Airtel Huu Mnaofanya Sasa ni Unyang'anyi.

Airtel Huu Mnaofanya Sasa ni Unyang'anyi.

Mchokoo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2015
Posts
1,188
Reaction score
1,604
Nimekuwa nikisikia watu wakilalama yako wewe Airtel ila sikuwahi kuwaza kuwa hali ni mbaya kiasi hiki.

Jamani nimeweka buku kununua bando la internet toka kwako, ndiposa nikawa nasubiri sms ya kuunganishwa.

Mweeee!!

Kama si unyang'anyi sasa kumbe hii ni nini ndugu zangu?

Wakati napokea ujumbe wa kuunganishwa katika KIFURUSHI hicho; ni hapohapo napokea tena ujumbe mwingine toka kwako wewe usemao kuwa umetumia asilimia 90 ya KIFURUSHI chako! ilihali mimi ndio kwanza nimewasha data!!!!!!
Tafadhari Airtel rudisha buku langu haraka kabla hujanikwaza zaidi.
SMS zako nimezituza, muda wake uko wazi mno! na nimeona zinatofautiana dk 2 tu ingawa kwa kweli ziliingia pamoja!!
Basi tukubali hiyo tofauti ya dk 2 ila najiuliza kweli ndani ya dakika mbili MTU anaweza kutumia asilimia 90 ya KIFURUSHI cha buku kwenye simu ya mkononi?
 
Pole, tafuta mbadala mapema. Juzijuzi tu kifurushi cha buku moja kwa siku sasa unapata 400mb badala ya 1gb. Kama unatokea mjini posta, vuka mataa ya moroco kuelekea mwenge, kabla ya victoria kuna watoa bando wapya na nafuu kwa bei hiyo waone haraka sana ufurahie maisha mapya na kuacha kusumbua kichwa.
 
Back
Top Bottom