Posho ni janga la Taifa. Mimi nafahamu kwamba kuna Mbunge Mmoja tu ambaye amezikataa posho za vikao naye ni ZZK wa CDM. Hakuna mbunge mwingine (labda January wa CCM) ambaye amezikataa posho. Watu wanaongea kinafiki tu kwamba posho za vikao hatuzitaki na ni sera yetu kuzikataa lakini hawaonyeshi kwa vitendo. Suala la posho limejaa unafiki mwingi sana. Afadhali hata huyo Serukamba na Shibuda wanaonyesha misimamo yao hadharani kwamba wanazitaka na ziongezwe kuliko wanafiki ambao wanajifanya hawazitaki eti ni sera ya chama lakini wanazila. Mimi ningefurahi sana kama wabunge wote wa CDM wangesusia posho kama Zitto ili kutekeleza hiyo sera yao, lakini wapi linapofika suala la posho wabunge wengi wa CDM wanakuwa wanafiki wakubwa. Jamani kama ni sera ya CDM si utolewe uamuzi wa chama kwamba hakuna kuchukua posho kwa kuwa hiko ni kuwaibia wananchi na atayechukua posho anagutwa chamani. Lakini kwa kuwa wengi ni pro posho, uamuzi kama huo hauwezi kufikiwa. POSHO NI JANGA LA TAIFA NDANI YA CCM NA CDM.
Mkuu mimi nilikuwa na maana kwamba wabunge wanaosema wanapinga posho waache unafiki wapinge kwa vitendo kama Zitto kuliko wanavyojificha ndani ya pazia la eti ni sera ya Chama lakini hawaitekelezi kwa vitendo. Na wanaoshabikia kama akina Serukamba nao wajitokeze hadharani na hata kwa hoja (najua haipo) na wananchi wawajue kwamba hawa ni makamanda wa posho. wanaozipinga wazikatae kwa vitendo, kama Zitto ameweza wao wanashindwa nini kwani wao wana nini?Hakuna afadhali mpolaji ni mpolaji .... kutokuwa na unafiki kuna saidia nini kukwepa hayo matumbo yao yenye njaa....... NENO UNAFIKI linatupeleka kubaya, kama kuna kosa ni kosa... lisemwe kama lilivyo, hayo mengi tuyaachie makanisa/misikiti wayafanya hatuko kwenye usafi wa roho [ kwenye mbinguni] , haki ndio msingi tunaotaka kujenga kwa ghalama yoyote ile
Peter Serukamba ni mbunge wa Kigoma Ujiji,na ni mjumbe wa NEC ya CCM, ni krimu ya siasa za Kijani na ni sura ya Ujana ya CCM,
Wakati taifa na wanamageuzi kwa ujumla wakipambana kukemea ukwasi tata wa Bunge letu chini ya Mama Makinda aka Bibi Kiroboto, Serukamba kupitia mtandao wa kijamii wa twita @serukamba bila haya wala kihoro, apambana waziwazi na wapinga posho kwa kusema "Kama Bunge haliongezi POSHO basi Bunge lifutwe!
Kwa maneno hayo tu, mimi binafsi namuona ni janga la kitaifa na lisiposhughulikiwa litaliangamiza taifa!
Kumbuka kila aliye mtz na alipae kodi ya haki basi kodi hiyo hutumiwa ikiwa ni pamoja na kuwalipa posho za kukaa bungeni wabunge na watumishi wengine, hivyo dhana ya Serukamba kuwa wengi wawanaopiga ukelele wa kupinga posha hasa kwake yeye hawamsaidii kwani hawakumchagua na hawatamchagua!
Hata kama mimi si mbunge naweza kuunga mkono suala la wabunge kulipwa vizuri zaidi (si lazima kwa njia ya posho ya vikao). Nianze kwa mambo mawili: Kwanza, kwa jinsi nilivyofuatilia suala hili, si kweli kwamba wabunge wanaoshabikia posho ni wa CCM tu. Asilimia 90 ya wabunge wa Chadema wanataka sana hizo posho, isipokuwa wengi wao wanawaogopa kama chui viongozi wao wakuu wanaopinga posho hizi. Pili, kusema kwamba wabunge wakafanye kazi walizotumwa na wapigakura wao, badala ya kudai posho ni kutojua kwamba wabunge hawana job description maalum ya kazi zao. Wabunge hawa wakishachaguliwa, kila jambo jimboni kwao ni kazi yao - kuanzia ufuatiliaji wa utekelezaji wa ahadi za serikali na za kwao wenyewe, kufuatilia kero za wananchi za aina yoyote ile, kusaidia wananchi kwa shida zao za kijamii (kama michango kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi, ujenzi na misaada ya makanisani na misikitini, misaada ya michezo na burudani) na shida binafsi za wananchi kama magonjwa, elimu ya watoto, michango ya misiba na harusi. Nilivyofuatilia wabunge wote wanaopinga posho hizi (kutoka CCM na upinzani) ni wale wabunge matajiri na wafanyabiashara kama vile Mbowe, Mohamed Dewji, Mkono, Ndensamburo n.k. na pia wabunge wanaopata misaada kwenye NGOs zao kama vile Zitto anayepata hela nyingi toka kwa wafadhili (Ujerumani) na chinichini kutoka kwa viongozi wa mashirika ya Umma wanaomwogopa kama mkt wa POAC, na wengine wenye NGOs kama January n.k. Hawa wana vyanzo vizuri tu vya kuhudumia majimbo yao kwa shida zote za wananchi. Lakini kwa wabunge wanaotegemea malipo ya Bunge tu wana hali mbaya sana. Na bahati mbaya, wananchi na viongozi wa dini mnaolaumu suala la posho ndio wa kwanza kuleta kadi za michango kwa wabunge. Mimi ningependekeza kwamba badala ya posho, wabunge wangelipwa tu mishahara mikubwa kama milioni kumi kwa mwezi. wala sitaweza kuwaonea wivu hata kama mimi mshahara wangu ni kiduchu. Wana majukumu makubwa. Wala simlaumu Serukamba kwa msimamo wake huo.
Bila kumsahau Ndugai, na makinda
Hata kama mimi si mbunge naweza kuunga mkono suala la wabunge kulipwa vizuri zaidi (si lazima kwa njia ya posho ya vikao). Nianze kwa mambo mawili: Kwanza, kwa jinsi nilivyofuatilia suala hili, si kweli kwamba wabunge wanaoshabikia posho ni wa CCM tu. Asilimia 90 ya wabunge wa Chadema wanataka sana hizo posho, isipokuwa wengi wao wanawaogopa kama chui viongozi wao wakuu wanaopinga posho hizi. Pili, kusema kwamba wabunge wakafanye kazi walizotumwa na wapigakura wao, badala ya kudai posho ni kutojua kwamba wabunge hawana job description maalum ya kazi zao. Wabunge hawa wakishachaguliwa, kila jambo jimboni kwao ni kazi yao - kuanzia ufuatiliaji wa utekelezaji wa ahadi za serikali na za kwao wenyewe, kufuatilia kero za wananchi za aina yoyote ile, kusaidia wananchi kwa shida zao za kijamii (kama michango kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi, ujenzi na misaada ya makanisani na misikitini, misaada ya michezo na burudani) na shida binafsi za wananchi kama magonjwa, elimu ya watoto, michango ya misiba na harusi. Nilivyofuatilia wabunge wote wanaopinga posho hizi (kutoka CCM na upinzani) ni wale wabunge matajiri na wafanyabiashara kama vile Mbowe, Mohamed Dewji, Mkono, Ndensamburo n.k. na pia wabunge wanaopata misaada kwenye NGOs zao kama vile Zitto anayepata hela nyingi toka kwa wafadhili (Ujerumani) na chinichini kutoka kwa viongozi wa mashirika ya Umma wanaomwogopa kama mkt wa POAC, na wengine wenye NGOs kama January n.k. Hawa wana vyanzo vizuri tu vya kuhudumia majimbo yao kwa shida zote za wananchi. Lakini kwa wabunge wanaotegemea malipo ya Bunge tu wana hali mbaya sana. Na bahati mbaya, wananchi na viongozi wa dini mnaolaumu suala la posho ndio wa kwanza kuleta kadi za michango kwa wabunge. Mimi ningependekeza kwamba badala ya posho, wabunge wangelipwa tu mishahara mikubwa kama milioni kumi kwa mwezi. wala sitaweza kuwaonea wivu hata kama mimi mshahara wangu ni kiduchu. Wana majukumu makubwa. Wala simlaumu Serukamba kwa msimamo wake huo.
Hayo ni mawazo yangu, na hayo no mawazo yako....Lakini kama ni semina, itabidi na wananchi na wanajamii (wapiga kura) nasi tupigwe msasa kuhusu suala hili.Red; Hiyo ndo job description unayodai hawana mkuu......ukitoa maneno ya aina yoyote ile...........
Blue; Hayo hata sisi tunafanya kwa uwezo wetu mdogo, cha maana wasimamie sera huko bungeni (hujasikia au kuona physical violence kwenye mabunge ya wenzetu????) as mengine( regarded monetory aids) ni majukumu ya serikali na wala si ya mbunge thus hata ukimpa posho ya 1M kwa siku still tatizo litakuwepo bcoz system itakuwa ni ile ile na wapiga kura watabaki hao hao with poor living quality and bulging quantity
Yellow; Hiyo ndo inaitwaga innovative and sustainable trouble shooting mode sio kutoa hoja ya kuongezwa posho.....waandaliwe semina on how to prepare sustainable projects kama wenzao
Green; Hapo ndo mkwamo unapoanzia sasa tena usirudie kuwaweka wazi this much kama anategemea bunge kwa kila kitu huyu ni hatari sana kwa jimbo na taifa......yeye analifanyia nini jimbo na taifa??? Ile dhana ya kulifanya taifa kuwa la kujitegemea haitafanikiwa kama tutaendelea kukumbatia mawazo tegemezi kama haya; Wafundishwe/ wajifunze kuvua na sio kupewa samaki wengi kila wanapokosa kitoweo.......!!!!!!!!!
Black; Attitude tegemezi hiyo.....umeanza na kusema watu wanasaidiwa sana na wabunge ndo maana kuna haja ya wabunge waongezewe posho n yet huoni sababu ya kuwezeshwa hao wala wewe?? ili mbaki kuwa omba omba kwa hao wabunge au??.....wakilipwa milioni kumi nan kakuhadithia kwamba itakuwa suluhu ya hizo changamoto ulizoorodhesha???
Ronaldo kwa kusoma tu mawazo yako nimegundua una mawazo mgando, huna tofauti na viongozi wa ccm walioshindwa kuwaletea wananchi maendeleo kwa rasilimali zilizopo na sasa wanategemea misaada toka nje huku wakiacha rasilimali zikivunwa bure na wawekezaji mabeberu..Hayo ni mawazo yangu, na hayo no mawazo yako....Lakini kama ni semina, itabidi na wananchi na wanajamii (wapiga kura) nasi tupigwe msasa kuhusu suala hili.
Hayo ni mawazo yangu, na hayo no mawazo yako....Lakini kama ni semina, itabidi na wananchi na wanajamii (wapiga kura) nasi tupigwe msasa kuhusu suala hili.
Serukamba ni mtu asiyekuwa na msimamo; ni bodyguard wa Lowassa na ndiko anakopata fedha nyingi za kuhonga ili agenda za Lowassa ziweze kufanikiwa!!
Hata kama mimi si mbunge naweza kuunga mkono suala la wabunge kulipwa vizuri zaidi (si lazima kwa njia ya posho ya vikao). Nianze kwa mambo mawili: Kwanza, kwa jinsi nilivyofuatilia suala hili, si kweli kwamba wabunge wanaoshabikia posho ni wa CCM tu. Asilimia 90 ya wabunge wa Chadema wanataka sana hizo posho, isipokuwa wengi wao wanawaogopa kama chui viongozi wao wakuu wanaopinga posho hizi. Pili, kusema kwamba wabunge wakafanye kazi walizotumwa na wapigakura wao, badala ya kudai posho ni kutojua kwamba wabunge hawana job description maalum ya kazi zao. Wabunge hawa wakishachaguliwa, kila jambo jimboni kwao ni kazi yao - kuanzia ufuatiliaji wa utekelezaji wa ahadi za serikali na za kwao wenyewe, kufuatilia kero za wananchi za aina yoyote ile, kusaidia wananchi kwa shida zao za kijamii (kama michango kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi, ujenzi na misaada ya makanisani na misikitini, misaada ya michezo na burudani) na shida binafsi za wananchi kama magonjwa, elimu ya watoto, michango ya misiba na harusi. Nilivyofuatilia wabunge wote wanaopinga posho hizi (kutoka CCM na upinzani) ni wale wabunge matajiri na wafanyabiashara kama vile Mbowe, Mohamed Dewji, Mkono, Ndensamburo n.k. na pia wabunge wanaopata misaada kwenye NGOs zao kama vile Zitto anayepata hela nyingi toka kwa wafadhili (Ujerumani) na chinichini kutoka kwa viongozi wa mashirika ya Umma wanaomwogopa kama mkt wa POAC, na wengine wenye NGOs kama January n.k. Hawa wana vyanzo vizuri tu vya kuhudumia majimbo yao kwa shida zote za wananchi. Lakini kwa wabunge wanaotegemea malipo ya Bunge tu wana hali mbaya sana. Na bahati mbaya, wananchi na viongozi wa dini mnaolaumu suala la posho ndio wa kwanza kuleta kadi za michango kwa wabunge. Mimi ningependekeza kwamba badala ya posho, wabunge wangelipwa tu mishahara mikubwa kama milioni kumi kwa mwezi. wala sitaweza kuwaonea wivu hata kama mimi mshahara wangu ni kiduchu. Wana majukumu makubwa. Wala simlaumu Serukamba kwa msimamo wake huo.
Nakubaliana na wewe kabisa! Tatizo je hawa wanaolia waongezewe posho ukigusa kuwa jamanie achieni ubunge kama posho ni ndogo!Suala la posho halihitaji mjadala Mhe. Mbunge, zifutwe kabisa. Kumbuka kwamba wabunge wanalipwa pesa (elfu 70) hizo kwa kila kikao kimoja, akikaa vikao vitatu tu ni mshahara wa mwalimu wa gredi 3A anayeanza kazi. By the way, hakuna mtu anayelazimishwa kuwa mbunge, ambaye haridhiki na posho iliyopo awaachie wenye kujitolea. Nukta.
Huwezi kuamini, hata Tundu Lisu na Uroho wake anataka posho ziongezwe!Peter Serukamba ni mbunge wa Kigoma Ujiji,na ni mjumbe wa NEC ya CCM, ni krimu ya siasa za Kijani na ni sura ya Ujana ya CCM,
Wakati taifa na wanamageuzi kwa ujumla wakipambana kukemea ukwasi tata wa Bunge letu chini ya Mama Makinda aka Bibi Kiroboto, Serukamba kupitia mtandao wa kijamii wa twita @serukamba bila haya wala kihoro, apambana waziwazi na wapinga posho kwa kusema "Kama Bunge haliongezi POSHO basi Bunge lifutwe!
Kwa maneno hayo tu, mimi binafsi namuona ni janga la kitaifa na lisiposhughulikiwa litaliangamiza taifa!
Kumbuka kila aliye mtz na alipae kodi ya haki basi kodi hiyo hutumiwa ikiwa ni pamoja na kuwalipa posho za kukaa bungeni wabunge na watumishi wengine, hivyo dhana ya Serukamba kuwa wengi wawanaopiga ukelele wa kupinga posha hasa kwake yeye hawamsaidii kwani hawakumchagua na hawatamchagua!