Ali Kiba-Simba Mnyama (Simba Anthem)

Ali Kiba-Simba Mnyama (Simba Anthem)

Huo ndio wimbo wa taifa wa simba?
Na hiyo style mnacheza mmeshika mikuyenge?
 
Yaani nyie kweli madunduka, huyo kiba ni Yanga damu, mnaenda kuilazimisha furaha kwake🤣
 
Goma ni lenyewe hili ... tukutane tar 6

Unyama Mwingi
 
Kiba chukua maokoto yako hapo umbumbumbuni
Yaache makolo yazubae
Af yakikuamini tuletee siri zote yanga
Yanga bingwa tena
 
Kuna baadhi ya vitu unaweza kuhama/kuacha/kubadilisha kama mke, gari, dini, nyumba, n.k. lakini kuna vitu viwili nahisi haviwezekani kabila na kuwa shabiki wa Simba/Yanga. Ndio maana ninapowaona baadhi ya watu wanapohangaika kuwa "serious" na sijui Manara kaenda Yanga, Diamond kahamia Yanga na sasa Kiba kahamia Simba nawashangaa sana. Kiukweli hizi timu mbili ni kama makabila huwezi kuhama kabila lako hata siku moja. Kwa hiyo hao wakina Manara, Diamond na Kiba waacheni watafute mkate wao wa kila siku.

Na kwa Kiba na Simba ni "win win" kwani Kiba atapata pesa na Simba itaingiza pesa na zaidi ni majibu kwa Diamond kuhamia Yanga lakini viongozi wanajua kabisa Kiba ni Yanga lakini hana madhara kwani haingii kwenye "dressing room"

Ni mtizamo tu.
 
Back
Top Bottom