AJABU: Chenge aitetea DOWANS ilipwe!

Tafadhali Baba Chenge, usitumie Udhahifu wa Viongozi wetu kuiua nchi yako. Sisi vijana wako utatuachaje kama Mwenyezi Mungu leo na kesho akikuita! Tuachie hata hiki kidogo tunachoweza kukiokoa.

Na Mungu akubariki baba!
 
kweli mzee chenge umeamua. Kila la heri
 
Siku 90 watatatoka tu.Nape ndiyo kiboko yao...watakoma
Acha ndoto za mchana wewe. Muulize Nape kama ana ubavu tena hata wa kuongea kuhusu mafisadi. Ameshapewa karipio kali na Bw. mkubwa nguvu atazitoa wapi tena? Mafisadi wataendelea kutesa kwa raha zao!!!
 

Kumbuka! ni mwanasheria si mchumi. Wacha upupu. Hizo sheria alizowashauri ndio leo zimefikisha hizo fedha kurudishwa. Angeweka madudu kwenye sheria hizo fedha ungesikia zinarudi? Fikiri, japo kidogo.
 
Mkuu unamtajia Tanzania daima unafikiri anasoma hilo gazeti huyu?huyu katumwa hapa special kwa kazi maalumu.
 
Hapa kuna tatizo.je hana washauri maana bado kashfa a,b,c na d hazijaaisha,au ni dharau?
 
Chenge kaombwa ushauri, mlitaka adanganye? Mna nini nyinyi? Khaaa, mnashangaza.
 
Dada, unafaa kuwa mke wa Nape wallah....maana mnafit kwelikweli!

Bahati mbaya kachelewa kidogo, mimi nna "fisadi" langu nyumbani ambalo hata huyo fisadi wenu akikutana nae anamuamkia. Fisadi wenu si unamjuwa? Yule wa malori used.
 
Jaman watz,kunakila namna na haja ya kukaa chini nakutafakari kwa kina jinsi gani tuweze komboa nchi yetu mikonon mwa hawa wachache wenye kuona nchi ni mali yao waliyorithi!ni mda sasa kila mtz kuweka maslah ya nchi yake mbele na kuachana na ushabiki wa kisiasa usiokuwa na tija!ni ulimbuken wa hali ya juu kuona mtu anashabikia uonevu unaofanywa na wachache kwa maslah yao!ntaita ujinga na upumbavu wa hali ya juu.TUWEKENI MASLAHI YA NCHI MBELE WATANZANIA.Mungu awalaan wote wanaojinufaisha wenyewe kupitia migongo ya watu masikin na wasiojiweza!Mungu tusaidie
 
Chenge amesoma jengo moja na Obama, HARVARD, chuo baba wa dunia, huyu tungemchukua tukampa TAKUKURU aiendeshe, tutawanyonga wangapi? basi tuanze na Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Karume na wote, nina uhakika asilimia 100 viongozi wetu wameiba japo mara 3 kila mmoja, ok Chenge amepokea asante ya dola mil 1, tunamsumbua, na Jeetu Patel amechota Billioni 400 za BOT na sehemu ya pesa hiyo ndio imeanzisha bank yake ya M, huyu anatetewa na Nimrod Mkono ndugu yake Mwalimu Nyerere, sasa fisadi ni nani?

Jamani mi kichwa kinanizunguuka tu. Chenge amenuna sasa apewe TAKUKURU amalizie hasira zake lakini tujue hatapatikana wa kuongoza nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…