Ajali ya Waziri Kigwangala: Je, kila mtanzania anahitaji matibabu bila ubaguzi?

field marshall1

JF-Expert Member
Sep 17, 2017
1,171
2,730
Nimesikitika kusikia waziri Hamis Kigwangala amepata ajali. Namuomba Mungu amponye kwa wepesi na haraka.

Hizi habari za waziri zilitangazwa sana na wengi wetu watanzania tuliziona kwenye magazeti na wengine kuziona kwenye TV's. Inapotokea ajali mengi yanasemwa kama vile mwendo, umakini wa dereva, hatari zingine kama wanyama kukatisha barabara na uchakavu/ubovu wa gari husika n.k. Lakini si nia yangu kueleza chochote au kuuliza chochote kuhusu haya hapo juu bali nitaongelea jambo moja tu kubwa ambalo wanaJamiiForums mnaweza kusaidia kutoa mawazo yenu.

Katika ajali hiyo ambayo imezungumzwa sana na vyombo vya habari hasa magazeti wale majeruhi wengine wanne pamoja na dereva hatufahamu hali zao na wanatibiwa wapi. Wengine tungependa kufahamu wanaendeleaje!

Pili ni faraja kuona jinsi Emergency unit ilivyofanya kazi kuokoa maisha yake kuanzia alivyopelekwa kwenye center ya Magugu baadaye Selian AMLC na mwisho kule Muhimbili kwa kutumia Helicopter na ndege. Hiyo system iliyotumika inahitaji pongezi kwa kufanya kazi haraka haraka kwa kuokoa maisha ya mtanzania na waziri wetu.

Swali la kwanza ninalouliza ni je huduma kama hiyo(Ndege na Helicopter) inakuwepo kwa watanzania wote wenye health insurance?

Nchi zilizoendelea hayo ni mambo ya kawaida kurusha helicopter kutoka eneo la tukio hadi kwenye hospitali ambazo mara nyingi hazipo mbali sana na miji.

Kwa wenzetu hata kama huna insurance (bima ya afya) utatibiwa na maisha yataokolewa. Hutaulizwa una bima au la.

Swali la pili, tumeona waziri amepelekwa hospitali zaidi ya moja. Ina maana bado hakuna specialized treatment kwenye hospitali zetu za mikoa au za rufaa?

Swali la tatu kwa wale raia wa kawaida wanaopata ajali kama aliyopata mhe. Kigwangalla je wanatibiwa vipi? Ke wanapelekwa kwenye specialized treatment(Kama wanayo bima au hawana)?
 
Pole ndugu, kwa Afrika kuwa kiongozi unakuwa mungu mtu. Huyo waziri hata kama hana hali mbaya atapata huduma tofauti kabisa na aliokuwa hata kama ndio wenye hali mbaya. Usishangae watu wanashinda kwa waganga kupata hayo madaraka. Unakuwa peponi ukiwa duniani.
 
Nimesikitika kusikia waziri Hamis Kigwangala amepata ajali....Namuomba Mungu amponye kwa wepesi na haraka. Katika ajali hiyo ambayo imezungumzwa sana na vyombo vya habari hasa magazeti
  1. wale majeruhi wengine wanne pamoja na dereva hatufahamu hali zao na wanatibiwa wapi...wengine tungependa kufahamu wanaendeleaje!.
  2. Pili ni faraja kuona jinsi Emergency unit ilivyofanya kazi kuokoa maisha yake kuanzia alivyopelekwa kwenye center ya Magugu baadaye Selian AMLC na mwisho kule Muhimbili kwa kutumia Helicopter na ndege. Hiyo system iliyotumika inahitaji pongezi kwa kufanya kazi haraka haraka kwa kuokoa maisha ya Mtanzania na waziri wetu.
  3. Swali la kwanza ninalouliza ni je huduma kama hiyo(Ndege na Helicopter) inakuwepo kwa watanzania wote wenye health insurance?
  4. Nchi zilizoendelea hayo ni mambo ya kawaida kurusha helicopter kutoka eneo la tukio hadi kwenye hospitali ambazo mara nyingi hazipo mbali sana na miji....kwa wenzetu hata kama huna insurance (bima ya afya) utatibiwa na maisha yataokolewa.....hutaulizwa una bima au la.
  5. Swali la pili, Tumeona waziri amepelekwa hospitali zaidi ya moja,ina maana bado hakuna specialized treatment kwenye hospitali zetu za mikoa au za rufaa? Swali la tatu kwa wale raia wa kawaida wanaopata ajali kama aliyopata mhe. Kigwangala je wanatibiwa vipi?
  6. je wanapelekwa kwenye specialized treatment(Kama wanayo bima au hawana)?
Mkuu field marshall 1
  1. Ni swali la msingi sana, tena kumetokea loss of life kwa mtu mmoja mwana fani mwenzetu, wengine hata pole tuu sikuzisikia!.
  2. Emergency unit hizo zipo kila mahali penye uwekezaji wa kimataifa kama migodini, uchimbaji wa gesi na vivutio vya utalii ambako ni mwekezaji ndio ameweka premium kubwa kwenye bima ya afya kuhusisha flying doctors, tena hospitali kubwa kwenye bima hiyo Nairobi Hospital na sio Muhumbili, the next level ni South Afrika na final level ni Europe na America na sio India!.
  3. Yes inapatikana sio tuu kwa Watanzania wote bali kwa mtu yoyote mwenye bima ya Afya ya international yenye highest premium inayohusisha flying doctors. Its very unfortunate NHIF hawana international coverage bali wana referrals only tena zitolewe na Muhimbili,
  4. Nchi za wenzetu kuwa na bima ya afya kwa wananchi wao wote ni lazima kama ilivyo kwa kuwa na social security ni lazima hata kama huna kazi utalipwa UB, hivyo huko kunapotokea emergency, they save life first, mengine yote ni next, na wenzetu na sisi tusio na bima, safari za kuingia nchi hizo huishia kweye dirisha la visa kwa sababu kuwa na bima ni lazima na kwa wasionazo unakata travel insurance ndipo unapewa visa,
  5. Kunapotokea emergency inayohusisha kuitwa flying doctors, wanakupeleka kwanza kwenye the closest proximity standard hospital, baada ya diagnosis ndipo unapelekwa kwenye specialized hospital, and take it from me, soon utasikia Dr, Kigwa is flown to India!. Situation kama hiyo ikitokea kwa wananchi wa kawaida, unahudumiwa kikawaida!.
  6. Specialize treatment ni baada ya diagnosis na prognosis.
Natoa pole na RIP kwa waliopoteza maisha, na get well soon kwa majeruhi.

P.
 
Mleta mada huduma za afya hutegemea kiwango cha bima ya afya ulichokata usilete uongo.Nenda bima yeyote ya afya ukitaka huduma inayojumuisha ambulance helikopta ndege hadi kutibiwa nje ya nchi ni mifuko wako watu wa bima watakukatia hiyo bima Bila shida nenda kampuni yeyote ya bima .Aina ya matibabu na huduma hutegemea bima uliyokata
 
Mkuu matabaka yapo tu duniani na hata mbiguni yalikuwepo kutoka kuumbwa kwa dunia na yataendelea kuwepo, ndio maana kukawa na mwanamke na mwanamme hili nalo ni tabaka, kuna malaika na sie binadamu wa kawaida, kuna tajiri na masikini, kuna viongozi na waongozwa.

It's obvious na haitakuja badilika milele. Hivyo basi tusilinganisha. Hata huko duniani unakotolea mifano iko hivyohivyo pia kiongozi anapewa kipaumbele.
 
Nimesikitika kusikia waziri Hamis Kigwangala amepata ajali....Namuomba Mungu amponye kwa wepesi na haraka. Hizi habari za waziri zilitangazwa sana na wengi wetu watanzania tuliziona kwenye magazeti na wengine kuziona kwenye TV's. Inapotokea ajali mengi yanasemwa kama vile mwendo, umakini wa dereva, hatari zingine kama wanyama kukatisha barabara na uchakavu/ubovu wa gari husika n.k. Lakini si nia yangu kueleza chochote au kuuliza chochote kuhusu haya hapo juu bali nitaongelea jambo moja tu kubwa ambalo wanajamii forums mnaweza kusaidia kutoa mawazo yenu. Katika ajali hiyo ambayo imezungumzwa sana na vyombo vya habari hasa magazeti wale majeruhi wengine wanne pamoja na dereva hatufahamu hali zao na wanatibiwa wapi...wengine tungependa kufahamu wanaendeleaje! Pili ni faraja kuona jinsi Emergency unit ilivyofanya kazi kuokoa maisha yake kuanzia alivyopelekwa kwenye center ya Magugu baadaye Selian AMLC na mwisho kule Muhimbili kwa kutumia Helicopter na ndege. Hiyo system iliyotumika inahitaji pongezi kwa kufanya kazi haraka haraka kwa kuokoa maisha ya mtanzania na waziri wetu. Swali la kwanza ninalouliza ni je huduma kama hiyo(Ndege na Helicopter) inakuwepo kwa watanzania wote wenye health insurance? Nchi zilizoendelea hayo ni mambo ya kawaida kurusha helicopter kutoka eneo la tukio hadi kwenye hospitali ambazo mara nyingi hazipo mbali sana na miji....kwa wenzetu hata kama huna insurance (bima ya afya) utatibiwa na maisha yataokolewa.....hutaulizwa una bima au la. Swali la pili, Tumeona waziri amepelekwa hospitali zaidi ya moja,ina maana bado hakuna specialized treatment kwenye hospitali zetu za mikoa au za rufaa? Swali la tatu kwa wale raia wa kawaida wanaopata ajali kama aliyopata mhe. Kigwangala je wanatibiwa vipi? je wanapelekwa kwenye specialized treatment(Kama wanayo bima au hawana)?

Weingine wanaachwa wajifia, na wengine hata majina hayatajwi
 
Dunia haijawahi kuwa mahari salama pa kuishi kwa masikini na wananchi wa kawaida. Tanzania viongozi hawajawahi kuwa makini na raia wao na ndo maana kwenye ajari za viongozi wote wa kiserikali vyanzo vya ajari huwa hatuambiwi kama makosa ya kibinadamu.
 
Hata chadema sio wanachadema wote hulipiwa matibabu Na chadema Na kubebwa Na ndege ya kupelekwa kutibiwa Nairobi Na ubeligji kama Tundu Lisu
Inasikitisha sana kuigeuza mada hii kuwa ya ushindani wa kisiasa kati ya ccm na chadema.
 
Binadamu is an unequal being, iko hivyo na ni Dunia nzima, kutegemea kwamba wewe utakuwa sawa na Waziri ni kujidanganya hakuna mahali hilo linafanyika, ndo maana hata mjamaa Nyerere yeye mwenyewe alikuwa more equal kuliko wengine hata alipotiwa sipo utakapo tibiwa wewe, chakula alichokula ni tofauti na chako, hata maji aliyoogea siyo kama yako!
 
Mimi nadhani kwakuwa ni kiongozi wa nchi anastahili huduma ambayo haiwezi kuwa sawa na mwananchi wa kawaida,ndio maana hata anapokuwa kwenye shuguli zake za kikazi hata usafiri anaoutumia yeye unakuwa tofauti na wa kwako...
 
Nimesikitika kusikia waziri Hamis Kigwangala amepata ajali....Namuomba Mungu amponye kwa wepesi na haraka. Hizi habari za waziri zilitangazwa sana na wengi wetu watanzania tuliziona kwenye magazeti na wengine kuziona kwenye TV's. Inapotokea ajali mengi yanasemwa kama vile mwendo, umakini wa dereva, hatari zingine kama wanyama kukatisha barabara na uchakavu/ubovu wa gari husika n.k. Lakini si nia yangu kueleza chochote au kuuliza chochote kuhusu haya hapo juu bali nitaongelea jambo moja tu kubwa ambalo wanajamii forums mnaweza kusaidia kutoa mawazo yenu. Katika ajali hiyo ambayo imezungumzwa sana na vyombo vya habari hasa magazeti wale majeruhi wengine wanne pamoja na dereva hatufahamu hali zao na wanatibiwa wapi...wengine tungependa kufahamu wanaendeleaje! Pili ni faraja kuona jinsi Emergency unit ilivyofanya kazi kuokoa maisha yake kuanzia alivyopelekwa kwenye center ya Magugu baadaye Selian AMLC na mwisho kule Muhimbili kwa kutumia Helicopter na ndege. Hiyo system iliyotumika inahitaji pongezi kwa kufanya kazi haraka haraka kwa kuokoa maisha ya mtanzania na waziri wetu. Swali la kwanza ninalouliza ni je huduma kama hiyo(Ndege na Helicopter) inakuwepo kwa watanzania wote wenye health insurance? Nchi zilizoendelea hayo ni mambo ya kawaida kurusha helicopter kutoka eneo la tukio hadi kwenye hospitali ambazo mara nyingi hazipo mbali sana na miji....kwa wenzetu hata kama huna insurance (bima ya afya) utatibiwa na maisha yataokolewa.....hutaulizwa una bima au la. Swali la pili, Tumeona waziri amepelekwa hospitali zaidi ya moja,ina maana bado hakuna specialized treatment kwenye hospitali zetu za mikoa au za rufaa? Swali la tatu kwa wale raia wa kawaida wanaopata ajali kama aliyopata mhe. Kigwangala je wanatibiwa vipi? je wanapelekwa kwenye specialized treatment(Kama wanayo bima au hawana)?
Kumbuka huyo yupo katika group la VIP na anakuwa treated kulingana na cheo chake; hata wodi katika hospitali kubwa zimegawanya ; mfano hospitali ya mkapa Dodoma kuna wodi za watu wa kawaida ( kama mimi hapa) , kuna wodi zinaitwa VIP 2 kwa ajili ya wabunge na wengineo ; kuna wodi zinaitwa VIP 1 kwa ajili ya Mawaziri n.k. Hzo wodi za VIP ukiingia utashangaa !
 
Nimesikitika kusikia waziri Hamis Kigwangala amepata ajali....Namuomba Mungu amponye kwa wepesi na haraka. Hizi habari za waziri zilitangazwa sana na wengi wetu watanzania tuliziona kwenye magazeti na wengine kuziona kwenye TV's. Inapotokea ajali mengi yanasemwa kama vile mwendo, umakini wa dereva, hatari zingine kama wanyama kukatisha barabara na uchakavu/ubovu wa gari husika n.k. Lakini si nia yangu kueleza chochote au kuuliza chochote kuhusu haya hapo juu bali nitaongelea jambo moja tu kubwa ambalo wanajamii forums mnaweza kusaidia kutoa mawazo yenu. Katika ajali hiyo ambayo imezungumzwa sana na vyombo vya habari hasa magazeti wale majeruhi wengine wanne pamoja na dereva hatufahamu hali zao na wanatibiwa wapi...wengine tungependa kufahamu wanaendeleaje! Pili ni faraja kuona jinsi Emergency unit ilivyofanya kazi kuokoa maisha yake kuanzia alivyopelekwa kwenye center ya Magugu baadaye Selian AMLC na mwisho kule Muhimbili kwa kutumia Helicopter na ndege. Hiyo system iliyotumika inahitaji pongezi kwa kufanya kazi haraka haraka kwa kuokoa maisha ya mtanzania na waziri wetu. Swali la kwanza ninalouliza ni je huduma kama hiyo(Ndege na Helicopter) inakuwepo kwa watanzania wote wenye health insurance? Nchi zilizoendelea hayo ni mambo ya kawaida kurusha helicopter kutoka eneo la tukio hadi kwenye hospitali ambazo mara nyingi hazipo mbali sana na miji....kwa wenzetu hata kama huna insurance (bima ya afya) utatibiwa na maisha yataokolewa.....hutaulizwa una bima au la. Swali la pili, Tumeona waziri amepelekwa hospitali zaidi ya moja,ina maana bado hakuna specialized treatment kwenye hospitali zetu za mikoa au za rufaa? Swali la tatu kwa wale raia wa kawaida wanaopata ajali kama aliyopata mhe. Kigwangala je wanatibiwa vipi? je wanapelekwa kwenye specialized treatment(Kama wanayo bima au hawana)?
Ukipatwa janga wakati upo na VIP ; jua VIP ndo atatangazwa zaidi na kuwa treated zaid yako ; ingawa na wewe utahudumiwa lakini habari zako hazitasikika. VIP anasikika zaid kwa sababu ya kujulikana na impact yake katika eneo husika au katika nchi au dunia nzima. Ila kwa Mwenyezi Mungu hakuna cha VIP ,kinachoangaliwa ni ucha Mungu na matendo yako ulioishi nayo. Hapo duniani tuwaachie VIP.
 
Mkuu matabaka yapo tu duniani na hata mbiguni yalikuwepo kutoka kuumbwa kwa dunia na yataendelea kuwepo, ndio maana kukawa na mwanamke na mwanamme hili nalo ni tabaka, kuna malaika na sie binadamu wa kawaida, kuna tajiri na masikini, kuna viongozi na waongozwa.

It's obvious na haitakuja badilika milele. Hivyo basi tusilinganisha. Hata huko duniani unakotolea mifano iko hivyohivyo pia kiongozi anapewa kipaumbele.
Huu upuuzi upo huku Afrika.

Nilipokuwa nikifanya kazi kwenye kampuni moja ya kigeni, wote tulikuwa na bima za aina moja. Pale upatapo ajali mbaya au ugonjwa ambao ni life threatening, vituo vyetu vya tiba ilikuwa Nairobi na South Africa. Utakaa hospitali ya karibu kusubiri kusafirishwa na kupata huduma ya kwanza. Mimi mwenyewe niliwahi kushughulikia evacuation ya majeruhi wawili kwa nyakati tofauti kwa kutumia air ambulance. Moja kwenda Nairobi akibebwa kutoka uwanja wa ndege wa Kahama na mmoja kwenda South Afrika akichukuliwa kutoka uwanja wa ndege Mwanza; wote kwa air ambulance toka Kenya.
 
Mkuu field marshall 1
  1. Ni swali la msingi sana, tena kumetokea loss of life kwa mtu mmoja mwana fani mwenzetu, wengine hata pole tuu sikuzisikia!.
  2. Emergency unit hizo zipo kila mahali penye uwekezaji wa kimataifa kama migodini, uchimbaji wa gesi na vivutio vya utalii ambako ni mwekezaji ndio ameweka premium kubwa kwenye bima ya afya kuhusisha flying doctors, tena hospitali kubwa kwenye bima hiyo Nairobi Hospital na sio Muhumbili, the next level ni South Afrika na final level ni Europe na America na sio India!.
  3. Yes inapatikana sio tuu kwa Watanzania wote bali kwa mtu yoyote mwenye bima ya Afya ya international yenye highest premium inayohusisha flying doctors. Its very unfortunate NHIF hawana international coverage bali wana referrals only tena zitolewe na Muhimbili,
  4. Nchi za wenzetu kuwa na bima ya afya kwa wananchi wao wote ni lazima kama ilivyo kwa kuwa na social security ni lazima hata kama huna kazi utalipwa UB, hivyo huko kunapotokea emergency, they save life first, mengine yote ni next, na wenzetu na sisi tusio na bima, safari za kuingia nchi hizo huishia kweye dirisha la visa kwa sababu kuwa na bima ni lazima na kwa wasionazo unakata travel insurance ndipo unapewa visa,
  5. Kunapotokea emergency inayohusisha kuitwa flying doctors, wanakupeleka kwanza kwenye the closest proximity standard hospital, baada ya diagnosis ndipo unapelekwa kwenye specialized hospital, and take it from me, soon utasikia Dr, Kigwa is flown to India!. Situation kama hiyo ikitokea kwa wananchi wa kawaida, unahudumiwa kikawaida!.
  6. Specialize treatment ni baada ya diagnosis na prognosis.
Natoa pole na RIP kwa waliopoteza maisha, na get well soon kwa majeruhi.

P.
Waliopoteza maisha wakina nani? Huu ni upoteshaji wa data ambao ni kosa kisheria.
 
Binadamu is an unequal being, iko hivyo na ni Dunia nzima, kutegemea kwamba wewe utakuwa sawa na Waziri ni kujidanganya hakuna mahali hilo linafanyika, ndo maana hata mjamaa Nyerere yeye mwenyewe alikuwa more equal kuliko wengine hata alipotiwa sipo utakapo tibiwa wewe, chakula alichokula ni tofauti na chako, hata maji aliyoogea siyo kama yako!
Nilipokuwa Butiama, wakati wa ujenzi wa nyumba ya mwalimu, mara nyingi tulikula pamoja na Mwalimu chakula kile kile. Sisi kila mmoja akila kwenye sahani yake lakini yeye akila na wajukuu zake kwenye chombo kimoja.

Mwalimu hata kwenda Uingereza alilazimishwa sana. Yeye binafsi alikataa kabisa. Ikafikia mpaka Mkapa mwenyewe kuingilia kati.

Tuongelee watu wengine lakini siyo mwalimu. Alikuwa zaidi ya wengi wetu tunavyoweza kufanya. Mungu amrehemu kwa kuiishi fadhila ya umaskini
 
Back
Top Bottom