ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,904
- 6,904
Wewe ni mpuuzi, huenda umeshindwa kuelewa kiingereza, ujinga wako usituambukize na sisi. sasa nimekopi na kupesti hii habari ya BBC iliyoandikwa kwea kiswahili ili ujue kuwa wewe sikuonei kukutukana.Feri yazama Zanzibar, 'mamia' wafariki
Mamia ya watu wanahofiwa kufariki dunia baada ya feri kuzama katika pwani ya kisiwa cha Zanzibar nchini Tanzania ikiwa imewabeba zaidi ya watu mia tano.
Zaidi ya watu arobaini na tatu wameaga dunia katika mkasa huo , mmoja wa mawaziri katika kisiwa hicho kinachojitawala amesema.
Takriban watu 260 wameripotiwa kuokolewa
Feri hiyo MV Spice Islander ilikuwa ikisafiri kati ya kisiwa kikubwa zaidi cha Unguja ikielekea Pemba ambacho pia ni kisiwa cha Zanzibar.Hadi kufikia sasa tumeopoa miili 43, lakini tumewaokoa manusura 259Mohammed Aboud, waziri anayehusika na maswala ya dharura Zanzibar.
"Hadi kufikia sasa tumeopoa miili 43, lakini tumewaokoa manusura 259," amesema Mohammed Aboud, waziri wa Zanzibar anayehusika na mikasa. Ameongeza kuwa 40 kati ya wale waliookolewa walikuwa na mejeraha mabaya.
kuadi mkubwa wa serikali ya umoja wa CUF na CCM. umepikwa unataka kuwapika na wengine? mpaka jana saa mbili usiku, miili 102 iliokolewa na watu wapatao 550s wameokolewa. achilia mbali waliokufa. kwa taarifa za awali, zilizotolewa na abiria waliokuwa wakisafiri katika meli hiyo ikiendelea kuzam, wanansema meli ilibeba watu zaidi 1,500 wakati uwezo wake ni 500 tu.