Kundi la wapiganaji la Somalia la Al Shabaab limefadhaishwa na taarifa za Kenya kuwahusisha na utekaji nyara wa raia wa kigeni wanne, wamedai wenyewe hawajihusishi na utekaji nyara wala uharamia na wanahisi Kenya inataka kuwachafulia CV yao.Wamesema taarifa hizo sio sahihi na kundi hili linalinda ardhi ya Somalia ambayo kwa sasa haina serikali na maadui zao huwa 'WANAWALIPUA TU' na hili la utekaji nyara na uharamia wa baharini unafanywa na wahuni tu ambao wao pia huwapinga.