Wadada badilikeni jamani, uongo wenu utawamaliza. Kuna mdada tumefahamiana siku 1 baada ya hapo tukawa tunawasiliana, hi leo tukakubaliana kuonana maeneo ya Feri-Kigamboni(alipenda hapo mana anakaa Kibada-kigamboni pia lengo kuu ilikua just kufahamiana). Nikamuambia aamue muda gani ni convinience kwake itakayo faa kuonana, hatimaye ka sugest kua ni saa 12:30 jioni. Ilipofka saa kumi jioni nikanza safari nikitokea Mbezi, nkafka posta, nkapanda Bodaboda mpaka Fery, nikavuka(muda wote nampa update ya safari). Nlipoanza kuvuka aka niupdate kua naye ndio anatoka home, bada ya kuvuka nkanza kumsubiria mpaka saa moja kamili, ikabdi nimpgia akasema amefka geti jeusi(kituoa jirani na feri), ikafka saa mbili dakika 5, nkapgia tena akasema amefka na yupo karbu na standi ya daladala. Nkamwambia nami nipo hapo, akakata simu, bada ya dak 5, akanitext "please wait kidogo" saa mbili na 30 nkapga simu akaniambia hvi "SAMAHANI NISAMEHE NIMESHNDWA KUJA". In short imeniuma sana na wadada kweli mmenikatsha tamaa na nimewachukia sana, nimeteseka sana na daladala muda huu ndio nafka geto! kibaya zaidi ni mara ya pili hili likinitokea! Wadada! wadada! wadada!