Alichosema Ismail Jussa

Alichosema Ismail Jussa

Well said Jussa, ukweli utabaki milele lakini chadema watajua kwamba hilo dude ni bovu baada ya uchaguzi...yaani ...nimecheka comment ya aina mkumbo ndio aina viongozi wa chadema tunaotegemea kuwapa nchi..waziri mkumbo ndio anaongea hivyo what a joke!

Chadema bado sana!
 
Rev. Kishoka,

Kwanza kama ingekuwa mimi ningemjibu mkulu kwa kuhitaji mifano na takwimu zinazodhihirisha aloyasema yote.
Kwa mfano swali la kwanza:-
1. Prof. Lipumba is more competent and more exposed in both local and international affairs and leadership than Slaa whose experience is merely of a whistleblower.

Jibu:- Sio kweli kabisa, tumemwona Obama mwenye experience ndogo akiwa joined na kina J. Biden, Clinton na the whole bunch of experienced fellas ambao wamempa tafu. Anachoshindwa kuelewa huyu jamaa yetu ni kwamba kiongozi anayetakiwa ni yule mwenye Uzalendo, vision na Mbunifu wa kile anachokitaka ku accomplish at the end ili kuondokana na matatizo/mahitaji tulokuwa nayo - now, how to achieve all this, ndipo anachagua watu wa kuwa naye na sisi tunasemea Lipumba is one of them...
Pili Lipumba ni mchumi sii mbunifu wala hana vision....huyu ni sawa na mpangaji wagharama za matumizi na mapato. Mara zote wachumi sii wabunifu ila wazuri kwa kukadiria matumizi na mapato pia njia bora za kuwezesha hivyo - Ni Lipumba anayemhitaji Dr. Slaa.

2. CUF ni chama cha kitaifa wakati Chadema iko Tanganyika tu;

Jibu:- Je CUF imeshinda majimbo mangapi bara?
Kwani tunapozungumzia chama cha kitaifa, kinachohesabika ni uwakilishi wake sio kuhesabu wingi wa vibanda vyake mikoani.

3. Kwa performance ya kisayansi na si ya kukusanya watu kwa helikopta, CUF ina nguvu zaidi Bara na Zanzibar, kigezo ni kila uchaguzi CUF imekuwa mara zote inashika nafasi ya chama cha pili na hivyo kukipa sifa ya kuwa chama mbadala - angalia matokeo hata ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji ambapo pamoja na magazeti kuibeba sana Chadema, bado CUF imeshika nafasi ya pili (kumbuka huu uchaguzi ulikuwa Bara peke yake)

Jibu:- Uchaguzi wa Kitaifa kulikuwa namajimbo 181 bara na Chadema ilipata ushindi wa viti 5 hali CUF hawakupata kitu. Zanzibar CUF walipata viti 22 kati ya viti 50. Kwa hiyo ushindi wa pili wa CUF unatokana na viti 22 vya visiwani na sio Bara. CUF haina nguvu bara sawa na Chadema isivyokuwa na nguvu visiwani.
pili, Uchaguzi wa sewrikali ya mitaa Chadema hawakushiriki na kusema kweli yalikuwa makosa makubwa. Hawakufanya hivyo kutokana na kuvunjika kwa umoja mlokuwa mmeanzisha hivyo wakaweka mawazo yao sehemu nyingine.

Swali la 4. jibu:- kuhusiana na CUF kujijenga zaidi ya Chadema. jamani lets not kid ourselves.. CUF imejijenga vipi?.. CUF na Chadema kitaasisi ni vyama ambavyo havina uwezo kabisa yaani wote wanabangaiza tu. Hili sii swala la kuhitaji mjadala kwani CUF na Chadema bado kabisa wamebanwa vibaya na CCM kiasi kwamba kujitangaza kwao kunategemea imani ya wanachama wake. Wote waliohama CUF wamepitia mitihani kama ya Chadema na vyama vingine vyote vidogo. Kumbuka kuhama kwa Lwakatale CUF ilitokea kipi.. fact is Hakuna aliye na afadhali.

5. Chadema kimeshindwa kujivua gamba la ukabila na udini na sasa ndiyo kinazidi kutopea huko wakati CUF imetanda kila pembe ya Tanzania;

Jibu:- Duh mkuu wangu, marafiki zangu wakubwa ni member waCUF damu, na kijiwe changu kikubwa ni pale K tea shop mjini Chagga st... ninawajua CUF kuliko unavyofikiria. Chadema kama ni Wadini au Wakabila, ni CUF pekee ndiyo ingeweza kuwaondoa ktk fikra hizo kama zipo kweli na mngewa join, lakini sio kuzungumzia nje hali CUF yenyewe inaonekana kusongwa na matatizo hayo hayo. Ushahidi wangu:- Why CUF imejikita kwa maswala ya Zanzibar zaidi ya bara?.

6. CUF kina mtandao wa chama wenye muundo uliokamilika wa uongozi uliojipanga kitaasisi wakati Chadema hakina muundo na huishia kuokota wajumbe wa vikao mitaani kupata uhalali wa vikao.

Jibu:- Chadema sii wajuzi wa kila kitu, vitu kama hivi ndivyo CUF could have bring in kama mchango wao. haiwezekani Chadema kuhitaji kuungana na chama ambacho hakina ubora wowote.

7. CUF kimeonyesha umakini mkubwa katika uongozi na hata katika Kambi ya Upinzani Bungeni kimeonyesha ukomavu tofauti na Chadema ambao hata wale wabunge wake 11 tu wanashindwa kuelewana..

Jibu:- Bungeni sio mahala pa kuonyesha unyenyekevu. Ni sehemu ya kuvuana nguo na sio kubebana kama CCM wanavyofanya ili mradi kulindana. Bungeni wajumbe wanakuja kuwakilisha wananchi na sio kuwakilisha chama. Kutoelewana ndio inaonyesha ukomavu wa watu kuona tofauti au matatizo ya bajeti inaposoimwa na sio kukubali kila unachoambiwa.

8. CUF kina misingi ya kidemokrasia na ndiyo maana hata Prof. Safari aliachiwa kushindana kwa uwazi na Prof. Lipumba kwenye nafasi ya Uenyekiti wakati Chadema kina uongozi wa kiimla wa muasisi wa Chama mwenye uwezo wa kumuengua mgombea Uenyekiti ili mkwewe apite bila ya kupingwa:

Jibu:- Kugombea kiti cha Uenmyekiti sio swala la demokrasia. hakuna kifungu chochote cha demokrasia kinacholazimisha au kushauri vyama kupitisha uchaguzi inapofikia swlaa la Mwenyekiti.. Na pengine huelewi kwamba Chadema mwenyekiti ni Mbowe na anayegombea Urais ni Dr.Slaa wakati CUF mwenyekiti ndiye mgombea kiti cha urais!

Yaani Rev. mkuu wangu huyu jamaa majibu tyake ni rahisi sana naweza kuyajibu pasipo hata kufikiria..Ila sidhani kama yeye yupo tayari kupokea maswali kutoka upande huu!.

Ni vizuri tukaweka sawa rekodi hapa. Uchaguzi wa serikali za mitaa uliopita (mwaka jana tu ) Chadema ilishirika kikamilifu swa na CUF. Matokeo (Bara) CUF wameshika nafasi ya pili. Hapa Dar Es Salaam Chadema imeambulia viti vya mitaa 4 (vinne ) tu wakati CUF wamelamba zaidi ya viti 60 (sitini)

Kusema Lipumba kapata kura nyingi zanzibar ndio maana kawa wa pili sio sahihi pia. Uchaguzi wa mwaka 2005 Lipumba kapata kura 1.3m kati ya hizo za zanzibar hazifika hata laki 2 kwani waliopiga kura zanzibar ni watu 460,000 tu assuming more than half walimpa Kikwete then Lipumba abaki chini ya laki 2

Nilitaka kuweka sawa hilo tu......
 
dah, yaani slaaa amuunge mkono lipumba?

mnaleta mzaha?!!

sla yuko juu ya huyu lipumba , na hili ndilo tatizo la cuf, wanategema mtu mmoja kama ulimi
 
Jusa anaweza kusema yote lakini it's a known fact that the mainland has never been their priority. Wanaona kuwa hawapotezi kitu huku bara, ndiyo sababu pamoja na kuwa zaidi ya nusu ya kura za urais alizopata Lipumba 2005 zilipatikana bara, kiasi cha ruzuku wanachopewa bara ni kichekesho ukilinganisha na kile kinachobaki visiwani.
Hofu yao kubwa ni kuwa chama kikipata nguvu bara kuna hatari ya wapemba kukosa sauti ndani ya chama hicho na msimamo wa Prof Safari katika hilo ndio uliomkosesha uenyekiti na si kama Jusa anavyotaka tuamini. Jusa ni kiongozi wa ngazi ya juu CUF, anayoandika wengine tunayachukulia kama msimamo rasmi wa chama chake, hivyo CHADEMA wasipuuzie mashambulizi haya. Ni vema kupitia wanachama wao wanaoifahamu vizuri CUF kama Lwakatare wakatueleza ni kwa nini tupuuze madai kama haya kwa kueleza ukweli ulivyo ndani ya chama hicho.

Si siri tena kuwa kwa sasa kuna mkakati baina ya CCM na vyama hivi vingine kuhakikisha kuwa CHADEMA haifanikiwi. Rejea kauli ya Mrema na waraka wa Vatican kuhusu Dr Slaa!
 
Hii makala imenikumbusha wale wote ambao huwa na tabia ya kudharau watoto. Eti hana ozoefu, kichekesho na maneno yaliyopitwa na wakati.

Kuna jamaa alishasema kuwa alipokuja Wayne Rooney, kijana mdogo kabisa na wala hakuhitaji afundishwe miaka kibao kufunga magoli. Au una kipaji cha kufunga au huna. Lipumba miaka yote hiyo, zaidi ya kugombea Urais, kafanya nini?

Kikwete alikuwa na uzoefu sana mambo ya nje na hasa kuomba misaada, kazi ambayo kaendelea kuifanya hata baada ya kuwa Rais.

Dr. Slaa ni mtu makini na mtu anayetaka mambo/nchi yaende kwa kuongozwa na siyo kuweka Autopilot.

Tunahitaji mtu atakayetimiza na kuturudisha kwenye maneno ya wimbo wa Babyface:

YouTube - Babyface - Simple Days

Bring back those simple times of yesterday
When a man was a man
And a friend was a friend
Bring back those simple times of yesterday
When you said what you meant
And you meant what you said ................


 
Jusa anaweza asiwe sahihi sana, lakini na wengi wanaomshambulia nao wanakwenda siko na ni kwa kigezo hicho CCM itaendelea kupeta.

Kama kungekuwa hakuna kudharauliana na kuna strategy ya upinzani ya pamoja, suala la Urais wangekubaliana kuliacha kwanza, kila chama kiende kivyake, wajikita zaidi na Ubunge na kila chama kusimika wabunge maeneo yenye ushawishi mkubwa. Jiji kama Dsm wapinzani wanaweza kupata viti alau vinne. CUF watumie nguvu nyingi Temeke na Kigamboni na Chadema Ubungo na Kawe/Segerea. CCM haiwezi kukubali Ikulu (Ilala) iende upinzani piga ua.

Lakini ni kwa dharau kama hizi ndio NCCR na Chadema mwaka 1995 walikataa kushirikiana na CUF kutengeneza kambi ya upinzani bungeni kwa madai kuwa NCCR ndio walistahili kutengeneza kambi ya upinzani kwa kuwa na wabunge 17 wa Bara. Kambi ikaundwa na CUF na UDP. Tazama kilichofuatia 2000 na 2005 kwa wabunge wa vyama hivyo na still Chadema (ya sasa) wanakiona CUF kama chama dhaifu.

Kwangu mimi neither Lipumba nor Slaa ninaamini atatoa upinzani mkali kwa JK. Pengine tujikumbushe upinzania alioutoa Mrema na wapi alipoishia.

Mazingira na wananchi wa Tanzania hawaonyeshi kwamba upinzani strong utatoka CUF pekee au Chadema pekee bali coordinated strategy/efforts. Mkakati wa kwanzani uwe Ubunge. Chadema iwekeze vya kutosha (kwa pesa, zana na nguvu kazi) kanda ya kaskazini na Nyanda za Juu Kusini. CUF iwekeze ukanda wa pwani na Zanzibar. Kanda ya ziwa na Dsm waachiane majimbo. Magharibi: Tabora iwe CUF, Kigoma iwe Chadema; Kanda ya Kati pia waachiane majimbo. Sio lazima kuachiana kuwe sawa kwa sawa bali kulingana na nguvu ya chama mahala hapo.

Mkakati wa pili ni Urais: Baada ya kujenga nguvu bungeni, wapinzani wanatafuta mtu anayekubalika kwa wananchi na pande zote kisha hao viongozi wawe nyuma yake. Asimame chini ya chama gani itategemea na chama kinachokubalika zaidi wakati huo.

Haya yatawezekana endapo kuna nia njema kwa wahusika.
 
Huyu jamaa ni naona ameandika kiushabiki zaidi, kijuu juu naona amesukumwa na mapenzi yake aliyonayo kwa chama cha Chake (CUF), pamoja na dini yake. Inaelekea jamaa ni mbaguzi wa kutupwa. CHADEMA hawana uhusiano na LIKUD hata kidogo,Na nivema akatambua kwamba hata wao CUF wanahaki ya kutafuta vyama RAFIKI popote duniani, Mkiona HAMAS au HEZIBOLAH kinaendana na sera zenu ni vema mkaungana nao na sio kuendeleza siasa za kizushi hapa.

Kama CUF imetapakaa na kukubalika Tanganyika kama alivyohisi ungetuambia mna wabunge wangapia Huku Tanganyika? Kama nyie sio wadini Mlimfanya nini Rwakatare?. naamini hata uchaguzi wa mwaka huu hamtapata kiti hata kimoja TANGANYIKA.


Kuna demokrasia gani ndani ya CUF, Si juzi hapa Prof safari alikuwa analalama amechezewa mchezo mchafu? Si busara hata kidogo kusingizia chadema ni chama cha kifamilia hata CCM mara nyingi wana wahusiha wazee ktk kusuluhisha mamabo yao, Mtei wanahusishwa pammoja na wazee wengine kama wakina Makani mbona huwataji?

Amejisahau kwamba CUF ni maarufu ZNZ kutokana na U unguja na Upemba? wenye macho tunasubiri siku atakapo Ngatuka Seif na ndo mwisho wa CAF, Muda ndo utatuambia kama hata haka kajamaa JUSSA katapata huo Ubunge, ni vema ukajifunza alipokufa kisiasa Mrema leo hii wako wapi wakina MBATIA; LAMWAI wa miaka ya 1995?

Walichokifanya wabunge wa CHADEMA kwenye hili bunge lililopita nadhani historia ya taifa letu itawatambua na kuwaenzi,
Hujajibu hoja mkuu. Ungefanya jambo la busara sana kama ungejibu hoja kwa vigezo vinavyofanana na jinsi jamaa alivyoandika na si majungu. Mfano, jamaa kasema uchguzi wa serikali za mitaa CUF ndo ilikuwa ya pili bara baada ya CCM, sasa na wewe labda sema CHADEMA ilikuwa hivi na vile...... CUF ni chama cha kileberali na chadema hawaeleweki na wewe sema chadema ni mlengo fulani, si masuala ya kuleta porojo humu mara kajiunge na hizbula, mara nini. Yo wrote non sense man, I'm sorry
 
Rev. Kishoka,

Kwanza kama ingekuwa mimi ningemjibu mkulu kwa kuhitaji mifano na takwimu zinazodhihirisha aloyasema yote.
Kwa mfano swali la kwanza:-
1. Prof. Lipumba is more competent and more exposed in both local and international affairs and leadership than Slaa whose experience is merely of a whistleblower.

Jibu:- Sio kweli kabisa, tumemwona Obama mwenye experience ndogo akiwa joined na kina J. Biden, Clinton na the whole bunch of experienced fellas ambao wamempa tafu. Anachoshindwa kuelewa huyu jamaa yetu ni kwamba kiongozi anayetakiwa ni yule mwenye Uzalendo, vision na Mbunifu wa kile anachokitaka ku accomplish at the end ili kuondokana na matatizo/mahitaji tulokuwa nayo - now, how to achieve all this, ndipo anachagua watu wa kuwa naye na sisi tunasemea Lipumba is one of them...
Pili Lipumba ni mchumi sii mbunifu wala hana vision....huyu ni sawa na mpangaji wagharama za matumizi na mapato. Mara zote wachumi sii wabunifu ila wazuri kwa kukadiria matumizi na mapato pia njia bora za kuwezesha hivyo - Ni Lipumba anayemhitaji Dr. Slaa.

2. CUF ni chama cha kitaifa wakati Chadema iko Tanganyika tu;

Jibu:- Je CUF imeshinda majimbo mangapi bara?
Kwani tunapozungumzia chama cha kitaifa, kinachohesabika ni uwakilishi wake sio kuhesabu wingi wa vibanda vyake mikoani.

3. Kwa performance ya kisayansi na si ya kukusanya watu kwa helikopta, CUF ina nguvu zaidi Bara na Zanzibar, kigezo ni kila uchaguzi CUF imekuwa mara zote inashika nafasi ya chama cha pili na hivyo kukipa sifa ya kuwa chama mbadala - angalia matokeo hata ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji ambapo pamoja na magazeti kuibeba sana Chadema, bado CUF imeshika nafasi ya pili (kumbuka huu uchaguzi ulikuwa Bara peke yake)

Jibu:- Uchaguzi wa Kitaifa kulikuwa namajimbo 181 bara na Chadema ilipata ushindi wa viti 5 hali CUF hawakupata kitu. Zanzibar CUF walipata viti 22 kati ya viti 50. Kwa hiyo ushindi wa pili wa CUF unatokana na viti 22 vya visiwani na sio Bara. CUF haina nguvu bara sawa na Chadema isivyokuwa na nguvu visiwani.
pili, Uchaguzi wa sewrikali ya mitaa Chadema hawakushiriki na kusema kweli yalikuwa makosa makubwa. Hawakufanya hivyo kutokana na kuvunjika kwa umoja mlokuwa mmeanzisha hivyo wakaweka mawazo yao sehemu nyingine.

Swali la 4. jibu:- kuhusiana na CUF kujijenga zaidi ya Chadema. jamani lets not kid ourselves.. CUF imejijenga vipi?.. CUF na Chadema kitaasisi ni vyama ambavyo havina uwezo kabisa yaani wote wanabangaiza tu. Hili sii swala la kuhitaji mjadala kwani CUF na Chadema bado kabisa wamebanwa vibaya na CCM kiasi kwamba kujitangaza kwao kunategemea imani ya wanachama wake. Wote waliohama CUF wamepitia mitihani kama ya Chadema na vyama vingine vyote vidogo. Kumbuka kuhama kwa Lwakatale CUF ilitokea kipi.. fact is Hakuna aliye na afadhali.

5. Chadema kimeshindwa kujivua gamba la ukabila na udini na sasa ndiyo kinazidi kutopea huko wakati CUF imetanda kila pembe ya Tanzania;

Jibu:- Duh mkuu wangu, marafiki zangu wakubwa ni member waCUF damu, na kijiwe changu kikubwa ni pale K tea shop mjini Chagga st... ninawajua CUF kuliko unavyofikiria. Chadema kama ni Wadini au Wakabila, ni CUF pekee ndiyo ingeweza kuwaondoa ktk fikra hizo kama zipo kweli na mngewa join, lakini sio kuzungumzia nje hali CUF yenyewe inaonekana kusongwa na matatizo hayo hayo. Ushahidi wangu:- Why CUF imejikita kwa maswala ya Zanzibar zaidi ya bara?.

6. CUF kina mtandao wa chama wenye muundo uliokamilika wa uongozi uliojipanga kitaasisi wakati Chadema hakina muundo na huishia kuokota wajumbe wa vikao mitaani kupata uhalali wa vikao.

Jibu:- Chadema sii wajuzi wa kila kitu, vitu kama hivi ndivyo CUF could have bring in kama mchango wao. haiwezekani Chadema kuhitaji kuungana na chama ambacho hakina ubora wowote.

7. CUF kimeonyesha umakini mkubwa katika uongozi na hata katika Kambi ya Upinzani Bungeni kimeonyesha ukomavu tofauti na Chadema ambao hata wale wabunge wake 11 tu wanashindwa kuelewana..

Jibu:- Bungeni sio mahala pa kuonyesha unyenyekevu. Ni sehemu ya kuvuana nguo na sio kubebana kama CCM wanavyofanya ili mradi kulindana. Bungeni wajumbe wanakuja kuwakilisha wananchi na sio kuwakilisha chama. Kutoelewana ndio inaonyesha ukomavu wa watu kuona tofauti au matatizo ya bajeti inaposoimwa na sio kukubali kila unachoambiwa.

8. CUF kina misingi ya kidemokrasia na ndiyo maana hata Prof. Safari aliachiwa kushindana kwa uwazi na Prof. Lipumba kwenye nafasi ya Uenyekiti wakati Chadema kina uongozi wa kiimla wa muasisi wa Chama mwenye uwezo wa kumuengua mgombea Uenyekiti ili mkwewe apite bila ya kupingwa:

Jibu:- Kugombea kiti cha Uenmyekiti sio swala la demokrasia. hakuna kifungu chochote cha demokrasia kinacholazimisha au kushauri vyama kupitisha uchaguzi inapofikia swlaa la Mwenyekiti.. Na pengine huelewi kwamba Chadema mwenyekiti ni Mbowe na anayegombea Urais ni Dr.Slaa wakati CUF mwenyekiti ndiye mgombea kiti cha urais!

Yaani Rev. mkuu wangu huyu jamaa majibu tyake ni rahisi sana naweza kuyajibu pasipo hata kufikiria..Ila sidhani kama yeye yupo tayari kupokea maswali kutoka upande huu!.


Asante niliyokupa ni ya content pamoja na mpangilio mzima wa majibu yako mkuu!

Posts nyingine zaweza kuwa nzuri lakini mtu akashindwa kuzisoma kwa jinsi zilivyokosa mpangilio; big up bro!
 
Lakini huyu Jussa ni swahiba mkubwa sana wa fisadi No 1 hapa nchini - RA. Anatuambia nini? Ni yeye ndiyo anacoordinate contributions to CUF from RA, pesa ambazo ni za wananchi alizoiba BoT. Na ndiyo maana kama mtakumbuka Mengi alipowataja mafisadi papa, Lipumba alitoa statement ya kumshambulia Mengi huku anajua wazi kwamba baadhi ya mafisadi papa hao waalipelekwa mahakamani. Kuyumba kwa Lipumba kuhusu ufisadi kulishangaza wengi na ni influence ya RA through Jussa.

Na kilichomkimbiza Lwakjatare kutoka CUF mnakijua? Ni michango hii ya kifisadi wanaopokea CUF kisirisiri kutoka RA, michango ambayo viongozi wa chama hicho walikuwa hawataki kueleza chanzo. Hizi habari ni za uhakika kabisa -- kuna siku Lwakatare atakuja kumwaga yote hadharani -- tena kwa ushahidi.
Onother UMBEYA/MAJUNGU. unajua ruzuku wanayopata CUF?
 
Sasa mlimtegemea huyu Mheshimiwa Jussa aseme nini? Yeye ni mwanachama wa CUF na anataka chama chake kishinde. Mpingeni hoja zake kama alivyofanya Mkandara na si kuingiza mambo ya kutupiana matope.

Amandla.....

Yaani ingekuwa watu wengi humu JF ni kama wewe, nafikiri ingekuwa raha saana. Nakupa 5 mkuu..
 
..lakini Jussa anamchukulia Maalim Seif kama Mungu mtu.

..sitegemei kiongozi yeyote yule wa upinzani aeneze kampeni chafu namna hii dhidi ya chama kingine cha upinzani.

..kama hawakubaliani, that is fine, lakini siyo waanze kupakaziana masuala ya ukabila,udini, etc etc.

..jambo lingine la ajabu sana ni kwamba Jussa anadharau uzoefu wa miaka 15 wa Dr.Slaa kama mwakilishi wa Karatu ktk wa bunge la Muungano.
 
Hujajibu hoja mkuu. Ungefanya jambo la busara sana kama ungejibu hoja kwa vigezo vinavyofanana na jinsi jamaa alivyoandika na si majungu. Mfano, jamaa kasema uchguzi wa serikali za mitaa CUF ndo ilikuwa ya pili bara baada ya CCM, sasa na wewe labda sema CHADEMA ilikuwa hivi na vile...... CUF ni chama cha kileberali na chadema hawaeleweki na wewe sema chadema ni mlengo fulani, si masuala ya kuleta porojo humu mara kajiunge na hizbula, mara nini. Yo wrote non sense man, I'm sorry

Penye rangi: Yeah, angetaja kwa mfano CUF ilitoka kapa kabisa katika viti vya Ubunge huku Bara mwaka 2005 na kwamba hiyo 'ndoa' yao na CCM imekiweka chama hicho ktk hali ngumu kwani kinaonekana kuelekea kwenye u-CCM-B na huenda kikapoteza kura nyingi pamoja na madiwani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom