Albert Msando afunguka kuhusu Zitto Kabwe

Divide them & thn rule

Asante mkuu kwa kunikumbusha historia,yaani kweli history deals with past,present and future events.Wenye uelewa wamekupata ila wa zidumu fikra za mwenyekiti hawawezi kuelewa.
 

ulitakaje
 

Nimekuelewa sana mkuu.....inatakiwa hii elimu nzuri uliotupa uiendeleze katika mahali unapotoka....naamin Tanzania bora itapatikana.....
 
wangemuacha mngesema anaogopwa,katimuliwa mnasema kaonewa!!!
 

Wanazani CHADEMA ni CCM ambayo SAMWELI SITA na NAPE NAUYE walianzisha Chama wakiwa Bado CCM na wakafumbiwa Macho, CHADEMA ni zaidi ya Makini.

Nape aliwaiomba gombea jimbo la Ubungo kupitia CDM akiwa mwana chama wa CCM, chama cha majambazi wakafumba macho.

Mwambieni ZZK cdm si ccm
 
Albert Msando Mmmmh!!

Ukimya ungetosha tu kwenye hili.
 
Labda kama ningekutana na huyo Msando ningemuuliza kwanza....Yeye yupo Chadema na inaifahamu chedema kuliko sisi wengine ambao ambao hatupo huko...sasa Msando anaijua vizuri katiba ya chama chake? na anaielewa? ok kama anasoma hakuona hivyo vipengele ambavyo yeye leo anaona chama chake si cha kidemokrasia?
 
Hoja dhaifu kabisa na zisizo na mashiko kutoka kwa mtu ambaye ni ati ni mwanasheria. Na kama hoja zenyewe ndio hizi hata huyo Zito mwenyewe namuonea huruma kwa ushauri aliokuwa akipewa na kuupokea.
 
Naye si aondoke tu CHADEMA.

Analialia nini sasa?

Kesi mmeshindwa. Mteja wako kafukuzwa. Hivyo kulialia hakusaidii. Au analialia ili aonewe huruma?

Umefukuzwa, ondoka. Vyama vya kisiasa Tanzania si CHADEMA peke yake.

Kajiungeni na chama cha Dovutwa huko.
 
Msando kama anaona hakuna demokrasia CHADEMA kwanini yeye anaendelea kuwa mwanachama? si bora atafute chama kingine ambacho anaona kinatenda haki zaidi kadri anavyotaka yeye
 
CHADEMA watamkumbuka sana ZITTO.

Ni zaidi ya miaka miwili na zaidi sasa tokea CHADEMA iwe mbali na ZZK, kama hakukumbukwa kipindi chote hicho si rahisi kukumbukwa sasa wala badae. Hata angeendelea kuwepo ndani ya chama, mchango wake ulishapotea muda mrefu sana.

Hili suala limefikia lilipofika kwa sababu ZZK mwenyewe kaamua lifike hapo, angetaka lisingefika hapo. Mbona David Kafulila alikumbwa na tatizo kama lake, lakini sasa hivi yupo na anaendelea kuwepo ndani ya NCCR? Kafanya nini Kafulila ambacho ZZK kashindwa kufanya?

Nafikiri alitakiwa kutambua tokea mwanzo kuwa demokrasia ni sauti ya wengi hata kama hawapo sahihi. Inawezekana kweli kamati kuu wapo wrong, lakini tukumbuke kuwa wao ndio walioifikisha CHADEMA hapo ilipo na hivyo ili waendelee ni lazima wawe sauti moja.

Kama ndani ya kamati kuu kuna mtu ambae hakubaliani na ile sauti moja, basi si vibaya akitoka ili wanaokubaliana waendelee kwa namna ile ile wanayokubaliana. Ni vizuri atoke ili akaendeleze harakati zake sehemu nyingine, chama kiendelee kuwepo na yeye aendelee kuwepo. Bila shaka siku moja wote watakutana katika kujenga nchi yetu wakiwa vyama tofauti lakini vyenye lengo moja.
 
katiba ni chombo kilicho tungwa ili kusimamia haki na usawa hivyo yeyote ataye kiuka masharti ya katiba lazima katiba hiyo hiyo imwajibishe pole sana kamanda zitto kabwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…