Kuna haja ya kuangalia haya malori yanayotoka huku kiwanda cha saruji,imekuwa kawaida kwa madereva wa hayo maloli kusababisha ajali,ni ajali nyingi zimetokea hilo eneo na kusababisha upotevu wa maisha ya watu,naweza kusema bila kupepesa macho,chanzo ni kiburi cha madereva wa hayo malori,kwani ajali zinatokea tu pale hayo malori yanaposhuka kutoka kiwandani na si yanapopanda,hii ni kutokana na mwendo mkali ambao hutoka nao juu kule kiwandani ambako ni mlimani na mwishowe huishia kushindwa kuyamudu hayo malori,hao madereva wana jeuri sana wanadai hiyo barabara ni yao na ni wavuta BANGI wakubwa.Kwa ufupi hizo ajali ni maksudi ya madereva wa hayo malori yanayobeba saruji,tena sana sana ni ya kiwanda chenyewe ndio yanayongoza kwa ajali,nafikiri kuna haja ya MV inspector wa Saruji kufukuzwa kazi ameshindwa kusimamia madereva wake pia anaitia hasara kampuni yake kwa milori yao kuangushwa kwa uzembe.Hata kuhamisha kituo kutoka kibaoni kwenda soko la nyuki hakusaidia kupunguza ajali,mi nafikiri hiyo barabara ingekuwa kwa magari madogo tu hayo malori yangetengenezewa barabara yake ,ambayo ingekuwa haijanyoka ingeenda upande upande hadi boko halafu ndio iingie barabara kuu,ni kama vile pale Korogwe kwenye hotel ya Dar Express walivyofanya kwenye ile barabara kuu ya Moshi-Tanga