Ajinyonga baada ya kufeli mtihani wa kidato cha nne 2014

Ajinyonga baada ya kufeli mtihani wa kidato cha nne 2014

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,163
Reaction score
11,230
Kijana mmoja ajulikanaye kwa jina la John Maduhu wa kijiji cha Pandagichiza, wilaya ya Shinyanga vijijini amekatisha maisha yake kwa kuamua kujinyonga baada ya matokeo ya kidato cha nne kumjia vibaya...


Capture.JPG
 
Daah.., hivi kama ndio mdogo wako au mtoto wako utajisikiaje.., ndio tatizo la kuwapa watu pressure.
 
​yaanihuyuu uwiiii naviwangoohivii kafeliiihatahuko alikoendaaAtafeliwalahiiuA
 
Aisee inasikitisha sana yaani yy kaona uamuzi wa mwisho ni kujitoa roho
ajue aendako ni katika shimo liwakalo moto huko ndo atajuta kujipeleka

nawaonea huruma wazaxzi wake waliomsomesha na kumkuza kiasi kile
lakini hawana mtoto mweeee

poleni wazazi wake huyu aliyejisuicide
 
Yapaswa kuwepo utaratibu wa kuwaandaa watoto kisaikolojia ili wayakubali matokeo na kutafuta mbinu za kurekebisha penye udhaifu.

Mkuu Manyerere Jackton unasihi kwa wanafunzi unatakiwa utolewe wakati wote mwanafunzi anapokuwa shule kama sehem ya kumsaidia kukua kiakili, na hata mitaala yetu inasema hivyo.

Tatizo ni kwamba pamoja na uwepo wa walimu waliosomea kozi hiyo na pia kama sehem ya mafunzo yao ya ualim katika ngazi zote, utekelezaji wake kwa vitendo imekuwa changamoto hasa.

Walimu na watawala wanang'ang'aniq kumuwezesha mtoto kupata A, b, c katikavufaulu, hili ya unasihi limebaki katika makaratasi tu!

Nimewahi tembelea shule nyingi za sekondari, yes utakuta eti kunamwalim wa unasihi na ofis anayo muulize akupe file linaloonesha kuwa ameshughulikia swala la unasihi ni shida tupu!

Ni vizuri pia sisi kama wazazi kuwapa elimu ya unasihi vijana wetu, ili akifeli kama hivi asichukue uamuzi mkali kama huu, atambue kuwa amefeli kwa kuwa hakujibidiisha katika masomo.
 
Last edited by a moderator:
​yaanihuyuu uwiiii naviwangoohivii kafeliiihatahuko alikoendaaAtafeliwalahiiuA

Wewe nawe!😩ndio nini sasa umeandika? Ungefanya mtihani wa form IV ungepata Div 0. Huwa unaniudhi kutupa shida ya kusoma point zako.
 
Back
Top Bottom