MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,194
SIKU chache baada ya Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC- CCM) kumteua mfanyabiashara, Mohammed Raza kuwania nafasi ya Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika Jimbo la Uzini, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimejibu mapigo.
Katika kuhakikisha kuwa kinalinyakua Jimbo hilo, Chadema imemteua Ali Mbarouk Mshimba kuwa mgombea wa Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho kwa Jimbo hilo la Uzini.
Taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Mwandamizi wa Habari na Uenezi, Ofisi ya Makao Makuu ya Chadema, Zanzibar, Dadi Kombo Maalim ilisema uteuzi huo umefanywa na Kamati Kuu ya Chadema Taifa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, uteuzi huo ulifanywa katika mkutano wa kawaida uliofanyika Dar es Salaam jana chini ya Makamu Mwenyekiti Taifa (Bara), Said Amour Arfi na Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa.
Uamuzi huo ulipitishwa kwa kauli moja na Kamati Kuu ya chama Taifa baada ya kupokea
taarifa ya mchakato wa uteuzi wa awali uliofanywa na ngazi husika za Chadema Jimbo la Uzini iliyowasilishwa na Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Hamad Musa Yusuph.
Katika taarifa hiyo Kamati Kuu ya Chama Taifa ilielezwa kwamba uchukuaji fomu za uteuzi wa ndani ya chama ulianza Disemba 15, mwaka jana na kuhitimishwa Januari 15 mwaka huu ambapo jumla ya wanachama watatu walichukua fomu za kugombea.
Kura za maoni za uteuzi wa mgombea zilifanywa Januari 17, mwaka huu ambapo Ali Mbarouk Mshimba alikubaliwa kwa kura zote 126 za wajumbe waliohudhuria mkutano mkuu wa jimbo, kati ya wajumbe 130 waliopaswa kuhudhuria kutoka katika shehia zote 13 za Jimbo la Uzini.
Mapendekezo hayo ya Jimbo la Uzini ya kumteua Ali Mbarouk Mshimba yaliridhiwa na kikao cha Kamati ya Utendaji ya Wilaya ya Kati kilichofanyika Januari 18, mwaka huu.\
Source:gazeti la habari leo januari 22, 2012
HONGERA CDM KWA KUDUMISHA MUUNGANO
Katika kuhakikisha kuwa kinalinyakua Jimbo hilo, Chadema imemteua Ali Mbarouk Mshimba kuwa mgombea wa Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho kwa Jimbo hilo la Uzini.
Taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Mwandamizi wa Habari na Uenezi, Ofisi ya Makao Makuu ya Chadema, Zanzibar, Dadi Kombo Maalim ilisema uteuzi huo umefanywa na Kamati Kuu ya Chadema Taifa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, uteuzi huo ulifanywa katika mkutano wa kawaida uliofanyika Dar es Salaam jana chini ya Makamu Mwenyekiti Taifa (Bara), Said Amour Arfi na Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa.
Uamuzi huo ulipitishwa kwa kauli moja na Kamati Kuu ya chama Taifa baada ya kupokea
taarifa ya mchakato wa uteuzi wa awali uliofanywa na ngazi husika za Chadema Jimbo la Uzini iliyowasilishwa na Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Hamad Musa Yusuph.
Katika taarifa hiyo Kamati Kuu ya Chama Taifa ilielezwa kwamba uchukuaji fomu za uteuzi wa ndani ya chama ulianza Disemba 15, mwaka jana na kuhitimishwa Januari 15 mwaka huu ambapo jumla ya wanachama watatu walichukua fomu za kugombea.
Kura za maoni za uteuzi wa mgombea zilifanywa Januari 17, mwaka huu ambapo Ali Mbarouk Mshimba alikubaliwa kwa kura zote 126 za wajumbe waliohudhuria mkutano mkuu wa jimbo, kati ya wajumbe 130 waliopaswa kuhudhuria kutoka katika shehia zote 13 za Jimbo la Uzini.
Mapendekezo hayo ya Jimbo la Uzini ya kumteua Ali Mbarouk Mshimba yaliridhiwa na kikao cha Kamati ya Utendaji ya Wilaya ya Kati kilichofanyika Januari 18, mwaka huu.\
Source:gazeti la habari leo januari 22, 2012
HONGERA CDM KWA KUDUMISHA MUUNGANO