Ajinyonga baada ya kugundua ana virusi vya Ukimwi

Sophia Charles Odipo mwenye umri wa miaka 23 Mkazi wa Mseto amefariki baada ya kujinyonga chanzo kikiwa ni baada ya kwenda Hospitali kupima afya yake mara mbili na kugundulika ana maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amesema "Huyu Dada alijinyonga kwa kamba mpaka kufa chumbani kwake baada ya kwenda Hospitali na kugundulika ana maambukizi ya UKIMWI"

Millard
Duh,huzuni kubwa sana,sasa sijui wale wanaosema haupo hapa watazungumza nini.Jamani tusijidanganye,Ukimwi upo na unauwa,tuendelee kuchukua tahadhari,unapokupata hutakuwa na wanzako unabaki peke yako ukitafakari na nafsi yako,hapa ndipo panapohotajika hekima ya Mungu either uendelee kupambana kwa kuishi nao au ukate tamaa na kuamua kujitoa uhai...
 
Waliompa majibu hawakumpa Ushauri Nasaha! Siku hizi ugonjwa huo ni wa kawaida kama unapata ushauri nasaha.Wapo watu ambao wanakaa na hao wadudu mpaka miaka 20!
 
Au alibakwa maana kama alikuwa anawaachia mabaharia wanamwagia ndani alifikiri UKIMWI umeenda likizo
 
Waliompa majibu hawakumpa Ushauri Nasaha! Siku hizi ugonjwa huo ni wa kawaida kama unapata ushauri nasaha.Wapo watu ambao wanakaa na hao wadudu mpaka miaka 20!
Hiyo 20 inafika kwa tabu nyingi,juhudi nyingi,mixer hofu. Na hata akipata magonjwa nyemelezi na yakamsumbua kisha akapona watu mnaweza asijue.

Halafu unaposema miaka 20 mbele maana yake age akiwa na miaka 43
 
Hayo mambo ya figo na hiyo dialysis mbona yako huko nchi maskini tu [ Ingawa nyie Jiwe aliwaita DONOR country!] , lazima hizo dawa zinazoletwa huko zina walakini!! Huko majuu wenye virusi wanatumia dawa na hawapati hizo side effects!!
Magic jonson inasemekana ana ngoma tokea 90s mpaka leo anadunda au jamaa ametupiga kamba 🙂🙂🙂🙂
 
Huku Njombe UKIMWI ni sawa na mafua tu. Sasa nijinyonge kisa mafua!!
 
Sheria ya mungu ipo too straight, sofia atakwenda jehanamu..kwa kosa la kukatisha uhai wake wa kusudi..neno R.I.P linatumika vibaya
 
Sophia Charles Odipo mwenye umri wa miaka 23 Mkazi wa Mseto amefariki baada ya kujinyonga chanzo kikiwa ni baada ya kwenda Hospitali kupima afya yake mara mbili na kugundulika ana maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amesema "Huyu Dada alijinyonga kwa kamba mpaka kufa chumbani kwake baada ya kwenda Hospitali na kugundulika ana maambukizi ya UKIMWI"

Millard
kansa inaua mapema kuliko ukimwi. Tatizo mtu akishatambua ana ukimwi anawaza mambo mengiiii.

Tena ukute bado msichana hajaolewa, anawaza ataolewa na nani, atazaa na nani, future yake itakuaje.

Kuna watu wengi tuu matajiri wenye uwezo mzr wana ukimwi hawana wake, nao wanahitaji wake na kuanzisha familia.

pia yawezekana usiolewe na mwenye ukimwi ila unao kwa kufuata maelekezo ya kitabibu mkazaa vzr na maisha yakasonga mbele bila hata kuambukizana.
 
Back
Top Bottom