Ali Kiba Fans' Special Thread...

Ali Kiba Fans' Special Thread...

nimemuona mimi katoka kimasomaso,

uzuri anao na sura naitangaza hii leo,

waje waje wanafiki leo mtajionea,

yaliyosemwa jana yamejirudia haya,

unalia nini mwenzako nimeshajenga nyumba ya kuishi sisi wawili,

tujenge tuwe na famili,

waache waseme wewe leo uko na mimi,

natule hizi raha tusahau ya duniani.

#Alikiba-kimasomaso
 
King anajua kuniweza, anafanya nimsubiri kwa hamuuuuuu, maana najua tu booonge la kitu kinakuja, hiyo colabo na fundi mwenzie daaaah, ninavyomkubali Bella sipati picha!

hiyo collabo itakuwa ni hatari sana. tuombe uzima tu atoto
 
Last edited by a moderator:
Kwa sauti Kiba hana mpinzani. Kwa plan za muziki wa kimaendeleo jamaa kaputi kabisa. Ngoja tusubiri kupata sauti kinanda tuwe tunaburudisha nafsi zetu kitandani.
 
Jaman wale ambao hatukulipia ving'amuzi na kushindwa kuona interview ya kiba citizen tv
...kiba leo ameirusha kwenye page yake YouTube nendeni mkaone busara za mfalme.
#:thumbup:kibamiakaelfumoja
 
Jaman wale ambao hatukulipia ving'amuzi na kushindwa kuona interview ya kiba citizen tv
...kiba leo ameirusha kwenye page yake YouTube nendeni mkaone busara za mfalme.
#:thumbup:kibamiakaelfumoja

Nilisubcribe basi fastaaa nikapata taarifa nimeshaicheki kwa mara nyingine.
 
Ku subcribe ndo unafanyaje mamy ata sijuii nielekezeee

Ukiingia tu kwenye ile page ya video, chini ya video upande wa kulia karibu na panapoandikwa views kuna mahali pameandikwa "subcibe" basi wabofya tu pale yakheee
 
Ukiingia tu kwenye ile page ya video, chini ya video upande wa kulia karibu na panapoandikwa views kuna mahali pameandikwa "subcibe" basi wabofya tu pale yakheee

Pale tayar mbona nimemsubcribe kiba na nikirudia inaniambia tayariii
 
Hivi Kiba kajibu jibu gani baya kuhusu diamond kwenye iyo interview ?
Maana kuna bint kasema bifu aliishi mpka Kiba aache kufanya interview za kipuuzi na asitembelee nyota ya dai

Alikiba aliulizwa maswali kama haya kuhusu dai...
Vip nyie mna bifu?
Akasema hapana hatuna bifu.
Akaulizwa tena "inavyojulikana ni kwamba wew ndo ulikuwa star ukaamua kupumzika ili umwache dai ang'ae"
Akajibu akasema tangu hajaacha mziki dai alikuwa anaimba na hawezi kusema kuwa yeye aliacha ili dai ang'ae hapana maana kuna vanesa barnaba omy dipos nk. Ambao waling'aa enzi hizo pia.
Akaulizwa kuwa "inajulikana daimond ni staa afrika na ni hard work vipi unalizungumziaje?
Akasema ni kweli kijana ni hard work na anafanya vyema.
Ndo ilipoishia hapo mkuu.
 
Naamini huu uzi ulianzishwa maksusi kwa ajili ya kujadili mafanikio yw Kiba, kutoa ushauri kwenye changamoto anazokumbana nazo na kuzitatua. Aidha, kumkosoa na kumpa mawaidha mema ili aweze kufanikiwa kimuziki.

Kinachonishangaza ni kugeuzwa kijiwe cha kusutana na kutoleana kauli zisizofaa. Tutumie vema majukwaa haya kwa maslahi ya wanamuziki na muziki kwa ujumla.

C.c nifah, I love you, cute b, forget about the past, my previous comments was meant to challenge your IQ and not insults as you used to perceive. I love you all, best wishes.
 
Goooood night guys.
Daah i love this pic, that smile though!
 

Attachments

  • 1436387374101.jpg
    1436387374101.jpg
    48.3 KB · Views: 162
Invisible hivi kwanini bado mnafta comments zetu yani sisi tupoteze mda wetu Ku comment nyie mfute. Ina maana gani basi kuwa na uu Uzi si muufunge tu watu tujue mana kuna mitandao mingine ka Instagram na fb. Mnalolifanya sio vizuri acheni mambo yenu ya ajabu kila siku tu mlalamikiwe. Fanyeni kazi yenu MNA bore. Hapa mtasubiri ka siku nne mfute tena. Wee Moderator wa hili jukwaa ujumbe ukufikie funga kabisa uzi kuliko ku delete comments. Bila sisi ungekua unafta nini. Avemaria ma dia hebu njoo huku.
 
Last edited by a moderator:
Niniiiiiiiiiiiiiii??? Inamaana tangu asubuhi tulikuwa tunafanya nini hapa?
Hiii nii zaidi ya chuki.
Adi natetemeka hasira.
Kwa nini coment zetu zifutweee? Invisible Moderator JAMII Forum.
Ni nini tumewakosea ninyi watu??
Mbona mnakuwa na tabia za kichuki juu yetu?....naichukia JAMII FORUM acha niangalie somewhere to go...
Sad
 
Last edited by a moderator:
Invisible hivi kwanini bado mnafta comments zetu yani sisi tupoteze mda wetu Ku comment nyie mfute. Ina maana gani basi kuwa na uu Uzi si muufunge tu watu tujue mana kuna mitandao mingine ka Instagram na fb. Mnalolifanya sio vizuri acheni mambo yenu ya ajabu kila siku tu mlalamikiwe. Fanyeni kazi yenu MNA bore. Hapa mtasubiri ka siku nne mfute tena. Wee Moderator wa hili jukwaa ujumbe ukufikie funga kabisa uzi kuliko ku delete comments. Bila sisi ungekua unafta nini. Avemaria ma dia hebu njoo huku.

Hiii imeshakuwa common adi sielew tunawakosea nini hawa watu...ujue hasira imenikaba adi natamani ningekuwa naishi na hawa ma mode jirani.
 
Last edited by a moderator:
Invisible kuna tatizo gani? Kwa nini mnatufanyia ivyo kila siku?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom