Airtel kwa hili mtapoteza wateja

Airtel kwa hili mtapoteza wateja

dada white

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
1,228
Reaction score
515
Moja ya kitu ambacho kilikuwa kinavutia vijana kununua line za airtel na kuachana na dhana iliyozoeleka kuwa airtel ni mtandao wa watu walionazo tu hapa Tz ni ile bundle yenu ya MB400 kwa siku 30 ambayo ilikuwa ikiuzwa kwa sh 2500.Naona hii bundle imebadilika bei na kuwa ya ni Tsh3500 kwa siku 10 tu na unapewa MB500.Kwa mchanganuo ina maanisha mtu anatumia Tsh 350 kwa siku hii kitu ni gharama sana hasa kwa watu wenye kipato cha chini.Kwa kulinganisha ni kifurushi cha extrema park cha tigokinakuwa kina faida sana kwa maana unapata sms zaidi ya 100,dakika 15,Mb50 kwa masaa 24.Kwa kweli airtel mtatufukuza wengi kwa ongezeko hili.Kile kifurushi chenu kilikuwa kina induce watu wanunue line zenu. Mi mwenyewe mtanikosa kwa kweli
 
wana jf.
mnapigia promotion makampuni ya cm au ndio mnawakirisha kero zenu ?. . .
 
Mi nimeamia zantel mb150
sh1500 kwa mwezi piga *149*07#.

Niliwahi kusema kuwa zantel bei zao ni nafuu mkanitukana mara promo, manager masoko@kazini, sasa naona mnajimuvizisha amia zanitel.
 
Zantel ni better kuliko hao wengine,hata kwenye speed haina mpinzani,Ile bronze package ni 600 mb kwa mwezi mzima,sh 4000 tu.
 
Wanatuchezea michezo!badala wafikilie kufanya mb500 kwa sh 2500 wao ndo kwanza wanfanya mb500 kwa sh 2500 kwa siku 10.upuuzi mtupu.alafu mtandao yenyewe hauna speed.
 
S.L.B ndio nn tena!? Weka wazi.
Kwa upande TTCL Broadband wako bomba lakini wbado wanafanya biashara kimazoea. 2GB Bundle wanauza 30,000 wakati Zantel kwa 20,000 kunapata 5GB. Ila hata Hivyo tunaibiwa sana ss watanzania. Garama halisi za Mtandao hatakiwi kuzidi 10,000 kwa Bundle ya 1GB kwa Mwezi. Lakini kwa vile tunahitaji Taarifa za kimtandao ndio maana tunalazimika kukubali kunyonywa.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
wana jf.
mnapigia promotion makampuni ya cm au ndio mnawakirisha kero zenu ?. . .

Kwani we unaonaje? Haiwezekani tukazungumzia kero ya kampuni fulani ya simu bila kufananisha na unafuu wa kampuni nyingine.Acha kukariri kila kitu ni tangazo mkuu.
Jifunze ku Take easy kwenye mambo madogo madogo
 
Back
Top Bottom