Habari wakuu.!
Juzi tulikua ofisi flani hivi ya TRA tunafatilia leseni zetu za gari, sasa tukiwa tunaelekea stand, ikaja V8 moja kali kuna jamaa mmoja hivi wa makamo,akasimama akatusalimia tukaitikia then akatuulza kwamba ""tunakifahamu kiwanda cha chemi cotex?"" tukamuuliza kile cha maeneo ya makonde, akasema ndio, sasa kwa vile na sisi ni wenyeji wa maeneo hayo na tulikua tunapita njia hiyo hiyo tukasema tuende nae, tukakwea, tulipofika maeneo yale akasema kuna hela nalipa kwa mkurugenzi wa kiwanda ili anipelekee products zake k/koo akalipa then tukaamsha jamaa alikua anatupigisha story kama kawa anasema yeye anapenda sana vjana wachapa kazi, tulipofika maeneo ya mbuyuni tukamwambia "bro sisi tunaishi salasala kama vp tushushe hapa" akasema poa,sasa mda tunataka kushuka akachukua simu yangu akasema ngoja niwaandikie namba yangu ili siku nyingine tunaweza kufanya hata biashara tukasema poa halafu akatupa hela ya boda boda elfu 40 sasa jana akanipigia simu anasema njooni ofisin kwangu, nikamuuliza kuna nn brother, akasema natafta vijana wa kazi afu mje na vyeti vyenu, nikamwambia kwamba mimi ndo kwanza nimemaliza form six juzi sina cheti, akasema hata leaving njoo nayo, nikamshitua mshikaj wangu tukaenda, tulipofika tukaingia ofisin kwake tukaa, sasa cha kushangaza tulimkuta yupo kifua wazi na kibukuta akainuka akaja akaanza kufungua zipu yangu, nikamsukuma, akaniambia nitawapa laki tano kila mtu, nataka mnifire,! Shit, nikamwambia siku nyingine, tukawa tumeondoka nilipofka home nikampigia simu nikamwambia huo ushenzi siwezi kufanya,. Kukaa kidogo akatuma laki mbili na 20 tigo pesa, nikamwambia sihitaji pesa kwa ujinga huo. Sasa leo nimebadilisha namba kwaajili ya huyu jamaa. Sasa mimi bado najiuliza inakuaje mtu mpk anakuwa shoga jaman maana kwa jinsi jamaa alivyo he looks like a real man kumbe ni gay, aise nawasihi vijana wenzangu tusishawishike kufanya upuuzi kama huo kwasababu tu ya hela, tulizike na vidogo tulivyo navyo.!
Mtanisamehe kwa thread ndefu.