Albert Msando sio raia wa Tanzania?

Albert Msando sio raia wa Tanzania?

Wakili huyu maarufu ameshutumiwa kuwa sio raia wa Tanzania.wazazi na ndugu zake wahojiwa kuhusu suala hilo.



=======Updates =======
.... kwa nchi kama Tanzania uraia wa mtu ni rahisi sana kuthibitishwa,mamlaka husika wafanye kazi yao tu....lakini ole wao wahamiaji haramu walioko ktk ardhi hii.
 
Acha uvivu kama umeweza kubrowse Jf unashindwa vipi kupitia blogs mbalimbali?

yaani ziletwe tuhuma halafu ushahidi tukatafute wenyewe? ni jukumu la anayeshitaki kuleta ushahidi. Kuna ugumu gani wa kulink kwa a "great thinker"?
 
yaani ziletwe tuhuma halafu ushahidi tukatafute wenyewe? ni jukumu la anayeshitaki kuleta ushahidi. Kuna ugumu gani wa kulink kwa a "great thinker"?
Mimi sijashitaki!!
 
vita gani?mnawezaje kushinda vita wakati zile ziara za mikoani zilishindwa kabla ya kuanza?
 
Hawa wachumia tumbo watawezaje kushinda vita ilihali tu mipango yao ya matamko uchwara imeshindwa vibaya? Hawana jipya zaidi ya kutapatapa kunakosababishwa na kuandamwa na dhambi ya usaliti!
 
Alipataje sifa za kujiunga na CHADEMA ilhali sio raia wa Tanzania? Kumbe CHADEMA hawako makini kabisa.

Mbona hata wenje sio raiya ,hata mbowe kuna taarifa kuwa ana asili ya somalia
 
High school kasoma Ilboru (HGL). Yeye aliingia Ilboru July 1997 ilhali kaka yake George Mwaria aliingia ILboru (A-level, the same school) mwaka 1994. Nawafahamu wote na walijulikana kama wachaga kutoka Moshi. Hii ya kutokuwa raia ni habari mpya kabisa!

Labda vigezo walivyotumia ni vipi?
 
Huyo albert msando ni nai hatumjui ana msaada gani kwa nji hii??
 
Ni Raia Wa Wapi Na Evidence Zipi?
Well, hatujui ni raia wa wapi, na hatuna evidence za alizaliwa wapi akaja akasajiliwa wapi, tunachojua ni kwamba anadaiwa yeye sio Mtanzania.

Sasa, huwezi ku prove a negative, yani sisi hatuwezi kuthibitisha kwamba yeye hajazaliwa ama hajasajiliwa Tanzania, ila yeye anaweza kusaidia ku prove a positive kwa manufaa yake yeye. Athibitishe - kwa makarati yake kutoka idara ya vizazi na vifo au taasisi za uhamiaji na uraia - kwamba yeye ni raia wa Tanzania. Unapoenda kuomba pasi ya kusafiria au labda kitambulisho cha taifa au kadi ya mpiga kura, kwa mfano, WEWE ndio unatakiwa ututhibitishie sisi kwamba WEWE ni Mtanzania.

Hilo moja, la makaratasi yake. Lakini la pili, kwa Tanzania haitoshi tu kusema nimezaliwa Tanzania. Itabidi pia atupe na makaratasi ya kizazi chake cha nyuma kutoka idara za Vizazi na Vifo au Uhamiaji na Uraia.
 
Zitto kwa kujua kutengeneza allies tu, sasa msando na issue yake na Maswi wapi na wapi jamani?
 
Last edited by a moderator:
Labda vigezo walivyotumia ni vipi?

Sijui kwa kweli. Kitu cha kujiuliza ni kwanini uhamiaji wameamua kudadavua uraia huyu jamaa akiwa kama Albert Msando wakati huohuo hawajihangaishi na uraia wa wazazi wake? Wazazi wake bado wapo hai tu. Anyway, hili jambo tuwaachie vyombo husika (uhamiaji), wao wanajua sababu hadi kufikia hatua hii.
 
Sidhani kama hawajui kwamba yeye ni Mtanzania kindakikindaki bali kutakua kuna jambo jingine wanamtafuta! Hii kitu nikidhani wanasumbuliwa Kagera na Kigoma kumbe sasa hata Kilimanjaro imeanza?! Ajabu hawahangaiki na Matajiri wa Kiarabu na Kisomali wanao hujumu Taifa kwa kupora wanavyotaka na kuchangia CCM makombo!

Hawa sio raia? Umetumia vigezo gani? Suala la uraia lisipochukuliwa vyema hutupeleka kwenye ubaguzi wa rangi. Hebu jiridhishe kwanza kisheria kama hawa unaowatuhumu kweli sio raia kabla hujaonekana mbaguzi tu wa rangi.
 
Back
Top Bottom