Albert Msando sio raia wa Tanzania?

Albert Msando sio raia wa Tanzania?

Yule ni msomali,


Unazungumzia Kinana, Msando, Jenerali Ulimwengu au Bashe?...Kwa kawaida siku hizi inapofika uchaguzi hao wote (hata mimi na wewe ) ni wahamiaji haramu bila kujali wanatoka chama gani kwani unapotishia kumega tonge lao lazima watumie dola kukukandamiza wakati zamani haikuwa hivyo na ndimo tuliweza kupata mawaziri mahili kama Amir Jamaal na akina Dereck Bryson-Mbunge Kinondoni na waziri mpaka alipokufa, hebu jaribu ku rewind nyuma na uwafufue watu hao leo uone kama wanaweza kugombea Ubunge wa ndani ya CCM
 
Kuna wakati unajiuliza bora nini, kuwa mwana CCM au kuwa mchawi? Nadhani bora kuwa mchawi kuliko mtu kuwa ccm
 
Hizi siasa za uraia ni ujinga , hivi raia halisi ni yule wa Msoga au?
 
mtoa mada angeweka source sio kuleta habari kihivi hivi tu, sio wote tunaofuatilia social networks
Acha uvivu kama umeweza kubrowse Jf unashindwa vipi kupitia blogs mbalimbali?
 
Kwenye hili swala tusitake kumuonea kabisaaa!
 
Raia wa Tanzania asie kua mzalendo ni sawa na mhamiaji haramu! May be Uhamiaji wako sahihi katika hili ...
 
Wakili huyu maarufu ameshutumiwa kuwa sio raia wa Tanzania.wazazi na ndugu zake wahojiwa kuhusu suala hilo.



=======Updates =======

Hii ni move ya kijinga. Ni move yao wenyewe ili mwishoni waje waseme kuwa Uhamiaji walipewa taarifa na CHADEMA ili ionekane CHADEMA wanamfuatilia.
 
Tuna mjua vizuri kakulia hapo mashamba ya miwa moshi na kasoma UD sheria walikuwa wapi siku zote na pia ni Diwani.

High school kasoma Ilboru (HGL). Yeye aliingia Ilboru July 1997 ilhali kaka yake George Mwaria aliingia ILboru (A-level, the same school) mwaka 1994. Nawafahamu wote na walijulikana kama wachaga kutoka Moshi. Hii ya kutokuwa raia ni habari mpya kabisa!
 
Hii ni move ya kijinga. Ni move yao wenyewe ili mwishoni waje waseme kuwa Uhamiaji walipewa taarifa na CHADEMA ili ionekane CHADEMA wanamfuatilia.
Itakuwa 'movie' ya kitoto sana kama ni hivyo.
 
Leo tarehe 26.06.2014 nimepeleka maelezo yangu ofisi ya Uhamiaji Moshi kuhusu uraia wangu. Kwa maelezo niliyopewa awali kuna wanaosema mimi sio Mtanzania.

Kufuatia hiyo Mzee wangu, Gaspar Mwaria Msando na kaka yangu George Mwaria Msando wamehojiwa leo kama wananifahamu.

Miaka 34 baada ya kuzaliwa hospitali ya serikali, kusomeshwa shule msingi ya serikali, shule ya sekondari ya serikali na chuo kikuu cha serikali leo natakiwa kuelezea kama ni raia.

Najiuliza, kama sio raia narudisha gharama zote za serikali? Je naenda wapi kama leo hii mimi sio raia? Stateless person?
 
Back
Top Bottom