Vile vile bahati nzuri sina tamaa ya fedha na naridhika na ninachokipata. Mwaka 2005, nakumbuka baada ya kumaliza shule, bi Mkubwa wangu siku moja aliingia chumbani mwangu bila mimi kujua na kuweka kwenye kabati langu la nguo begi dogo jeusi, lililokuwa na nembo iliyosomeka "Sport" mimi nilipoliona sikuwa na wasiwasi kuwa labda kuna kitu kibaya (silaha au mali ya wizi) imefichwa chumbani mwangu. Chumbani mwangu nilikuwa naingia na marafiki zangu ambao nao ni waaminifu. Hakuna hata rafiki yangu mmoja aliewahi kupekua.
Baada ya miezi miwili bi Mkubwa akaniambia nimpelekee lile begi sebuleni na nimsaidie kuhesabu. Nilihesabu zilikuwa Tsh 60milioni. Na sijaiba/wala kuibiwa hata thumni.