Wewe ni mpuuzi, huenda umeshindwa kuelewa kiingereza, ujinga wako usituambukize na sisi. sasa nimekopi na kupesti hii habari ya BBC iliyoandikwa kwea kiswahili ili ujue kuwa wewe sikuonei kukutukana.
Feri yazama Zanzibar, 'mamia' wafariki
Mamia ya watu wanahofiwa kufariki dunia baada ya feri kuzama katika pwani ya kisiwa cha Zanzibar nchini Tanzania ikiwa imewabeba zaidi ya watu mia tano.
Zaidi ya watu arobaini na tatu wameaga dunia katika mkasa huo , mmoja wa mawaziri katika kisiwa hicho kinachojitawala amesema.
Takriban watu 260 wameripotiwa kuokolewa
Feri hiyo MV Spice Islander ilikuwa ikisafiri kati ya kisiwa kikubwa zaidi cha Unguja ikielekea Pemba ambacho pia ni kisiwa cha Zanzibar.
Hadi kufikia sasa tumeopoa miili 43, lakini tumewaokoa manusura 259
Mohammed Aboud, waziri anayehusika na maswala ya dharura Zanzibar.
"Hadi kufikia sasa tumeopoa miili 43, lakini tumewaokoa manusura 259," amesema Mohammed Aboud, waziri wa Zanzibar anayehusika na mikasa. Ameongeza kuwa 40 kati ya wale waliookolewa walikuwa na mejeraha mabaya.