Pata pesa, Bila shaka unawaona tu watu wakitoka kwenye mageti ya kifahari, magari ya kifahari, maisha ya kifahari, huwa hatuwaulizi wamepataje, elewa tu kwamba the end justifies the means