Haya majanga yataitokea puani serikali ya ccm kwasababu wamewapa wanafunzi ruhusa ya kula, kuchati fb,kusikiliza miziki ya bongo fleva, kuzurura halafu pktoba wakutane mjengoni. Haingii akilini kufanyia majaribio maisha ya watu kwakuwaharibia mfumo wamaisha kwakuwapa mwanya mkubwa wakufaulu kwa marks za ajabu ajabu, ama kweli kipofu kaona mwezi kadhani harufu ya wali. Hongereni kwa huu upofu mnaozidi kuuendeleza,hiyo ''big results now'' inawazuzua hadi mnaleta majanga yatakayogharimu maisha ya watoto wetu. Watanzania wenzangu tutambue kwamba watoto wetu ndio watakaoathirika na mfumo huu usio na chembe ya matumizi ya akili ya kawaida ktk kufikiri,kuamua na hao wadau ambao mnasema mmewashirikisha inaleta utata na wao pia inawezekanaje washiriki upuuzi huu kama ni wadau wa elimu kweli ????????? Serikali kama kweli hili mmeliamua liwe hivi kwanini waziri anapingana na katibu mkuu wake???? Kwanza hii ni dalili yakukurupuka, pili wizara na watendaji wake wote hawajui watendalo,tatu, wizara haina bodi yawashauri wakitaaluma ndio maana kila mtu anakuja na wazo lake halafu mnaishia kuzozana kwenye vyombo vya habari......aibu yenuuuu hiyo wizara ya elimu. Na wewe rais inakuwaje unamtoa mtu kwa matrekta ,ma cartepiller unampa wizara ya elimu???????/ huoni kama unawadharau wananchi sasa hebu ona madhara yake watu wanaamka nakuja na upuuzi eti wanafanya majaribio kwamda wamiaka minne... Hebu tufikiri haya sio mahindi wala kilmo cha pamba ambacho unaweza chukua mbegu fulani kujaribu kama zinaweza kuzalisha magunia mengi, hii ni elimu na maisha ya watu hebu acheni huu upuuzi na maisha ya watu.